Makada kadhaa wamelalamikia kitendo cha CCM kutochukua hatua kadhaa kumdhibiti mgombea wa uraisi kupitia chadema Dr. Slaa; makada hao ambao wengi wao ni mafia walisomea Urusi na Romania, walilaumu mbinu hafifu zilizotumika kumdhibiti Dr. Slaa, kada mmoja alikaririwa kwa kusema " walijaribu kuweka vinasa sauti Dodoma sasa walitaka wamsikie anavyosoma Biblia? Tuliwaomba vijana watuachie kazi lakini walikataa wakidai hii ni karne ya 21 mbinu za kizamani zingeshindwa kumnasa Slaa, enzi zetu kazi hii ingekuwa ndogo sana tungetafuta kijana kiume wa kimbulu tungempatia kiasi kidogo tu kama tshs 5m alichotakiwa kusema ni Slaa kanilawiti !!! kwa kauli hiyo sisi tungemaliza mchezo ni mtanzani gani duniani ambaye hajawahi kuisikia kashfa ya ngono inavyotikisa kanisa katoliki duniani? Basi nakuhakikishia Slaa angekuwa anahangaikia dhamana kipindi badala ya kufanya kampeni za uchaguzi" Kada mwengine mwingine alimlaumu Raisi Kikwete kwa kutowathamini alidai Raisi Mkapa aliwathamini sana ndio maana haikuwa kazi kubwa kwao kuwamaliza watu kama, Mtikila,Mrema na Dr. Salmin hata hivyo walidai bado hawajachelewa kama wataombwa msaada kiufundi wako tayari kusaidia.