Dola kuishughulikia CHADEMA

Dola kuishughulikia CHADEMA

Joined
Aug 29, 2010
Posts
10
Reaction score
0
DAWATI LA HATUDANGANYIKI limepokea taarifa za kuaminika kutoka vyanzo vyake kuwa kuwa mara tu baada ya mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CHADEMA, siku ya Jumamosi tarehe 28 Agosti 2010 wakuu wa Idara ya intelejensia walikutana na timu ya Kampeni ya CCM kwa ajili ya kutoa mlisho nyuma, na kupanga mikakati ya kuikabili CHADEMA, na yafuatayo yalijiri:-

a)Idara ililazimika kutolea ufafanuzi sababu zilizopelekea shauri wake wa kutaka matangazo ya TBC ya mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za CHADEMA kurejeshwa mara moja baada ya kukatizwa. Walieleza kuwa ilitokana na maelfu ya wananchi waliohudhuruia mkutano huo kuwa wa kwanza kugundua kukatishwa kwa matangazo hayo na kuamua wenyewe, bila ya kushawishiwa na kiongozi yeyote kuchukua hatua kali sana dhidi ya TBC. Viongozi wa CHADEMA walistukia tuu mkutano ukitaka kuvurugika kwa wananchi kudai vikali kurejeshwa kwa matangazo hayo. Ilielezwa kuwa kuvurugika kwa mkutano ikwa sababu ya kukatishwa kwa matangazo ya chombo cha umaa kama TBC iimeelezwa kuwa ingekuwa ni aibu kubwa kwa Serikali na TBC.

b)Idara ilitoa taarifa kuwa licha ya umati wa watu waliohudhuria kutofikia ule wa mkutano wa uzinduzi wa CCM, lakini kwa kuwa umati huo kila mtu alijinyanyua kutoka atokako na kuja Jangwani kwa ajili ya CHADEMA tofauti na maandalizi makubwa ya usafiri, fedha, burudani za kila aina, viburudisho n.k yaliyofanywa na CCM kuwafikisha watu kwa maelfu Jangwani. Hizo ni dalili mabaya na ni tishio kubwa kwa CCM. Na ikaamuliwa kuwa iandaliwe mikakati ya kuwakatisha tamma wananchi wenye mapenzi na CHADEMA.

Mkakati
:- Ilamuliwa kuwa upandikizwe mgogoro baina ya viongozi wa CHADEMA na mgombea wake Dr W. Slaa; na kuwachonganisha na wapiga debe wao akina Marando, Shibuda, Mpendazoe n.k kwa nia ya kuwakatisha tamaa wenye mapenzi na CHADEMA na wote wanaotarajia kuwapigia kura wagombea wa CHADEMA.

Iliamualiwa kwa kuwa wananchi wanampenda sana Dr W Slaa, zisambazwe habari kuwa aelewani na Mwenyekiti wake Ndg Freeman Mbowe kwa sababu Dr Slaa sio kutoka kabila la wachagga. I


likubaliwa kuwa taarifa hizo zianze kusambazwa wiki inayoanzia Jumatatu ya tarehe 30 Agosti 2010. Na tathmini ifanyike kujua mafanikio yake wakati zinatungwa mbinu mpya.

Iliamuliwa kuwa magazeti ya New Habari Corporation ikiwemo Mtanzania, Rai n.k yaanze kutumika kwa kazi hiyo wakati waandishi zaidi wa kufanya kzai hiyo wakitafutwa.



Ili wananchi wenye mapenzi mema na CHADEMA waweze kusadiki taarifa zitakazosambazwa ilikubaliwa kuwa magazeti yatakayotumika yaanze kwanza kwa kipindi kifupi kuandika habari njema kuhusu CHADEMA na wagombea wake; na baada ya mashabiki wake kuyaamini magazeti na vyombo hivyo vya habari ndipo kazi ya kuisamabaratisha CHADEMA ianze rasmi.

Ili kutekeleza mipango hiyo waandishi wa gazeti la Mtanzania walipatiwa maelekezo ya kurekebisha kichwa cha habari na maudhui ya habari za uzinduzi wa CHADEMA zilizochapishwa tarehe 29/8/2010, kwa lengo hilo.

Vyombo vya habari vya Serikali ya ikiwemo magazeti ya Daily News na Habari Leo na TBC na redio za TBC vilielekezwa kuanza mara moja kazi ya kuipamba CHADEMA kama chama na watu wa fujo mbele ya jamii makakati amabo unadaiwa kufanikiwa sana kuisambaratisha CUF mwaka 2005, wakati Mkuu wa chombo kimoja cha dola alipodai siku moja kabla ya upigaji kura wamekamata shehena ya majambia yenye rangi za bendera za CUF

c)Pingamzi la CHADEMA dhidi ya Jakaya Kikwete mkutano ulikubaliana kuwa kuaniza sasa idara ihakikishe kuwa inamgeuzia kibao Dr Slaa na kusambaza habari kwa wafanyakazi na umma kuwa DR Slaa anapinga wafanyakazi kuongezwa mishahara ndio maana CHADEMA inamuwekea pingamizi mgombe wa CCM Jakaya Kikwete kwa kitendo cha kuwaongezea mishahara watumishi wa umma katika kipindi hiki cha kampeni.

Dawati litaendelea kuwahabarisha!!!!!!!
 
Watanzania kwa fix,mko mbali!You can fool some people for some time but you can't fool all the people all the time!
 
Mmmmmh kazi ipo mwaka huu. Kama ndivyo nadhani kaulimbiu ya ...hatudanganyiki... inafaa sana. Yaani hao sniffers hawaamini kuwa wanaweza kuongozwa na watu tofauti na mazoea? Sasa kama ni sniffers wa ukweli kwa nini hawakuona kuwa hali imeanza kuwa mbaya toka 2008? Hata bibi yangu anajua kuwa listi ya 'wajasiriamali wazawa' ilipotajwa mambo yangekwenda kusiko

Naona sniffers koko wameanza kuja ukumbini kupoteza mwelekeo, karibuni. Mkuu usisahau kuwaita na wenzako, we have been fooled all the time, and you know that!
 
tulikipata wageni 5 kwa wiki kama wewe hapa Jf itakuwa burudani sana..kama hayo uliyoyaandika ya kweli, basi siasa ya Tz inazidi kupata kale kaugonjwa ka jamaa.
 
Hata kama umetunga conspiracy hii lakini ni tamu na inawezekana. To start with, nimeshangaa gazeti la Majira la jana likibeba bango la tangazo la CCM front page, na magazeti ya Mtanzania kumsifia Dr. Slaa. Aidha, kimya cha Zitto kinatia shaka kana kwamba kazi ya kuchonganisha imeishaanza.

Kwa sasa nguvu ya mapambano dhidi ya Chadema itaelekezwa kwenye vyombo vya habari kuliko mikutano yao maana si rahisi kumchafua Dr. Slaa kupitia mikutano ya kampeini.
 
2010 Hatudanganyiki - Mhh wewe uliyeposti hii habari mbona mgeni? au multiple profile?:glasses-nerdy:
 
Mkuu sniffer anataka kutuambia yeye si kati ya hao ambao kazi yao ni kuchonganisha wakati anaanza kwa kauli ya kuchonganisha

Jamaa huwa kazi yake ni kupindisha mijdala yenye tija kwa taifa sababu anatetea mkate wake!
 
Tatizo idara ya usalama haijajifahamu kuwa ndani yake kuna maoptimistics na si wazalendo wa kweli. Naamini hiyo intelejensia waliyonayo haikushushwa mbinguni bali vichwa vya watu ndivyo vilijipanga kubuni na kuboresha uwezo wa kiitelejensia. Wasisahau kwamba kuna watu wamezaliwa na intelejensia as kipaji. ningeishauri idara ya UwT yafuatayo.

  • wakae mbali na siasa hasa kipindi hiki cha uchaguzi au wajitahidi kufanya hivyo kwa kificho (ingawa tutawagundua na kuwaumbua)
  • Waweke maslahi ya nchi kwanza na si maslahi ya chama wala siasa.
  • Watoe ulinzi sawa kwa wagombea wote wa kiti cha urais bila kujali anatoka chama gani
  • Tunampenda rais wetu lakini sisi wananchi tunaweza kutompigia kura hata wakifanya mbwembwe namna gani hivyo wasitutishe wananchi ili tumpe ushindi kisaikolojia
  • wao wapo kwa mujibu wa sheria ambayo siyo msahafu hivyo nguvu yetu ipo ktk kuidhibiti hiyo sheria. wajitahidi kuonesha uzalendo na mapenzi mema kwa TANZANIA hasa ukichukulia tupo nyuma sana kiuchumi kutokana na ubwetekaji wa watawala waliokosa karama za uongozi.
Amini amini nakuambieni.....
 
Peoples powerrrrrrrrrrrrrrrrrrr, 2010 hatudanganyikiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.
 
Ili kutekeleza mipango hiyo waandishi wa gazeti la Mtanzania walipatiwa maelekezo ya kurekebisha kichwa cha habari na maudhui ya habari za uzinduzi wa CHADEMA zilizochapishwa tarehe 29/8/2010, kwa lengo hilo.

Dawati litaendelea kuwahabarisha!!!!!!!

Kama hii taarifa ni ya kweli, naanza kushawishika ni kwa nini Gazeti la Mtanzania liliwapamba sana CHADEMA jana Sunday.

Hatudanganyiki; najua between the lines utakuwa una link kali sana na CCM na Intelligencia. Na ni wazi kuwa kinachokusukuma ni uzalendo wa Nchi yako na machungu uliyoyanayo. Kila jema lina malipo yake hata kama no body knows you.

On the other hand: CHADEMA msiidharau taarifa yoyote mnayoipata. Ifanyieni kazi kadiri mnavyoweza both Kiinteligensia, Kisiasa na kisheria.

CCM: Nyie ni wakongwe na mliruhusu Demokrasia. Tambueni kuwa Demokrasia ni kwa ajili ya Maendeleo ya Nchi. Ni jambo jema mkakabiliana na ushindani bila kutumia mbinu chafu.

Muonekano ulivyo wa Uchaguzi huu ni tofauti na miaka mingine. Jifunzeni kutoka Pemba au visiwani. Hatuhitaji kumwaga damu au mtu kuchinjwa shingo!

Mpenda Haki na Amani asiyefungamana na Chama Chochote

Superman!
 
tulikipata wageni 5 kwa wiki kama wewe hapa Jf itakuwa burudani sana..kama hayo uliyoyaandika ya kweli, basi siasa ya Tz inazidi kupata kale kaugonjwa ka jamaa.

Unamaanisha kale ka kuanguka hadharani au........!!!!
 
Kama hii taarifa ni ya kweli, naanza kushawishika ni kwa nini Gazeti la Mtanzania liliwapamba sana CHADEMA jana Sunday.

Hatudanganyiki; najua between the lines utakuwa una link kali sana na CCM na Intelligencia. Na ni wazi kuwa kinachokusukuma ni uzalendo wa Nchi yako na machungu uliyoyanayo. Kila jema lina malipo yake hata kama no body knows you.

On the other hand: CHADEMA msiidharau taarifa yoyote mnayoipata. Ifanyieni kazi kadiri mnavyoweza both Kiinteligensia, Kisiasa na kisheria.

CCM: Nyie ni wakongwe na mliruhusu Demokrasia. Tambueni kuwa Demokrasia ni kwa ajili ya Maendeleo ya Nchi. Ni jambo jema mkakabiliana na ushindani bila kutumia mbinu chafu.

Muonekano ulivyo wa Uchaguzi huu ni tofauti na miaka mingine. Jifunzeni kutoka Pemba au visiwani. Hatuhitaji kumwaga damu au mtu kuchinjwa shingo!

Mpenda Haki na Amani asiyefungamana na Chama Chochote

Superman!
Wewe unaonekana chadema kabisa. Haina haja yakujificha, huo utakuwa unafiki.
 
DAWATI LA HATUDANGANYIKI limepokea taarifa za kuaminika kutoka vyanzo vyake kuwa kuwa mara tu baada ya mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CHADEMA, siku ya Jumamosi tarehe 28 Agosti 2010 wakuu wa Idara ya intelejensia walikutana na timu ya Kampeni ya CCM kwa ajili ya kutoa mlisho nyuma, na kupanga mikakati ya kuikabili CHADEMA, na yafuatayo yalijiri:-

a)Idara ililazimika kutolea ufafanuzi sababu zilizopelekea shauri wake wa kutaka matangazo ya TBC ya mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za CHADEMA kurejeshwa mara moja baada ya kukatizwa. Walieleza kuwa ilitokana na maelfu ya wananchi waliohudhuruia mkutano huo kuwa wa kwanza kugundua kukatishwa kwa matangazo hayo na kuamua wenyewe, bila ya kushawishiwa na kiongozi yeyote kuchukua hatua kali sana dhidi ya TBC. Viongozi wa CHADEMA walistukia tuu mkutano ukitaka kuvurugika kwa wananchi kudai vikali kurejeshwa kwa matangazo hayo. Ilielezwa kuwa kuvurugika kwa mkutano ikwa sababu ya kukatishwa kwa matangazo ya chombo cha umaa kama TBC iimeelezwa kuwa ingekuwa ni aibu kubwa kwa Serikali na TBC.

b)Idara ilitoa taarifa kuwa licha ya umati wa watu waliohudhuria kutofikia ule wa mkutano wa uzinduzi wa CCM, lakini kwa kuwa umati huo kila mtu alijinyanyua kutoka atokako na kuja Jangwani kwa ajili ya CHADEMA tofauti na maandalizi makubwa ya usafiri, fedha, burudani za kila aina, viburudisho n.k yaliyofanywa na CCM kuwafikisha watu kwa maelfu Jangwani. Hizo ni dalili mabaya na ni tishio kubwa kwa CCM. Na ikaamuliwa kuwa iandaliwe mikakati ya kuwakatisha tamma wananchi wenye mapenzi na CHADEMA.

Mkakati
:- Ilamuliwa kuwa upandikizwe mgogoro baina ya viongozi wa CHADEMA na mgombea wake Dr W. Slaa; na kuwachonganisha na wapiga debe wao akina Marando, Shibuda, Mpendazoe n.k kwa nia ya kuwakatisha tamaa wenye mapenzi na CHADEMA na wote wanaotarajia kuwapigia kura wagombea wa CHADEMA.

Iliamualiwa kwa kuwa wananchi wanampenda sana Dr W Slaa, zisambazwe habari kuwa aelewani na Mwenyekiti wake Ndg Freeman Mbowe kwa sababu Dr Slaa sio kutoka kabila la wachagga. I


likubaliwa kuwa taarifa hizo zianze kusambazwa wiki inayoanzia Jumatatu ya tarehe 30 Agosti 2010. Na tathmini ifanyike kujua mafanikio yake wakati zinatungwa mbinu mpya.

Iliamuliwa kuwa magazeti ya New Habari Corporation ikiwemo Mtanzania, Rai n.k yaanze kutumika kwa kazi hiyo wakati waandishi zaidi wa kufanya kzai hiyo wakitafutwa.



Ili wananchi wenye mapenzi mema na CHADEMA waweze kusadiki taarifa zitakazosambazwa ilikubaliwa kuwa magazeti yatakayotumika yaanze kwanza kwa kipindi kifupi kuandika habari njema kuhusu CHADEMA na wagombea wake; na baada ya mashabiki wake kuyaamini magazeti na vyombo hivyo vya habari ndipo kazi ya kuisamabaratisha CHADEMA ianze rasmi.

Ili kutekeleza mipango hiyo waandishi wa gazeti la Mtanzania walipatiwa maelekezo ya kurekebisha kichwa cha habari na maudhui ya habari za uzinduzi wa CHADEMA zilizochapishwa tarehe 29/8/2010, kwa lengo hilo.

Vyombo vya habari vya Serikali ya ikiwemo magazeti ya Daily News na Habari Leo na TBC na redio za TBC vilielekezwa kuanza mara moja kazi ya kuipamba CHADEMA kama chama na watu wa fujo mbele ya jamii makakati amabo unadaiwa kufanikiwa sana kuisambaratisha CUF mwaka 2005, wakati Mkuu wa chombo kimoja cha dola alipodai siku moja kabla ya upigaji kura wamekamata shehena ya majambia yenye rangi za bendera za CUF

c)Pingamzi la CHADEMA dhidi ya Jakaya Kikwete mkutano ulikubaliana kuwa kuaniza sasa idara ihakikishe kuwa inamgeuzia kibao Dr Slaa na kusambaza habari kwa wafanyakazi na umma kuwa DR Slaa anapinga wafanyakazi kuongezwa mishahara ndio maana CHADEMA inamuwekea pingamizi mgombe wa CCM Jakaya Kikwete kwa kitendo cha kuwaongezea mishahara watumishi wa umma katika kipindi hiki cha kampeni.

Dawati litaendelea kuwahabarisha!!!!!!!
Safi sana. Sasa ni zamu yenu. Mlishindwa kuwasaport wenzenu sasa mmeanza kutapata. Acheni kulia, gonjeni panga liwapitie kwanza ndo mpate adabu. We losted important person bugeni.
 
Kama hii taarifa ni ya kweli, naanza kushawishika ni kwa nini Gazeti la Mtanzania liliwapamba sana CHADEMA jana Sunday.

Hatudanganyiki; najua between the lines utakuwa una link kali sana na CCM na Intelligencia. Na ni wazi kuwa kinachokusukuma ni uzalendo wa Nchi yako na machungu uliyoyanayo. Kila jema lina malipo yake hata kama no body knows you.



On the other hand: CHADEMA msiidharau taarifa yoyote mnayoipata. Ifanyieni kazi kadiri mnavyoweza both Kiinteligensia, Kisiasa na kisheria.

CCM: Nyie ni wakongwe na mliruhusu Demokrasia. Tambueni kuwa Demokrasia ni kwa ajili ya Maendeleo ya Nchi. Ni jambo jema mkakabiliana na ushindani bila kutumia mbinu chafu.

Muonekano ulivyo wa Uchaguzi huu ni tofauti na miaka mingine. Jifunzeni kutoka Pemba au visiwani. Hatuhitaji kumwaga damu au mtu kuchinjwa shingo!

Mpenda Haki na Amani asiyefungamana na Chama Chochote

Superman!



Ukituliza akili vizuri basi utaona kuwa Mr Hatudanganyiki anaongea kilekile ambacho huwa kinafanywa na RA. Salva Rweyemamu, Muhingo,Makamba, Makalla, Lowassa etc.. kabla ya kudodosa mimi mwenzenu naelekea kukubali, hebu angalieni Mtanzania la jana lilivyokuwa
 
Safi sana. Sasa ni zamu yenu. Mlishindwa kuwasaport wenzenu sasa mmeanza kutapata. Acheni kulia, gonjeni panga liwapitie kwanza ndo mpate adabu. We losted important person bugeni.

UPUMBAVU.jpg
 
Kama hii taarifa ni ya kweli, naanza kushawishika ni kwa nini Gazeti la Mtanzania liliwapamba sana CHADEMA jana Sunday.

Hatudanganyiki; najua between the lines utakuwa una link kali sana na CCM na Intelligencia. Na ni wazi kuwa kinachokusukuma ni uzalendo wa Nchi yako na machungu uliyoyanayo. Kila jema lina malipo yake hata kama no body knows you.

On the other hand: CHADEMA msiidharau taarifa yoyote mnayoipata. Ifanyieni kazi kadiri mnavyoweza both Kiinteligensia, Kisiasa na kisheria.

CCM: Nyie ni wakongwe na mliruhusu Demokrasia. Tambueni kuwa Demokrasia ni kwa ajili ya Maendeleo ya Nchi. Ni jambo jema mkakabiliana na ushindani bila kutumia mbinu chafu.

Muonekano ulivyo wa Uchaguzi huu ni tofauti na miaka mingine. Jifunzeni kutoka Pemba au visiwani. Hatuhitaji kumwaga damu au mtu kuchinjwa shingo!

Mpenda Haki na Amani asiyefungamana na Chama Chochote

Superman!


well said.CHADEMA ni chama makini sana na kawaida yao huwa hawakurupuki....wanafanyia kazi mamabo haya kwa umakini mkubwa sana .Believe me
 
Mkakati mwengine ni kuifanya Jamiiforum iwe not reachable maana nasikia ni mwiba!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom