DMO Iramba aikashifu serikali ya Magufuli mbele ya Jafo

DMO Iramba aikashifu serikali ya Magufuli mbele ya Jafo

ashatakiwe kwa uchochezi,tabia mbaya hiyo ya kuchonganisha serikali tukufu na wananchi
 
Akiongea mbele ya Naibu Waziri Selemani Jafo,Mganga Mkuu wa Iramba ametoa taarifa kuwa hawajapokea fedha za Madawa toka July 2016!

DMO alijikita zaidi kuonyesha uhaba wa pesa za dawa na motisha kwa watumishi wa afya,pia uhaba wa watumishi.

Amesema serikali ijitahidi kuleta pesa kwa wakati ili kuwezesha huduma.

Hii ni kuikashifu serikali ya JPM ambayo imefunja rekodi Afrika Mashariki na kati ya kukusanya mapato kiasi cha kununua ndege mbili kwa mpigo kwa keshi.

Hahahahaa! nia yako nini mkuu? Watu wakurupuke kumfuta kazi au? Alichokiongea tofauti na Title yako..

By the way: Ulikusudia kuleta uchochezi kiasi kwamba ukasema DMO "Anaionya" serikali badala ya "kuionesha" (See red line)
 
Akiongea mbele ya Naibu Waziri Selemani Jafo,Mganga Mkuu wa Iramba ametoa taarifa kuwa hawajapokea fedha za Madawa toka July 2016!!DMO alijikita zaidi kuonyesha uhaba wa pesa za dawa na motisha kwa watumishi wa afya,pia uhaba wa watumishi.Amesema serikali ijitahidi kuleta pesa kwa wakati ili kuwezesha huduma.MY TAKE: DMO atambue serekale makini ya CCM haijaleta magonjwa
Hilo ni kosa, yeye siyo katibu mkuu wa wizara. Hata Seleman Jafo yeye anatafuta kick tu
 
Malofa MTU anaeleza ukweli wao eti aikashifu ,

Post #91 ndio inakufaa sana wewe. Hapo ndio unapoweza kujipima jee jukwaa hili ni size yako au ni sawa na Mzee Warioba kumpa suruali ya Marehemu Pepe Kalle avae
 
mkuu jaribu kunisoma katikati ya mstari utanielewa tu,

Shida ni kuwa jukwaa hili sasa hivi limevamiwa na watu wasio tafakari hoja kwa kina. Ule weledi wa zamani umepotea kabisa sasa sijui ni watoto wamekuwa wengi kuweza kuelewa wanaambiwa nini au ni matokeo ya Div 5?
 
Akiongea mbele ya Naibu Waziri Selemani Jafo,Mganga Mkuu wa Iramba ametoa taarifa kuwa hawajapokea fedha za Madawa toka July 2016!!DMO alijikita zaidi kuonyesha uhaba wa pesa za dawa na motisha kwa watumishi wa afya,pia uhaba wa watumishi.Amesema serikali ijitahidi kuleta pesa kwa wakati ili kuwezesha huduma.MY TAKE: DMO atambue serekale makini ya CCM haijaleta magonjwa
Nimepitia huu uzi zaidi ya mara 25 sijaona sehemu yeyote DMO aliapotoa kashfa.

Kwa nini unahangaika na mipasho namna hii hata mke wako akikusoma atakudharau sana.

Hivi unajua maana ya kashfa?
 
Mahitaji ya dawa na vifaa tiba kwa watanzania kwa siku moja gharama yake ni zaidi ya maradufu ya bei ya hizo ndege. Na ni kwa siku moja tu. Ni karibu na gharama ya kulisha chakula watanzania. Ni kitu ambacho hakiwezekani. Ni jukumu la kila mwananchi kujinunulia mwenyewe huduma hizo badala ya kutegemea kuletewa na serikali. Maduka binafsi ya dawa hayajawahi kuishiwa dawa. Sasa kelele za nini?
Sasa,Kama ni Hivyo,Kuna Faida Gani ya Watanzania Kulipa Kodi?
 
Nimepitia huu uzi zaidi ya mara 25 sijaona sehemu yeyote DMO aliapotoa kashfa.

Kwa nini unahangaika na mipasho namna hii hata mke wako akikusoma atakudharau sana.

Hivi unajua maana ya kashfa?
Mkuu,mtoa mada ametumia tafsida!ameandika kinyume!
 
Back
Top Bottom