KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa amesema Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta ni mtu hatari ambaye CHADEMA kimegundua kuwa anaweza kufanya lolote kupata madaraka.
Dk. Slaa alisema Sitta hatakiwi kuaminiwa kwa kuwa hata alipokuwa spika, huku akiwa mwana CCM, mara kadhaa alijaribu kuomba kujiunga na CHADEMA iwapo CCM ingemtosa.
"Huyu mtu haaminiki hata katika dhamira yake, kwa kuwa tulikutana zaidi ya mara 100 na hata tukawa tunaandikiana vimemo, yeye akiwa katika kiti cha spika. Kama anabisha leo akanushe juu ya uhaini wake dhidi ya CCM," alisisitiza Dk. Slaa.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana mjini Iringa wakati akizungumza na waandishi wa habari, akijibu kauli iliyotolewa na Sitta aliyedai kwamba CHADEMA hakijastahili kupewa madaraka kwa kuwa hakina watu wenye uzoefu wa uongozi.
Sitta alidai mwenye uzoefu wa uongozi ndani ya CHADEMA ni Dk. Slaa pekee; akashutumu Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, kwamba uzoefu pekee alionao ni kuongoza kumbi za disko.
Sitta ambaye ni Mbunge wa Urambo Mashariki (CCM), na ambaye yumo katika fitina za kimakundi ya wanaoutaka urais ndani ya CCM, alisema hayo mjini Karagwe wiki hii, kama njia ya kijikweza mbele ya umma; na kuwashusha viongozi wa CHADEMA, ambacho chini ya uongozi wa Mbowe kimejengeka kuwa chama kikuu cha upinzani kinachotishia kuiondoa CCM madarakani.
Akijibu hoja hiyo, Dk. Slaa alidai kuwa mara kadhaa walizokutana, Sitta akiwa Spika wa Bunge alimweleza kuwa ana kundi la wabunge 55 waliokuwa tayari kuondoka katika CCM, na kwamba wangefanya hivyo siku tatu kabla ya Bunge la mwaka 2010 kumalizika.
CHANZO: GUMZO LA JIJI
Dk. Slaa alisema Sitta hatakiwi kuaminiwa kwa kuwa hata alipokuwa spika, huku akiwa mwana CCM, mara kadhaa alijaribu kuomba kujiunga na CHADEMA iwapo CCM ingemtosa.
"Huyu mtu haaminiki hata katika dhamira yake, kwa kuwa tulikutana zaidi ya mara 100 na hata tukawa tunaandikiana vimemo, yeye akiwa katika kiti cha spika. Kama anabisha leo akanushe juu ya uhaini wake dhidi ya CCM," alisisitiza Dk. Slaa.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana mjini Iringa wakati akizungumza na waandishi wa habari, akijibu kauli iliyotolewa na Sitta aliyedai kwamba CHADEMA hakijastahili kupewa madaraka kwa kuwa hakina watu wenye uzoefu wa uongozi.
Sitta alidai mwenye uzoefu wa uongozi ndani ya CHADEMA ni Dk. Slaa pekee; akashutumu Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, kwamba uzoefu pekee alionao ni kuongoza kumbi za disko.
Sitta ambaye ni Mbunge wa Urambo Mashariki (CCM), na ambaye yumo katika fitina za kimakundi ya wanaoutaka urais ndani ya CCM, alisema hayo mjini Karagwe wiki hii, kama njia ya kijikweza mbele ya umma; na kuwashusha viongozi wa CHADEMA, ambacho chini ya uongozi wa Mbowe kimejengeka kuwa chama kikuu cha upinzani kinachotishia kuiondoa CCM madarakani.
Akijibu hoja hiyo, Dk. Slaa alidai kuwa mara kadhaa walizokutana, Sitta akiwa Spika wa Bunge alimweleza kuwa ana kundi la wabunge 55 waliokuwa tayari kuondoka katika CCM, na kwamba wangefanya hivyo siku tatu kabla ya Bunge la mwaka 2010 kumalizika.
CHANZO: GUMZO LA JIJI