Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Na Restuta James

Jumla ya Sh. bilioni 75.2 zimelipwa na serikali kwa kampuni ya Richmond/ Dowans kama malipo ya kuweka mitambo nchini (capacity charge), kati Desemba, 2006 na sasa.


Najua mimi sijui hesabu sana lakini hizi za "MAGAZIJUTO" nazijua kidogo..

FEDHA ZILIZOIBWA BOT = 133 BILIONI
FEDHA ZILIZORUDISHWA = 50 BILIONI
SALIO = 83 BILIONI

FEDHA ZA DOWANS ZILIZOLIPWA NA SERIKALI = 75 BILIONI

JUMLA YA FEDHA ZILIZOIBWA NA ZILIZOLIPWA NA HAZIKO MIKONONI MWA WATANZANIA = 158 BILIONI

Tukichukulia fedha zilizorudisha na kutoa zile ambazo zimelipwa kwa Dowans = 75 - 50 - 25 BILLIONI

HIVYO BASI, Hesabu zinatuonesha kuwa shilingi bilioni 50 ambazo zimerudishwa kufuatia wizi wa EPA zinafuta furaha yoyote kwani wakati huo huo tumelipa shilingi bilioni 75 kwa kampuni isiyokuwa na Mkataba na bado tunadaiwa shilingi bilioni 25!

Kwa msingi huo; hadi pale fedha za EPA zitakaporudishwa kufikia Bilioni 75 tutakuwa even, na chochote zaidi ya hapo tutakuwa tumekaribia kurudisha deni.

Na endapo fedha zote za EPA (Bilioni 133) zitarudishwa tutakuwa even kwenye EPA na kuendelea kubakiwa na deni lisilolalazima la BILIONI 75! na zaidi kwani bado tunaendelea kulipa.

Lakini kuna jambo jingine linaloshtua:

Bilioni 75 zikigawanywa kila siku kuanzia Disemba 2006 hadi Februari 29 mwaka huu tunajikuta tunalipia shilingi 164,473,684.2 kwa siku... hii inakaribiana na ile namba ya Dr. Mwakyembe (plus or minus).

Sasa kwa vile tunaendelea kulipa kila siku kiasi hicho ina maana ya kwamba kwa mkono mmoja tunapokea, na kwa mikono miwili tuna toa.. je hili ni Taifa la vichaa!!?
 
Na Restuta James

Jumla ya Sh. bilioni 75.2 zimelipwa na serikali kwa kampuni ya Richmond/ Dowans kama malipo ya kuweka mitambo nchini (capacity charge), kati Desemba, 2006 na sasa.


Najua mimi sijui hesabu sana lakini hizi za "MAGAZIJUTO" nazijua kidogo..

FEDHA ZILIZOIBWA BOT = 133 BILIONI
FEDHA ZILIZORUDISHWA = 50 BILIONI
SALIO = 83 BILIONI

FEDHA ZA DOWANS ZILIZOLIPWA NA SERIKALI = 75 BILIONI

JUMLA YA FEDHA ZILIZOIBWA NA ZILIZOLIPWA NA HAZIKO MIKONONI MWA WATANZANIA = 158 BILIONI

Tukichukulia fedha zilizorudisha na kutoa zile ambazo zimelipwa kwa Dowans = 75 - 50 - 25 BILLIONI

HIVYO BASI, Hesabu zinatuonesha kuwa shilingi bilioni 50 ambazo zimerudishwa kufuatia wizi wa EPA zinafuta furaha yoyote kwani wakati huo huo tumelipa shilingi bilioni 75 kwa kampuni isiyokuwa na Mkataba na bado tunadaiwa shilingi bilioni 25!

Kwa msingi huo; hadi pale fedha za EPA zitakaporudishwa kufikia Bilioni 75 tutakuwa even, na chochote zaidi ya hapo tutakuwa tumekaribia kurudisha deni.

Na endapo fedha zote za EPA (Bilioni 133) zitarudishwa tutakuwa even kwenye EPA na kuendelea kubakiwa na deni lisilolalazima la BILIONI 75! na zaidi kwani bado tunaendelea kulipa.

Lakini kuna jambo jingine linaloshtua:

Bilioni 75 zikigawanywa kila siku kuanzia Disemba 2006 hadi Februari 29 mwaka huu tunajikuta tunalipia shilingi 164,473,684.2 kwa siku... hii inakaribiana na ile namba ya Dr. Mwakyembe (plus or minus).

Sasa kwa vile tunaendelea kulipa kila siku kiasi hicho ina maana ya kwamba kwa mkono mmoja tunapokea, na kwa mikono miwili tuna toa.. je hili ni Taifa la vichaa!!?
 
Najua mimi sijui hesabu sana lakini hizi za "MAGAZIJUTO" nazijua kidogo..

FEDHA ZILIZOIBWA BOT = 133 BILIONI
FEDHA ZILIZORUDISHWA = 50 BILIONI
SALIO = 83 BILIONI

FEDHA ZA DOWANS ZILIZOLIPWA NA SERIKALI = 75 BILIONI

JUMLA YA FEDHA ZILIZOIBWA NA ZILIZOLIPWA NA HAZIKO MIKONONI MWA WATANZANIA = 158 BILIONI

Tukichukulia fedha zilizorudisha na kutoa zile ambazo zimelipwa kwa Dowans = 75 - 50 - 25 BILLIONI

HIVYO BASI, Hesabu zinatuonesha kuwa shilingi bilioni 50 ambazo zimerudishwa kufuatia wizi wa EPA zinafuta furaha yoyote kwani wakati huo huo tumelipa shilingi bilioni 75 kwa kampuni isiyokuwa na Mkataba na bado tunadaiwa shilingi bilioni 25!

Kwa msingi huo; hadi pale fedha za EPA zitakaporudishwa kufikia Bilioni 75 tutakuwa even, na chochote zaidi ya hapo tutakuwa tumekaribia kurudisha deni.

Na endapo fedha zote za EPA (Bilioni 133) zitarudishwa tutakuwa even kwenye EPA na kuendelea kubakiwa na deni lisilolalazima la BILIONI 75! na zaidi kwani bado tunaendelea kulipa.

Lakini kuna jambo jingine linaloshtua:

Bilioni 75 zikigawanywa kila siku kuanzia Disemba 2006 hadi Februari 29 mwaka huu tunajikuta tunalipia shilingi 164,473,684.2 kwa siku... hii inakaribiana na ile namba ya Dr. Mwakyembe (plus or minus).

Sasa kwa vile tunaendelea kulipa kila siku kiasi hicho ina maana ya kwamba kwa mkono mmoja tunapokea, na kwa mikono miwili tuna toa.. je hili ni Taifa la vichaa!!?


Na hiki ndicho ambacho mafisadi wanajaribu sana kufukia ili watu wasione hii hesabu na huu usanii unaofanywa huko serikalini.
 
Mojawapo ya vitu vinavyoendelea kunishangaza siku hizi zote ni kwanini serikali yetu inajiuma uma kuvunja mkataba na Dowans. Hili halipaswi kuwa hivyo.

a. Imeweza kuthibitishwa kuwa kampuni iliyoingia Mkataba na Tanesco ya Richmond Development Company LLC haijawahi kusajiliwa Tanzania na haikupewa kibali cha uwekezaji.

b. Imeweza kuthibitishwa kupitia Kamati Teule ya Bunge hiyo kampuni yenyewe haipo jinsi ilivyotajwa na kimsingi ni kampuni hewa.

Hivyo kutokana na hayo mawili tu kuna mambo kadhaa ambayo tunaweza kuona yanafuatana.

1. Kanuni za kuingia mikataba zina presume mambo makubwa matatu; kwanza, anayeingia mkataba yupo, pili, aneyeingia mkataba ana uwezo wa kisheria kufanya hivyo, tatu anayeingia mkataba anafanya hivyo kiuaminifu kuwa ataweza kuutekeleza.

2. Kwa vile tumeshaona hapo juu kuwa aliyeingia mkataba wa Richmond hakuwepo na hakuwa na nguvu za kufanya hivyo basi kile kilichoingiwa hakiwezi hata chembe kuwa mkataba.

3. Mkataba unaoingiwa kiudanganyifu (fraudelent) siyo mkataba halali.

Kwa vile Kamati Teule ya Bunge imeweza kuthibitisha pasipo shaka kuwa Mkataba wa Richmond uliingiwa kwa njia ya udanganyifu na kampuni ambayo haipo na isiyo na uwezo wa kuingia mkataba huo hivyo HAKUNA KITU KAMA MKATABA WA RICHMOND kwa sababu huwezi kuingia Mkataba na kampuni ambayo HAIPO.

Kanuni hii ndiyo inaongoza hata annulments za ndoa kwamba endapo mtu anaingia kwenye ndoa (mkataba) kwa njia ya udanganyifu au pasipo uhalali wa kufanya hivyo (kama ndoa ya baba na binti) basi ndoa hiyo inaweza kuwa annulled (maana yake siyo tu inafutwa, bali haikuwepo in the first place)

4. Kwa vile kampuni ya Richmond haipo, na kwa vile mkataba wenyewe nao haupo basi Dowans hawawezi kurithi kitu ambacho HAKIPO.

Hivyo, serikali haihitaji kwenda mahali popote ni kuwaambia Dowans park your stuff and leave kwa sababu HAKUNA mkataba kati yako na TANESCO. Hili halihitaji uwe mtaalamu wa fizikia kuweza kuliona.

Sio watimuliwe tu bali pia warudishe pesa zote walizolipwa mpaka leo hii pamoja na wale richmond au assets zao zote zichukuliwe na SK kisha ziuzwe na kitakachopatikana kiingizwe kwenye mfuko wa hazina.
 
MAKAMPUNI ya kuzalisha umeme ya Richmond na Dowans yanamilikiwa na mtu mmoja, MwanaHALISI limegundua.

Vyanzo mbalimbali vya taarifa ndani ya serikali vimekiri pia kwamba hayo ni makampuni ya mfanyabiashara mmoja mashuhuri raia wa Tanzania.

http://halihalisi.co.tz/08/05/14/


haya sasa makubwa kumbe anaeturamba ni mtanzania mwenzetu katunzunguka toka Richmond na kuja Dowans ni nani?

mbona hawajamtaja au ni majungu na sasa wanaogopa
 
Lisemwalo lipo kama halipo laja. wewe subiri tu. hata ufisadi ulianza kufunuliwa hivi hivi!!!!
 
Ni Mtanzania, kiongozi wa CCM
Hoseah kung’olewa TAKUKURU
Akina Karamagi wachunguzwa
Toleo Na. 097
Serikali yafichua kigogo wa Dowans
Na Saed Kubenea
MAKAMPUNI ya kuzalisha umeme ya Richmond na Dowans yanamilikiwa na mtu mmoja. Taarifa ndani ya serikali imekiri pia kwamba hayo ni makampuni ya mfanyabiashara mmoja mashuhuri raia wa Tanzania... CCM na CUF kamilisheni kazi mloianza
Tahariri
MAZUNGUMZO ya kutafuta muwafaka kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF) yanaendelea kukwama. Kukwama kwa mazungumzo hayo kumetokana na misimamo iliyowekwa na vyama hivi...
Hatimaye Stella amfikia Waziri Mkuu
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda ameingia kijijini Ubungo Msewe kwa kutaka ripoti kamili ya ufuatiliaji tuhuma mbalimbali zilizofikishwa kwake, MwanaHALISI imefahamishwa...
‘Kochonkocho’ dhidi ya ufisadi
Na Ndimara Tegambwage
WIKI iliyopita kulikuwa na taarifa katika vyombo vya habari juu ya vijana waliokamatwa kwa madai ya “kumtukana” rais mstaafu Benjamin Mkapa. Lakini habari hizo hazikusema ni matusi yapi alitukanwa...
Hujuma yaua Shirila la Bima
Na Iddy Mkwama
HABARI za kuwapo ufisadi uliokithiri ndani ya Shirika la Bima la Taifa (NIC), si ngeni na hazishangazi kwa wengi hasa wale wanaofuatilia mwenendo wa shirika hilo...
Ya Chenge yathibitisha CCM chama genge
NI lazima uwe na shahada ya falsafa ili ukielewe vema Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kadri siku zinavyokwenda ndivyo mambo yanavyozidi kudhihirisha kwamba chama tawala ni dude lisiloweza kueleweka...
Polisi wakigoma itakuwaje?
Na Ndimara Tegambwage
NANI anataka kuona askari polisi na askari magereza wakifanya maandamano na migomo wakidai serikali iwasikilize na kuwalipa mishahara inayolingana na kazi yao? Nani?
Masebu: EWURA ni marefa uwanjani
ANAKABILIWA na changamoto nyingi kama msomi binafsi, ila ana changamoto mahsusi kama kiongozi wa taasisi nyeti. Wala hakujua angeongoza moja ya taasisi alizoziakisi baada ya kutakiwa kubuni mfumo mpya wa uendeshaji mamlaka za kusimamia utoaji huduma kwa umma...
Wapelelezi wa SFO waiumbua TAKUKURU
Na Stanislaus Kirobo
HAKUNA ubishi kuwa “ufisadi” ni neno lililochukua nafasi kubwa zaidi magazetini katika awamu hii ya uongozi wa nchi kuliko huko nyuma...
Rais Kikwete sasa aendeleza ‘mduara’
Na Saed Kubenea
RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya tano ya Baraza la Mawaziri tangu ashike madaraka ya kuongoza nchi, takribani miaka miwili na nusu iliyopita...
Karume aliyakimbia Mapinduzi
Na Joseph Mihangwa
NIMEPOKEA maswali mengi na hoja mbalimbali kutoka kwa wasomaji wa gazeti hili kutokana na makala yangu iliyochapishwa katika toleo la 30 Aprili 2008 iliyobeba kichwa cha habari kisemacho: “Karume na zimwi la Mapinduzi”...
Siasa-mzaha zinazidisha tu mgogoro Zanzibar
INASIKITISHA sana kuona jitihada zilizochukuliwa na vyama viwili hasimu katika siasa za Zanzibar, zimeishia...
Si bure, Manji ana lake Yanga
"Si Bure, Yussuf Manji ana lake Yanga." Ndivyo ninavyolazimika kuamini kutokana na mambo kadhaa yaliyojitokeza tangu bilionea huyo alipotia mguu Yanga mwaka 2006...Na Saed Kubenea
MAKAMPUNI ya kuzalisha umeme ya Richmond na Dowans yanamilikiwa na mtu mmoja, MwanaHALISI limegundua.

Vyanzo mbalimbali vya taarifa ndani ya serikali vimekiri pia kwamba hayo ni makampuni ya mfanyabiashara mmoja mashuhuri raia wa Tanzania.

Kupatikana kwa taarifa hizo kumefuta madai ya baadhi ya viongozi nchini waliokuwa wakisema kuwa Dowans ni kampuni iliyosajiliwa nchini Costa Rica, Marekani Kusini.

Lakini taarifa zinasema kuwa serikali imethibitishiwa na Mwanasheria Mkuu wa Costa Rica kwamba nchini humo hakuna kampuni inayofahamika kwa jina la Dowans.

Aidha, imefahamika kuwa akaunti za kampuni ya Dowans, ambayo mfanyabiashara Rostam Aziz amewahi kukiri kufahamiana kibiashara na maofisa wake, ziko Dubai, Falme za Nchi za Kiarabu.

Taarifa hizi zimeleta mshangao na maswali mengi, kwani wachunguzi wa mambo wanauliza, kama akaunti ziko Dubai, nani amekuwa akikusanya fedha kila mwezi kwenye dirisha la hazina.

Vyanzo vya habari vya gazeti hili vinasema wafanyakazi wa kampuni ya mfanyabiashara mmoja jijini Dar es Salaam ndio walikuwa wakikusanya fedha hizo.

“Ilifikia mahali kigogo mmoja wa Hazina akawasiliana kwa barua na Ikulu kueleza nani hasa alikuwa anaagiza au kukusanya fedha hizo, na wakati mwingine kuleta rabsha pale anapocheleweshewa malipo,” vimeeleza vyanzo vya habari.

Kupatikana kwa taarifa kuhusu makampuni haya kunaondoa utata, siyo tu juu ya umiliki wake bali pia nani amekuwa akichota mamilioni ya shilingi kutoka hazina kugharimia mradi huu.

Kwa karibu miaka miwili sasa, mmiliki wa makampuni haya amekuwa akikinga Sh. 152 milioni kutoka Hazina kila mwezi kama gharama za mitambo bila kujali kama umeme umezalishwa au haukuzalishwa.

Mkutano wa 12 wa Bunge la Jamhuri unaoanza tarehe 10 mwezi ujao, unatarajia kuelezwa ugunduzi huu wa mmiliki wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda atakapokuwa anatoa taarifa ya serikali ya utekelezaji wa mapendekezo ya Ripoti ya Kamati ya Dk. Harrison Mwakyembe.

Ni katika mkutano huo wa Bunge, Pinda ataorodhesha hatua zilizokwishachukuliwa na serikali katika kutekeleza mapendekezo 23 ya Kamati ya Mwakyembe.

Moja ya hatua ambazo zinatarajiwa kutangazwa ni ile ya serikali kutekeleza maoni ya Kamati ya kumwajibisha Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hoseah.

Taarifa kutoka serikalini zinasema Hoseah ataondolewa kwenye nafasi yake kabla ya Mkutano wa 12 wa Bunge kuanza mjini Dodoma.

Kamati ilipendekeza Hosea awajibishwe kwa sababu alilitia aibu taifa kwa kutoa taarifa potofu kuhusu mkataba kati ya serikali na Richmond.

TAKUKURU ilisema kwamba mkataba wa Richmond haukuwa na matatizo na kwamba serikasli ilikuwa haijapoteza lolote katika kuwa kwenye mkataba huo.

Mwingine ambaye anatarajiwa kung’olewa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Athur Mwakapungu ambaye anaponzwa na kushiriki kwake katika mchakato mzima wa kutoa zabuni kwa Richmond na kuficha ukweli kwa Kamati ya Mwakyembe.

Taarifa zinasema huenda Mwanasheria mkuu wa Serikali Johnson Mwanyika akasalimika kutokana na mfumo wa utendaji ndani ya ofisi yake. Haikuelezwa zaidi.

Hata hivyo imefahamika kuwa baadhi ya watendaji katika ofisi hiyo watawajibishwa kutokana na kushiriki kwao katika mchakato mzima wa mkataba huo.

MwanaHALISI limedokezwa kwamba, kwa sasa serikali inafanya taratibu za kisheria kuona namna ya kusitisha malipo hayo ambayo tafsiri yake ni kuvunja mkataba na Dowans.

Uamuzi huo wa serikali umechochewa na taarifa ya Mwanasheria Mkuu wa Costa Rica kwa Kamati Teule ya Bunge kwamba nchini humo hakuna kampuni inayoitwa Dowans.

Dowans ambayo imekuwa inadaiwa kusajiliwa Costa Rica iliingiza ndani ya nchi mitambo kutokea Afrika Kusini huku akaunti zake zikiwa Dubai.

Katika uchunguzi wake, MwanaHALISI imebaini, serikali kwa kupitia Timu Maalumu (Task Force) iliyoundwa na waziri mkuu, pamoja na mambo mengine, ilipitia mkataba kwa kina na kuona namna ya kusitisha malipo kwa Dowans.

Tayari serikali imefungua akaunti maalum kwa ajili ya kuhifadhi fedha ambazo zingekuwa zinatiririkia kwenye mikono ya Dowans hadi “kieleweke.”

Bunge la bajeti linatarajiwa kuanza Juni 10 huku joto la kisiasa nchini likiwa juu, kufuatia tuhuma mbalimbali za ufisadi na mawaziri kuendelea kujiuzulu kwa tuhuma hizo.

Katika mkutano wa 10, aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa na wenzake Nazir Karamagi na Dk. Ibrahim Msabaha, walijiuzulu kutokana na mkataba wa kifisadi wa Richmond/Dowans.

Hata hivyo, waziri mkuu amethibitisha kuwa viongozi wote waliojiuzulu, wanafuatiliwa kwa makini ili kujua walivyohusika katika kashfa za ufisadi.

Pinda alikuwa akiongea na waandishi wa habari, juzi Jumatatu juu ya hatua za serikali katika kutekeleza mapendekezo ya kamati ya bunge. Alisema fikra za serikali ni kwamba “haitoshi kwa viongozi hao kujiuzulu.”
 
Ni Mtanzania, kiongozi wa CCM
Hoseah kung’olewa TAKUKURU
Akina Karamagi wachunguzwa
Toleo Na. 097
Serikali yafichua kigogo wa Dowans

Mkuu Lunyungu,

Hii copy and paste yako inazoa kila kitu? Kwi kwi kwi!!!!

Usije ukatulisha sumu!
 
haya mazingaombwe mengine ...akaunti imefunguliwa kupokea pesa zilizotakiwa kwenda Dowans?? Nina hofu huenda watu wametengeza kaulaji kiaina hapo?? Vinginevyo hiyo akaunti iwe na maelezo na may be utaratibu ulio wazi wa kui-monitor vinginevyo mnawanyima Dowans wengine wanajipongeza upande wa Pili....Ni noma mazee
 
Ukimaliza kusoma habari yenyewe nafikiri huna haja ya kujiuliza maswala mengi tayari ni meisha pata picha ya mwenye kukusanya mapato ya TANESCO kila mwezi nafikiri kuna haja ya kuturudishia pesa zetu zikiwa pamoja na liba.
 
Kwanza mnisamehe kwa jinsi nilivyo copy .Unajua niko Dar joto na mambo cafe mana nilitaka kuweka urahisi wa watu kusoma .

Mwelekeo wa cinema hii mambo yote ni Rostma lakini JK kasema hashitakiwi mtu na wameachia madaraka yanatosha .Mie nashangaa mambo mengine bwana .
 
lakini kama kweli serikali imefungua A/C ya kuingiza fedha za DOWANS it is Ok ili mpaka kieleweke.
 
Je Raia Mwema walikurupuka kumuomba samahani fisadi Rostam Aziz?
 
MAKAMPUNI ya kuzalisha umeme ya Richmond na Dowans yanamilikiwa na mtu mmoja, MwanaHALISI limegundua.

Vyanzo mbalimbali vya taarifa ndani ya serikali vimekiri pia kwamba hayo ni makampuni ya mfanyabiashara mmoja mashuhuri raia wa Tanzania.

http://halihalisi.co.tz/08/05/14/


haya sasa makubwa kumbe anaeturamba ni mtanzania mwenzetu katunzunguka toka Richmond na kuja Dowans ni nani?

mbona hawajamtaja au ni majungu na sasa wanaogopa

Kwa sababu
(a) Hawana uhakika ni udaku kama kawaida ya press yetu bongo
(b) Ni waoga hii inajulikana kwa waandishi koko
(c) Wanabana kidogo ili wavutiwe vijisenti....typical TZ media
 
june 10 mbona ni keshokutwa!!
tunataka pesa yote iliyochotwa irudishwe......hivi milioni zote hizo kwa mwezi, si afadhali hata tungezikusanya tukasaidia mahospitali!
ufisadi uliofanywa tanzania haujawahi kutokea africa kwengine kokote, manake nchi nyengine anayekula ni mmoja tu, ila tanzania wanaokula ni kila aliyeko madarakani.
hivi tutafika kweli
 
Back
Top Bottom