Hakuna anayemtukana bali anajitukana mwenyewe. Watu wanachofanya ni kumwelezea jinsi alivyo na afanyavyo. Hatakiwi kumlaumu mtu zaidi ya nafsi yake mwenyewe.
Rais anafanya vizuri ili kuweza kuwatambua watu hawa. Wanamsema vibaya, wanamkosoa na kumkejeli kama vile wana uzalendo na maono kuwazidi wale waliopo CCM.
Kisha Rais kuweza kuwapima anawalambisha kidogo tu hela na ahadi ya vyeo, kwisha kabisa. Wanaanza kuimba nyimbo za kumsifa Rais yule yule waliyekuwa wakimkosoa mwanzoni. Baada ya hapo Rais anajua kuwa huyu siyo wa kumwamini ni opportunist. Mtumie kwa wakati fulani kwa lengo fulami na mahali fulani. Muda ukifika, mtupe tu huko. Hana maana na wala hawezi kuaminika kwa lolote.
Hawa ni kama mke wa mtu, uwe na uhusiano naye, umshauri kumfanyia ubaya mumewe ili aachane naye na kisha umwoe, halafu anakubali. Huyo kamwe siyo mwanamke wa kumwamini kwa lolote. Mtumie kwa starehe yako lakini usimwamini kwa jukumu lolote muhimu na linalohitaji mtu wa kuaminika.
Watu kama Waitara, na wote waliobadilika kutokana na ahadi ya fedha na vyeo, ni wa kuwatumia kwa muda fulani tu huko CCM, kisha ni kuwatupa huko wakahangaike na mambo binafsi, na siyo uongozi. Hawa siku CCM ikipoteza madaraka, watakuwa wa kwanza kuondoka, hawatapoteza muda kuipigania CCM.