DMO Iramba aikashifu serikali ya Magufuli mbele ya Jafo

DMO Iramba aikashifu serikali ya Magufuli mbele ya Jafo

Akiongea mbele ya Naibu Waziri Selemani Jafo,Mganga Mkuu wa Iramba ametoa taarifa kuwa hawajapokea fedha za Madawa toka July 2016!!DMO alijikita zaidi kuonyesha uhaba wa pesa za dawa na motisha kwa watumishi wa afya,pia uhaba wa watumishi.Amesema serikali ijitahidi kuleta pesa kwa wakati ili kuwezesha huduma.Hii ni kuikashifu serikali ya JPM ambayo imefunja rekodi Afrika mashariki na kati ya kukusanya mapato kiasi cha kununua ndege mbili kwa mpigo kwa keshi.
Mahitaji ya dawa na vifaa tiba kwa watanzania kwa siku moja gharama yake ni zaidi ya maradufu ya bei ya hizo ndege. Na ni kwa siku moja tu. Ni karibu na gharama ya kulisha chakula watanzania. Ni kitu ambacho hakiwezekani. Ni jukumu la kila mwananchi kujinunulia mwenyewe huduma hizo badala ya kutegemea kuletewa na serikali. Maduka binafsi ya dawa hayajawahi kuishiwa dawa. Sasa kelele za nini?
 
Wananchi mkiumwa mjitetemeshe wenyewe kujitibu. Muelewe kuwa magonjwa hayaletwi na serikali wala CCM! Msisubiri serikali iwahudumie maana haina fedha. Pia msikae kulalamikalalamika tu bali mfanye kazi!
mmebakiza miaka 4 tu ya kutawala,baada ya hapo tunawaweka bench
 
aisee,jamaa mchochezi kabisa.

sasa naibu waziri alienda kukagua nini kama hakuna dawa? ajira za afya zimesitishwa,angetuambia kama kuna watumishi wa kutosha,unaweza.kuta wagonjwa wanahudumiwa na wafagizi
Mkuu kwa jinsi serikali hii ya kidhalimu ilivyo basi utasikia kasimamishwa kazi kwa kuongea ukweli
 
Kla cku tunackia kayombo akisema mwez huu tumevuka malengo lakin bado huduma ni hafifu sana serikali ina madeni kila kona dawa hamna waziri anasema dawa zipo,makamu wa rais akanusha na kusema dawa hakuna
 
Akiongea mbele ya Naibu Waziri Selemani Jafo,Mganga Mkuu wa Iramba ametoa taarifa kuwa hawajapokea fedha za Madawa toka July 2016!!DMO alijikita zaidi kuonyesha uhaba wa pesa za dawa na motisha kwa watumishi wa afya,pia uhaba wa watumishi.Amesema serikali ijitahidi kuleta pesa kwa wakati ili kuwezesha huduma
Kichwa cha mada na Maelezo ya mada yanatofautiana kabisa.

Labda kichwa cha mada kingekuwa 'DMO amweleza Waziri Changamoto za Huduma ya Afya'

Hapo ingeendana na Maelezo yako ya ndani uliyoyaeleza.
 
Huo ni ukweli sio kashifa, kichwa cha habari yako kilitakiwa kuwa DMO Iramba aelezea changamoto zilizopo wilayani kwake
nadhani alitaka kueleza indirectly kuwa siku hizi ukizungumzia ukweli kwa kukosoa utendaji wa serikali unaweza kuonekana umetoa kashfa.
 
Kla cku tunackia kayombo akisema mwez huu tumevuka malengo lakin bado huduma ni hafifu sana serikali ina madeni kila kona dawa hamna waziri anasema dawa zipo,makamu wa rais akanusha na kusema dawa hakuna
Mkuu wiki hii ulishapita bandarini na kule chini kwenye yard ya magari ni Aibu! hamna kitu!. Kwanza huyu kayombo maneno yake hayana tofauti na yule waziri wa ulinzi wa iraq Mohamed saeed al sahhaf aliyetoa maneno ya majigambo dhidi ya marekani huku akijua sio kweli
 
Kichwa cha mada na Maelezo ya mada yanatofautiana kabisa.

Labda kichwa cha mada kingekuwa 'DMO amweleza Waziri Changamoto za Huduma ya Afya'

Hapo ingeendana na Maelezo yako ya ndani uliyoyaeleza.
Tangu mamvi abwagwe hawa bavichaa wamekalia kupindisha ukweli tu. Ndio kazi iliyobaki.
 
Uandishi mwingine wa habari wa kijinga kweli mbona DMO kaeleza changamoto za wilayani kwake lakini mwandishi anadai kaikashifu serikali ya ccm mwandishi kizumba kweli.
 
Akiongea mbele ya Naibu Waziri Selemani Jafo,Mganga Mkuu wa Iramba ametoa taarifa kuwa hawajapokea fedha za Madawa toka July 2016!!DMO alijikita zaidi kuonyesha uhaba wa pesa za dawa na motisha kwa watumishi wa afya,pia uhaba wa watumishi.Amesema serikali ijitahidi kuleta pesa kwa wakati ili kuwezesha huduma.MY TAKE: DMO atambue serekale makini ya CCM haijaleta magonjwa

Sasa ndio umeandika nini
CCM bana [emoji25][emoji25]
 
Akiongea mbele ya Naibu Waziri Selemani Jafo,Mganga Mkuu wa Iramba ametoa taarifa kuwa hawajapokea fedha za Madawa toka July 2016!!DMO alijikita zaidi kuonyesha uhaba wa pesa za dawa na motisha kwa watumishi wa afya,pia uhaba wa watumishi.Amesema serikali ijitahidi kuleta pesa kwa wakati ili kuwezesha huduma.MY TAKE: DMO atambue serekale makini ya CCM haijaleta magonjwa
DMO ndie anaesema ukweli sababu yeye yuko kwenye field, kama hela haijaletwa basi haijaletwa tu.
Adanganye kua Pesa na madawa zimeletwa na kila kitu kiko poa si hawatampa then atakaehangaika ni yeye??
 
Sasa mkuu amemkashifu kivipi hapo?? Au MTU akisema ukweli inakuwa kumkashifu mkuu??
 
Akiongea mbele ya Naibu Waziri Selemani Jafo,Mganga Mkuu wa Iramba ametoa taarifa kuwa hawajapokea fedha za Madawa toka July 2016!!DMO alijikita zaidi kuonyesha uhaba wa pesa za dawa na motisha kwa watumishi wa afya,pia uhaba wa watumishi.Amesema serikali ijitahidi kuleta pesa kwa wakati ili kuwezesha huduma.MY TAKE: DMO atambue serekale makini ya CCM haijaleta magonjwa
Angalia usikute uliomuiga kauli hii ya your take ni mmoja kati ya wanne .source takwimu ya tafiti
 
Msema ukweli ni mpenzi wa Mungu.... ndo anavo
sema no 1 wetu na kuonyesha yuko serious na hilo alimtumbua mkuu wa shy ndani ya mwez mmoja kwa kusema uwongo... sidhani kama DMO anaweza mdanganya waziri tena hadharani na kwa suala la pesa kuletwa .... huo ndo ukweli alio sema na hawawez mfanya kitu .... wakimgusa tu... mkulu wa shy arudishwe.... ha haa haaa haaaaa.... tz yangu....
 
Dawa za nini. Kachimbeni mizizi mnywe mbona babu zenu zamani walikunywa miti shamba na walipona? Hapa kazi tu mlifikiri lelemama viwanda haviwezi kuja kwa kuendekeza mambo madogomadogo kama haya.
 
Back
Top Bottom