Double Standard Kuhusu Kauli ya "Zanzibar Sio Nchi!"

Double Standard Kuhusu Kauli ya "Zanzibar Sio Nchi!"

Wanafiki ni viumbe wabaya sana!
Linapokuja suala la Muungano basi utawaona wako sera za CCM! Na kujifanya watu wa karibu saaana na CCM!

Likija suala la Uongozi wa nchi wanavaa yale yale magwanda yao ya CDM!

Hivi huu unafiki utaisha lini!?
 
KUEPUKANA NA KUFUATWA FUATWA NA NZI ONDOA CHAKULA ULICHOBEBA UBAVUNI.

Wazanzibar mmewanyonya vyakutosha na kuwadhulumu kwakiwango kisichoelezeka. Wanataka sasa nchi yao yenye mamlaka kamili nyie mwalalamikia udouble standard wao. Wenye double standard ni sisi watanganyika/serikali isiyotaka kuwaacha wazanzibar na taifa lao.

Kwanini tunaendelea kuwanyonya na kuiharibu Zanzibar yao huku twajifanya eti wao ndio wananufaika? Mnaogopa nini kuwapa taifa lao? Au mnaogopa nchi kuongozwa na sheria za dini ndio maana gharama kubwa yatumika kuulinda muungano/ukoloni kwa wazanzibar?
We utakuwa mzanzibara. Nasubiri muungano ufe tukutimue
 
Hapa ndugu unaimba wimbo moyo wako unapenda kabisa. Hapa nawe umekuwa mwanaCCM kwakuwa inaulinda muungano ambao upo kwa ajili ya kupambana na uislamu kama maelezo yako yanavyojieleza.

Wewe ni CHADEMA damu lakini hapa unaiunga mkono CCM kisa CIA inaisapoti ili kuhakikisha muungano haufi ili kupambana na uislamu usijefanya zanzibar dola ya kidini huoni wewe pia ni double agent mkuu!!? Hapa unajifanya kuibebesha CCM majukumu/responsibility kuwa ndio inajua pekee inachokifanya na kumbe nawe ndio ngoma unapenda CCM iendelee kucheza.

Huu ndio unafiki ambao mimi ninauchukia kwasababu nyie chadema hata serikali tatu mwazitaka kwa makusudio ya kisiasa tu lakini hampo tayari muungano kuvunjwa. Nyie mwataka kuja endeleza utawala wa ki imla kama aliokuwa akiuendesha Nyerere.
Mkuu mimi nazungumzia maslahi ya nchi, sio u-CHADEMA wala u-CCM. Hilo la external influence liko wazi kabisa wala halihitaji speculations! Soma taarifa ya Siri ya CIA juu ya Mapinduzi ya Zanzibar, 1964 in context ndio utaelewa namaanisha nini hapa!
Kwa taarifa yako hata Constitutional Review Commission (CRC) ya akina Warioba walilijadili hili kwa kirefu sana!

Ukweli ndo huo, wewe baki na "CHADEMA/CCM Politics," dunia inaendeshwa kwa underground movements kwa kiasi kikubwa!
 
KUEPUKANA NA KUFUATWA FUATWA NA NZI ONDOA CHAKULA ULICHOBEBA UBAVUNI. Wazanzibar mmewanyonya vyakutosha na kuwadhulumu kwakiwango kisichoelezeka. Wanataka sasa nchi yao yenye mamlaka kamili nyie mwalalamikia udouble standard wao. Wenye double standard ni sisi watanganyika/serikali isiyotaka kuwaacha wazanzibar na taifa lao. Kwanini tunaendelea kuwanyonya na kuiharibu zanzibar yao huku twajifanya eti wao ndio wananufaika? Mnaogopa nini kuwapa taifa lao? Au mnaogopa nchi kuongozwa na sheria za dini ndio maana gharama kubwa yatumika kuulinda muungano/ukoloni kwa wazanzibar?

Sasa mimi nashindwa kuwaelewa maccm,hivi kwanin. Huwa mnapinga serikali tatu kwenye rasimu ya katiba kama kweli mnauchungu nazenji mlitakiwa kulipigania hili lipite

Cc boko halam,biggshow,Buchanan
 
Sijazungumzia suala "Takwimu" zilizotolewa kwenye Tume ya Warioba bali ni kauli ya "Zanzibar Sio Nchi" ilipotolewa na Jaji Agustino Ramadhan hatukuona pilikapilika za Kubadili Katiba ya Zanzibar, 1984 ili Zanzibar iwe "nchi" lakini PM Pinda, mtoto wa Mkulima aliponyanyua tu mdomo, unajua kilichotokea!mbona unataka ku-divert mada kwa makusudi?

Sawa tunajua Watanganyika weng wameizwa na mabadiliko ya katiba ya Zanzibar, lakin kama hiyo ndio hoja yako, labda nawe nikuulize,
Kwan nani aliyetegemea haya mabadiliko ya Katiba ya Muungano yatatokezea?
hatakat za kudai katiba mpya zilianza kushika kasi tokea mwaka 1995 kama ni shindikizo la chama cha CUF, lakin Watanganyika na Serikali yao hawana habari nalo, sasa iweje Jana baada ya CDM kushinikiza katiba mpya Watanganyika weng walikubali mabadiliko,
Je, hapa sio double standard....? ama ni Kwa Wazanzibar tu?
 
Wanafiki ni viumbe wabaya sana!
Linapokuja suala la Muungano basi utawaona wako sera za CCM! Na kujifanya watu wa karibu saaana na CCM!

Likija suala la Uongozi wa nchi wanavaa yale yale magwanda yao ya CDM!

Hivi huu unafiki utaisha lini!?

Sio unafiki, watu hatuangalii "personalities" tunaangalia masuala! Ukweli ni ukweli tu hata kama utasemwa na Shetani!
 
Kwa hiyo wewe fikra zako zinaishia hapo kwenye mafuta au ndio muendelezo wa kejeli kwa wazanzibar? Zanzibar ni taifa lenye kila utajiri na zanzibar ni taifa ambalo kwa hadhi yake halikupaswa kuwa ombaomba kwa Watanganyika. Leo hii Zanzibar ndio inategemea eti iwezeshwe na watanganyika ili kuendesha nchi wakati Zanzibar inautajiri wa kuweza kuindesha serikali bila kuwa ombaomba. Maliasili zinabebwa kinyemela kutoka Zanzibar na kuja kuinufaisha Tanganyika kisha Twasema Zanzibar inategemea Tanganyika.

Maliasili gani zinachukuliwa kutoka Zanzibar kuja tanganyika? Toa mifano hapa sio pa ku bwabwaja story zakwenye kahawa.
 
Nini Pinda kwa upande wa Zanzibar hata JK akisema Zanzibar siyo nchi watamjia juu,kwa sababu kwani
yeye ni nani kwenye nchi ya Zanzibar?? Tatizo ni unafiki wa watanganyika kujifanya tunang'anga'na na
Zanzibar na kuendelea kuendesha Tanganyika kwa mgongo wa Tanzania'
 
Sasa mimi nashindwa kuwaelewa maccm,hivi kwanin. Huwa mnapinga serikali tatu kwenye rasimu ya katiba kama kweli mnauchungu nazenji mlitakiwa kulipigania hili lipite

Cc boko halam,biggshow,Buchanan

Muungano wa Serikali 3 utaongeza kero zaidi ya kuzipunguza! Ukiangalia Rasimu ya 2 utaona tayari matatizo yatakayokuwa created na hizo Serikali!
Katiba ya Muungano (kwa mujibu wa Rasimu hiyo) sio Supreme kwa maana kwamba katiba 3 (ya Zanzibar, Tanganyika na Muungano) zina hadhi sawa!
Nyerere aliwahi kusema kwenye kitabu chake cha "Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania" kuwa "Mafahali wawili hawakai zizi moja" na kwamba Tanganyika atakuwa Gorbachev wa kuiua Tanzania na akifanya hivyo atajimaliza mwenyewe!"
Kwa hiyo hapa tusidanganyane, tunaruka mkojo na kukanyaga kinyesi!
 
What the hell is double standard nyinyi??acheni unafiki wenu...!!

Watu mmekaa kushingilia jambo moja kila siku kwa maslahi yenu huku mmeweka pamba maskion ndio nin sasa??

Kama wao wazanzibar wenyewe wanataka taifa lao iweje nyinyi muendelee kuwawekea ngumu na kuwatolea kauli za kejeli?

What is double standard wakati watu wameweka nia yao mbele na inaonekana?

Hakuna nchi katika dunia hii inayoitwa Zanzibar...hii hapa chini ni sehemu ya list ya nchi zilizopo duniani
 

Attachments

  • 1393313676548.jpg
    1393313676548.jpg
    54.5 KB · Views: 53
Mkuu mimi nazungumzia maslahi ya nchi, sio u-CHADEMA wala u-CCM. Hilo la external influence liko wazi kabisa wala halihitaji speculations! Soma taarifa ya Siri ya CIA juu ya Mapinduzi ya Zanzibar, 1964 in context ndio utaelewa namaanisha nini hapa!

Kwa taarifa yako hata Constitutional Review Commission (CRC) ya akina Warioba walilijadili hili kwa kirefu sana!

Ukweli ndo huo, wewe baki na "CHADEMA/CCM Politics," dunia inaendeshwa kwa underground movements kwa kiasi kikubwa!

Mkuu kwanza nakuomba upunguze kunipiga Ban kwakumsalandia bwana mdogo Lema na unawaacha wanaomtukana Jk. Nimeyasema haya kwakuwa wahenga wana msemo wao wasemao UMUONAPO ZUMBE HAPOHAPO MSALIMIE.

Tukirudi kwenye mnakasha nikubaliane na wewe kuhusu hili la influence ya nje katika politics zetu na bila shaka ni kila nchi yeyote duniani haikosi hali hiyo. Lakini Unapowasema wazanzibar ati ni double standard kwenye kauli zao kuhusu masuala ya muungano ni vyema na wewe pia ukajipima ni msafi kiasi gani.

Kumbuka unapomnyooshea kidole kimoja mwenzako vyengine vinne vinakuzodoa mwenyewe. Uzuri tunafahamiana humu ndani kwa maandiko yetu ndio maana nakuambia wenye undumilakuwili sio wazanzibar tu bali sisi watanganyika ni zaidi ya hapo.

Therefore if we wish to solve the problem then we should remove our hypocratical ideas and deed. Lazima tukisema flani ni mzinzi ni vyema tujitathmini sisi ni wasafi kiasi gani. Arrasso!?
 
Sio unafiki, watu hatuangalii "personalities" tunaangalia masuala! Ukweli ni ukweli tu hata kama utasemwa na Shetani!

Ukweli upi!?

Mpaka leo watu wanajifanya hawana fahamu!
Muungano gani tunaoongelea humu na kuupigia kelele!

Zanzibar wana.
Nyimbo yao ya taifa!
Jeshi lao.
Anaekagua gwaride ni RAIS WAO!
Mwenye kutoa Amri ya heshi hilo RAIS WA ZANZIBAR!

Masuala ya Ulinzi yote ya Zanzibar Wanayasimamia Serikali ya ZAnzibar!

Sasa huo muungano umebaki wapi?

Kama sio kwenye Dhulma tu! Ya Bara kukwiba mapato na haki ambayo wazanzibari wanastahili kupewa??

Ule mfuko wa Muungano ulioko kwenye katiba! Ambao fedha zake zinatakiwa kutumia kwa ajili ya huo Muungano hebu nipe takwimu toka umeanzishwa Zanzibar WAMEPATA SHS NGAPI!!?

Jibu ni HAKUNA KITU!

sasa kama sio UNAFIKI NI KITU GANI HAPO!?

Acheni hizo!

Huu muungano ulishakufa Zamaani kabisa!
Kilichobaki ni ULAFI TU NA DHULMA Ya haki za watu tunaojifanya kuwaita WANANCHI WENZETU!
 
Nini Pinda kwa upande wa Zanzibar hata JK akisema Zanzibar siyo nchi watamjia juu,kwa sababu kwani
yeye ni nani kwenye nchi ya Zanzibar?? Tatizo ni unafiki wa watanganyika kujifanya tunang'anga'na na
Zanzibar na kuendelea kuendesha Tanganyika kwa mgongo wa Tanzania'

Hata Zanzibar inaing'ang'ania Tanzania, ndio maana wanaishi popote katika nchi hii bila kuulizwa na mtu yeyote! Wanaongoza Wizara na Idara zisizo za Muungano bila hofu yoyote! Pia tumesikia kauli mbalimbali za Wazanzibari wenyewe wakiombea Muungano wa Serikali 2 uendelee! Hata wale wasioupenda kabisa Muungano still bado wanataka Muungano wa "Nkataba!"
Hawa Wazenj wanakuwa kama wanawake akitaka umpende zaidi atatishia kurudi kwao, huku akibaki pale pale!
Kwa hiyo asikudanganye mtu, hakuna wanaoung'ang'ania Muungano kama Wazanzibari!
 
Kwa nini tuiachie Zanzibar wajukuu wa sultani! Mnadhani Watanganyika wajinga waache ndugu zao warejeshwe kwenye utumwa?

We Mtanganyika ni mjukuu wa nani? Hujui hata unachokiandika. Wewe ni mzembe wa kufikiri na ni mzembe wa kutumia busara. Afadhali tu ungekaa kimya ukaficha aibu yako ya ujinga wa kutokwenda shule na ujinga wa kushindwa kujifunza kupitia hadithi za babu zako kuhusina na historia ya nchi yetu.
 
Sasa mimi nashindwa kuwaelewa maccm,hivi kwanin. Huwa mnapinga serikali tatu kwenye rasimu ya katiba kama kweli mnauchungu nazenji mlitakiwa kulipigania hili lipite

Cc boko halam,biggshow,Buchanan

Mimi msimamo wangu ni serikali tatu although haiwezi kutatua matatizo ya muungano lakini ni muelekeo mzuri wa kuuvunja muungano. Kila serikali hkiwa na maamuzi yake na kushirikiana katika mambo kadhaa hiyo itakuwa hnaipa ahueni Zanzibar ya kutawaliwa totally na tanganyika.
 
Angalia sana mkuu, ukisema ukweli sana juu ya hili utaitwa mwana Chadema. Imefika mahali watu hawataki tena kufikirisha ubongo wao bali kurukia mambo ya itikadi za vyama tu.

Kuwa na fikra huru ni jambo jema lakini kama unafadhiliwa mpaka pesa ya kununua bando lazima uuze na akili yako.
 
We utakuwa mzanzibara. Nasubiri muungano ufe tukutimue

Mimi ni mtanganyika halisi ninapenda haki itendeke kwa watu wote. Dhulma si jambo jema na kumsaidia/kumnusuru ndugu aliyedhulumiwa ni jambo la heri mbele za Mungu.
 
Hata Zanzibar inaing'ang'ania Tanzania, ndio maana wanaishi popote katika nchi hii bila kuulizwa na mtu yeyote! Wanaongoza Wizara na Idara zisizo za Muungano bila hofu yoyote! Pia tumesikia kauli mbalimbali za Wazanzibari wenyewe wakiombea Muungano wa Serikali 2 uendelee! Hata wale wasioupenda kabisa Muungano still bado wanataka Muungano wa "Nkataba!"

Hawa Wazenj wanakuwa kama wanawake akitaka umpende zaidi atatishia kurudi kwao, huku akibaki pale pale!

Kwa hiyo asikudanganye mtu, hakuna wanaoung'ang'ania Muungano kama Wazanzibari!

Kwan hakuna Watanganyika wanaoishi Zanzibar...?

lakini kama unataka Wizara zenu zisiwe na Wazanzibar, basi musitumie nembo yetu ya Muungano kama vile Zanzibar tunavyotumia nembo yetu!!

Almuhimu hapa lazima Watanganyika waitafute Tanganyika yao....
 
Tatizo sio Wazanzibari bali ni viongozi wa Tanganyika wanoing'ang'ania Zanzibar isijitenge na kujitegemea.

Kwa ufupi tatizo la muungano lipo kwa Tanganyika zaidi kuliko Zanzibar kwakuwa yenyewe imeshajitambulisha kama nchi ikwa na vigezo vyote vya nchi. Sasa Tangayika ipo wapi? Hakuna viongozi waoga kama wale wanaotokea Tanganyika. Mtu atatolewa Zanzibar na kupewa wizara ya Tanganyika wote wanafyata mikoa. Hebu hilo lifanyike Zanzibar uone cha moto. Hata rais anateua wazanzibar kushika wizara zisizo za muungano ili kujibembeleza tu hakuna mantiki yoyote.

Viongozi wa Tanganyika wanakabiliwa na kitu kinachoitwa "fear oa unknown" kwamba hivi leo Tanganyika ikirudi itakuwaje? Tutaitawala vipi maana hatuna uzoefu wa kuendesha nchi yetu wenyewe, je mimi nitakuwa nani nk nk. Wazanzibari hawana shida kwani tayari wanaserikali yao na system ya uongozi inayofanya kazi.

TANGANYIKA BILA ZANZIBAR INAWEZEKANA. WAKE UP TANGANYIKANS!
 
Mkuu kwanza nakuomba upunguze kunipiga Ban kwakumsalandia bwana mdogo Lema na unawaacha wanaomtukana Jk. Nimeyasema haya kwakuwa wahenga wana msemo wao wasemao UMUONAPO ZUMBE HAPOHAPO MSALIMIE. Tukirudi kwenye mnakasha nikubaliane na wewe kuhusu hili la influence ya nje katika politics zetu na bila shaka ni kila nchi yeyote duniani haikosi hali hiyo. Lakini Unapowasema wazanzibar ati ni double standard kwenye kauli zao kuhusu masuala ya muungano ni vyema na wewe pia ukajipima ni msafi kiasi gani. Kumbuka unapomnyooshea kidole kimoja mwenzako vyengine vinne vinakuzodoa mwenyewe. Uzuri tunafahamiana humu ndani kwa maandiko yetu ndio maana nakuambia wenye undumilakuwili sio wazanzibar tu bali sisi watanganyika ni zaidi ya hapo. Therefore if we wish to solve the problem then we should remove our hypocratical ideas and deed. Lazima tukisema flani ni mzinzi ni vyema tujitathmini sisi ni wasafi kiasi gani. Arrasso!?

Mkuu inawezekana na mimi nina mapungufu yangu lakini sidhani kama ni vibaya kusema kile ninachoamini! Tushindane kwa hoja sio ku-attack personalities!
Nimeona sasa hivi mmeshaanza kugeuza mjadala na kunijadili mimi badala ya hoja iliyoko mezani! Jadili hoja yangu zaidi ili tusaidia kujenga nchi yetu! Who knows? Unaweza kunishawishi nikabadili mawazo niliyo nayo na kuwa na mtizamo mpya, na ndio maana tuko hapa Jukwaani!
Na huo "undumila kuwili wa Watanganyika" unaousema ndio upi? Unasema hivyo kwa ajili ya "ku-balance equation" au namna gani? Mbona hutoi detail? Au ndo juhudi za ku-divert mada?
 
Back
Top Bottom