Dkt. Slaa: Sitta ni kielelezo cha mfumo uliooza, mlinda mafisadi na ufisadi

Mkuu Chintu;
Utatufanya tukufuru bure mbele ya Mungu; ikiwa Slaa ni chaguo la Mungu basi utawafanya watu wengi sana wahoji hekima za Mungu ndio sababu nakuambia usimchanganye Mungu kabisa na kahaba huyu; labda kama Mungu wenu ni kuwachonga kama wa kihindi; huyu aliyekuwa akiwalamba wanakwaya na wanamaombi ndani ya nyumba ya Bwana; misalaba kila kona hakumuogopa Mungu; kweli wewe unataka kuanimbia katika mamilioni ya watanzania awe huyu mtu mchafu mzinifu mkubwa kama Slaa; hivi kabla ya kuandika huu utumbo akilia yako ilikuwa 100% ? Hayo madude mnayobwia angalieni sana yatawatia uchizi.

Chama
Gongo la mboto DSM

....imenisaidia kujua naongea na mtu mwenye upeo gani?
 
Hon:6 kajitakia kagusa pabaya, anapima kina cha maji kwa njiti ya kiberiti? Ndiyo basi tena hatapata nafasi ccm walikuwa wanamtafutia sababu wamejua ukweli alivyo ndumila ku wili, hata hao mawazili/wabunge 55 watamkimbia na kumkana hadharani hakuna anayetaka aibu. Sioni msafi ccm.
 
Mpaka sasa nashindwa kukubali kuwa Dr Slaa hakujua kuwa kina Sitta walikuwa wakiwatumia kwa ajili ya kulinda maslahi yao ndani ya CCM kama ambavyo wamekuwa wakitumikantangia uchaguzi wa 1995.

Pia nashindwa kuchagua ama nimpongeze Dr Slaa kwa kujiingiza mkenge wa kuthibitisha jinsi alivyo na hulka ya uropokaji cum ukurupukaji uliokosa mahesabu mapana ya kisiasa ama kumuonea huruma kwa kuthibitisha jinsi gani anavyoweza kuwa Amiri Jeshi Mkuu asiyeweza kuaminika iwe kwa wanauslama wake na siri za nchi ama viongozi wenzake wa ndani na nje kuhusiana na usalama wa mazungumzo yao siri ambayo ndio msingi mkuu wa diplomasia ya uongozi wa aina yoyote ile.

Kikubwa zaidi ni kuwa Dr Slaa ameweza kumjibu Sitta kwa kuonyesha kuwa ukweli ni kuwa ukitoa muonekano wa haiba ya kiblazameni, ukweli Mbowe is better in wisdom, trustworthy and political calculations than the rogue Dr Slaa. Labda nguvu za giza za posho ya shilingi milioni 7 kwa mwezi zipo kazini!

Nachelea kusema kuwa maisha ya Mzee wetu huyu kisiasa yanaendelea kunithibitishia mapenzi ya mungu kwa Tanzania yetu ambaye daima amekuwa akitupa nafasi watanzania kuwapima na kuwajua zaidi viongozi wetu kama ilivyokuwa kwa Mzee Lyatonga Mrema, Mtikila na sasa Mzee wetu Dr Slaa.
 
Kwanza kabisa nngependa kufahamu huyu jamaa ni nani?? Uhusiano wake na Zitto Kabwe ni upi?? Sijiingizi katika kujadili mtu lakini kama Twittfam mmoja wapo huwa naona mahusiano mema yaliyopo kati ya hao vijana tajwa hapo juu!!

Je haya yaweza kuwa mawazo ya vijana wengi ndani ya Chama kuhusu viongozi wao??

Natambua huyu si Kiongozi wa Chama lakini anaweza kuwa mwanachama! Vijana tunapoanza kuleta visa na mikasa ndani ya chama si busara na si Afya kwa ukuaji wa Chama. Tujisahihishe!!

Omar Ilyas ‏@omarilyas

Dr Slaa amefanikiwa kumjibu Sitta kwa kuonyesha kuwa ukitoa muonekano wa haiba ya kiblazameni aliyonayo Mbowe...


Omar Ilyas ‏@omarilyas ...Mbowe is better in wisdom, trustworthy and political calculations than the rogue Dr Slaa...

 
Kwa kukusaidia mimi si mwanachama wa CHADEMA wala CCM ingawa hapo kala nilikuwa naunga mkono juhudi za CHADEMA kutokana na imani yangu ya umuhimu wankujenga mfumo madhubuti wa siasa za demokrasia ya vyama vingi ingawa kiitikadi na tamaduni za kisiasa navutiwa zaidi na kujinasibisha na misingi asilia ya CCM. Mengine yawe ya kweli, uzushi na ya kufikirika yatafuata kutoka kwa wale wanaonijua pamoja na wale wanaodhani wananifahamu.

Karibu...
 
Kwa kukusaidia mimi si mwanachama wa CHADEMA wala CCM ingawa hapo kala nilikuwa naunga mkono juhudi za CHADEMA kutokana na imani yangu ya umuhimu wankujenga mfumo madhubuti wa siasa za demokrasia ya vyama vingi ingawa kiitikadi na tamaduni za kisiasa navutiwa zaidi na kujinasibisha na misingi asilia ya CCM. Mengine yawe ya kweli, uzushi na ya kufikirika yatafuata kutoka kwa wale wanaonijua pamoja na wale wanaodhani wananifahamu.

Karibu...

Safi sana Mkuu!
Nilidhani tuko pamoja, nashukuru kwa maelezo haya!!
 
ansbert ngurumo leo kamchanachana mr 6 na kumuweka pale anapostahili.....
nina ujasiri wa kusema mr 6 ni baba wa unafiki wote uliomo ccm.

ilikuwa ccj, chadema..nex?


READ ON...............


[COLOR="#0000CD"[SIZE=3]]

[COLOR="#0000FF"]Hatujamjua Sitta halisi?



Ansbert Ngurumo




VIGOGO hawa wawili wanafanana tabia za kisiasa, ingawa wanatofautiana kimtazamo. Ni Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta.

Mwaka 2005, Kikwete alikuwa amepangwa na kujipanga kushinda urais kwa gharama zozote. Kwa kutazama vigingi vilivyokuwa mbele yake ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), akatafuta mahali pa kuponea.

Alizungumza na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwamba iwapo angekwamishwa, akakosa kuteuliwa na CCM kuwa mgombea, ahamie CHADEMA na apewe fursa ya kugombea.

Ikumbukwe kuwa hadi mwaka 2005, CHADEMA ilikuwa haijawahi kuweka mgombea urais. Mwaka 1995, CHADEMA ilimuunga mkono Augustine Mrema wa NCCR-Mageuzi.

Mwaka 2000, CHADEMA ilimuunga mkono mgombea wa Civic United Front (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba.

Katika mara zote mbili, CHADEMA iliamini kwamba ili kupunguza nguvu za CCM, na ili kupata ushindi, vyama vya upinzani viunge mkono chama cha upinzani chenye nguvu katika ngazi zote – udiwani hadi urais.

Lakini tabia za kisiasa ndani ya vyama vyetu zimedhihirisha kwamba wanyonge wawili au watatu anapoungana dhidi ya mmoja mwenye nguvu, wanashindwa kirahisi, kuliko kama kila mmoja angetumia rasilimali na nguvu zake kumshambulia mbabe mmoja.

Na baadaye imedhihirika kwamba, baadhi ya vyama vipo kwa kuwa vimesajiliwa, lakini baadhi ya waanzilishi wake ni wanachama waandamizi wa CCM. Hivyo, wanatumia vyama hivyo kudhoofisha vingine.

Vile vile, imekuja kudhihirika kuwa baadhi ya vyama, haviwezi kuunga mkono vyama vingine, hata kama huko nyuma viliwahi kufaidi matunda ya kuungwa mkono na vyama hivyo hivyo. Ndivyo ilivyokuwa mwaka 2005.

Baada ya Kikwete kufanikiwa kuteuliwa na CCM kuwa mgombea urais, ilibidi CHADEMA waamue ama kuendelea kuiunga mkono CUF au waweke mgombea, CUF nayo iwaunge mkono.

Waliweka mgombea; CUF ikakataa kuwaunga mkono. Sina kumbukumbu kama NCCR-Mageuzi iliombwa kuwaunga mkono, lakini ninachotaka kusisitiza hapa ni kwamba kabla ya kujeruhiwa, CHADEMA kilikuwa kinaamini kwamba kuunganisha nguvu za vyama ni njia ya kukuza upinzani na kuiondoa CCM madarakani.

Lakini CHADEMA haikukua kisiasa hadi pale ilipoweka mgombea urais. Ikapata hamasa kitaifa. Wananchi wakapata fursa ya kujua sera za CHADEMA. Viongozi wakaanza kujipanga. Na chama kikapata kusoma alama za nyakati na kujipanga upya kabla ya 2010.

Lakini historia itabaki kuwa, katika roho hiyo hiyo ya kupenda kukaribisha “wageni” waje kugombea urais na kukuza chama, CHADEMA ilikuwa inajitia kitanzi cha kisiasa.

Kwa mfano, iwapo Kikwete angehamia CHADEMA mwaka 2005; kutokana na wimbi la Kikwete la wakati ule, na hisia za jamii dhidi ya serikali ya rais Benjamin Mkapa, ambazo baadhi zilichochewa na propaganda ya kambi ya Kikwete; leo hii CHADEMA ingekuwa madarakani, lakini ingepata shida kujitetea na kujisafisha na kashfa ya wizi wa pesa za EPA!

Mungu bariki, Kikwete hakuingia CHADEMA! Amepata urais kupitia CCM, ikawa fursa ya CHADEMA kumsoma na kumjua Kikwete halisi, ambaye amepeleka ombwe la uongozi ndani ya CCM – ombwe lile lile ambalo lingekuwa limehamia CHADEMA.

Leo hii, CHADEMA inaweza kusimama kifua mbele na kutamka bila aibu kwamba, “Rais Kikwete ni kiongozi dhaifu.” Kauli ambayo kama angeshinda urais akiwa CHADEMA ingekimaliza chama kile kile.

Kwa hiyo, mazingira ya kisiasa yaliyomnyima Kikwete fursa ya kuwa mgombea urais (au hata kuwa rais) akiwa katika CHADEMA, ni moja ya sababu ambazo zimeifanya CHADEMA ikue, ikomae na kuheshimika mbele ya Watanzania, hadi kufikia kuitetemesha CCM kwa miaka mitano mfululizo, na kutishia kuiondoa madarakani sasa.

Sasa limeibuka na hili la Samuel Sitta, ambaye mara mbili aliomba CHADEMA imteue kugombea nyadhifa mbili kuu - urais na uspika mwaka 2010.

Haikubaliki kwamba mtu yule yule aliyetamani kugombea kupitia chama hicho hicho mara mbili, leo anaibuka na kutoa kauli kwamba chama hicho hicho hakifai kukabidhiwa nchi. Na akasisitiza kuwa chama kina mtu mmoja tu – Dk. Willibrod Slaa – anayefaa kuwa rais, na anayejua uongozi!

Hivi yeye kama angefaulu kupitishwa na CHADEMA na akawa rais, angeongoza nchi kwa kushirikiana na Dk. Slaa pekee?

Hivi Samuel Sitta huyu huyu aliyewaziba midomo wabunge wasijadili na kuhitimisha sakata la Richmond bungeni, ndiye mwenye ujasiri wa kunyoshea kidole wengine?

Sitta huyu huyu aliyetishia kumfunga Dk. Slaa alipompelekea nyaraka za wizi wa EPA, akidai kwamba Dk. Slaa ameghushi, ndiye huyu anayejitokeza leo kumsifu mtu yule yule?

Sitta anasahau kuwa licha ya Dk. Slaa kuwa nyota katika chama hicho, naye ni tunda la CHADEMA inayokua na kuimarika.

Na anasahau kwamba kama CHADEMA ingeingia Ikulu, mfumo wake wa kuongoza nchi si ule anaoujua Sitta – uliotumiwa na CCM kwa miaka 51 sasa.

Anasahau pia kwamba serikali mpya inapoingia madarakani, haileti kila mtumishi na kumchomeka; bali hutumia watumishi wale wanaokuwamo, na kuingiza wachache kulingana na mahitaji ya huduma na mfumo.

Sitta hataki kuamini kwamba CHADEMA inao watu wengi wenye uwezo mkubwa unaoendana na zama na mahitaji ya kisasa, ambao hata hawajulikani kwake kwa maana hawaandikwi magazetini au kutangazwa kwenye televisheni.

Hivi kweli, miongoni mwa mamilioni ya Watanzania walio nyuma ya CHADEMA, inakosa wataalamu 15 wa kushika nyadhifa za uwaziri katika serikali (ndogo) ya CHADEMA?

Nakubaliana na majibu ya Dk. Slaa kwamba Sitta anatafuta madaraka kwa nguvu zote. Ndiyo maana alitumia mkutano wa udiwani Mwanza kutangaza nia yake ya kugombea urais badala ya kumpigia kampeni diwani husika!

Ni Sitta huyu huyu,, ambaye mwaka 2005 wakati wa kampeni, aliahidiwa uwaziri mkuu; lakini akaukosa baada ya kampeni – pale Rais Kikwete alipotafakari na kusema anapata shida kumpa uwaziri mkuu mtu ambaye yeye rais atamsalimia shikamoo!

Na hata hatimaye alipoupata Edward Lowassa, Sitta hakulala hadi kombora la Richmond lilipohitimisha kazi yake, Lowassa akaanguka. Hata ile timu ya “wapambanaji wa ufisadi” ndani ya CCM iliyoundwa na Sitta, haikuwa na mapambano yoyote dhidi ya ufisadi, bali ilikuwa na malengo mawili:

Kwanza, ilitaka kuangusha utawala wa Kikwete na Lowassa; ikamtoa Lowassa kafara kwa kile ambacho Rais Kikwete alikiita “ajali ya kisiasa.” Wanaojua sakata halisi la Richmond sasa watakubaliana nami kwamba, Sitta aliwaziba wabunge midomo wasijadili tena Richmond, kwa kuwa alikuwa ameshamwangusha “mbaya wake.”

Lakini, tatizo la Richmond limebaki pale pale hadi leo; na mafisadi wameendelea kutamalaki ndani ya CCM na serikali.

Mbaya zaidi, baadhi ya wale waliojiita wapambanaji wa ufisadi, wamekosa meno na ujasiri wa kuendeleza mapambano hayo. Wako wapi leo?

Pili, nia ya Sitta kuunda kikosi cha “wapambanaji dhidi ya ufisadi” ilikuwa kuua nguvu ya kina Dk. Slaa, Zitto na wabunge wengine wa CHADEMA na vyama vingine walioibua ufisadi ulioitetemesha serikali, na ambao sasa unakaribia kuiondoa madarakani.

Sitta alilenga kumlinda Kikwete na kumtosa Lowassa. Lakini matokeo yake, naye alitishiwa mara kadhaa kufukuzwa uanachama CCM; na walipoamini kwamba kazi imekamilika, kwa hasira ya kile alichowatendea huko nyuma, nao wakamnyang’anya uspika waliokuwa wamempa kumpoza.

Sasa amekosa vyote – urais, uspika, uwaziri mkuu! Alichobaki kufanya sasa, katika mbio za kuusaka urais, amewafuata makanisani wale wale anaowaita mafisadi.

Yeye akiingia kanisani na kuchangisha mamilioni, hakuna shida. Wenzake wakiingia kanisani na kuchangisha mamilioni yale yale, anadai wanatumia makanisa kujisafisha![/COLOR][/SIZE][/COLOR]
Wote wawili, Kikwete na Sitta, wamewahi kutamani kutua CHADEMA kupata urais. Mmoja amepata; mwingine amekosa.

Bahati nzuri, Rais Kikwete amekuwa muungwana katika matamshi yake dhidi ya CHADEMA, maana anakumbuka historia, na nafsi inamsuta.

Tatizo la Sitta, amekosa vyote, na (kama alivyosema Dk. Slaa) amepoteza kumbukumbu! Au hatujamjua vema Sitta halisi?


(Maswali Magumu, Tanzania Daima 2 Septemba 2012)
 
leo nkitutana na kijani lazma nmtie kofi hata moja tu..unafk wa kikwete,6 na nape hauna tofaut,uroho wa madaraka

unajua "unafiki" wa 6 ndiyo ulimpa nguvu dr slaa, zitto et el bungeni? na CDM ikaonekana ni makini, 6 asingekua spika CDM isingekua hapa ilipo. Inabidi kua sober kidogo unapotaka kumuita 6 mnafiki anayependa maslahi binafsi kuliko ya taifa.

6 kama angetaka kujaza tumbo angekua kama spika aliyemtangaulia tu (msekwa) na kua rubber stamp ya serikali bila kuiuma hata kidogo, leo hii angebaki kua spika na labda wangefikiria na kumpa urais 2015 kwa sababu ni "safe hands na mwanamtandao mzuri atakayewalinda". Hii ndiyo ingekua usaliti wa maslahi ya taifa na siyo vinginevyo.

Hii term "unafiki" imetungwa na Mbowe, wale waandishi wa mfukoni wakisaidiana na EL na kama CDM wanaitumia wanatupa wakati mgumu sisi wengine kuwaamini wako wapi haswa kwenye haya masuala ya ufisadi zaidi ya kua rhetoric tu ya kisiasa.(utapingaje ufisadi halafu unapanga strategy na EL na RA) kama siyo usanii na opportunism ya Mbowe na genge lake kwa watz maskini na wasio na upeo.
 
Ama kweli umdhanie ndiye kumbe siye.Hivi sitta ataweka wapi uso wake mbele ya umma wa CCM kwa tuhuma hizi?

huyu mzee ana uso mgumu sana mbona CCJ aliwatosa na pia juzi mafuta ya rwanda ambayo kagame aliyakataa , kwasababu yalikuwa na ethanol ya 12% kuliko waliyozoea kwa uasalama wa magari yao amabayo ni 6%, sitta baada ya kurudishwa hayo mafuta akapanga na mafisadi kuzunguka nchi zite za EAC kuhamasisha kuwa ethanol hiyo ni sawa tu ilikulinda masilahi ya wezi waliofanya ufisadi huo, leo umkubali kuwa ni msafi kivipi.tayari amefanikisha mafuta hayo yameshatumika kwenye soko hili na nchini.
 
hapo kale nilikua mfuasi wa Chadema mpaka nilipogundua kuwa ni chama cha kikanda na kidini na kinamtenga zitto. Halima Mdee huko huko kwenye twitter alikuelezea vizuri. Na mimi narudia huna jipya. huko kwenye twitter uridai kuwa jf ina wajinga mbona umo na wajinga sasa baki kwenye twitter. for your information twitter imeanzishwa na watu wa maghsribi unaoona ni mashetani
 
Inyoosheni hii thread ili tuijadili vizuri. Inaonekana kuna something interesting in it...
 
hapo kale nilikua mfuasi wa Chadema mpaka nilipogundua kuwa ni chama cha kikanda na kidini na kinamtenga zitto. Halima Mdee huko huko kwenye twitter alikuelezea vizuri. Na mimi narudia huna jipya. huko kwenye twitter uridai kuwa jf ina wajinga mbona umo na wajinga sasa baki kwenye twitter. for your information twitter imeanzishwa na watu wa maghsribi unaoona ni mashetani
Mkuu Shalom JF ni zaidi ya Dunia, hapa huwa wanakuja tu!
 
hiki ndicho kilichopo kichwani mwangu about ccm.

1. Sisiemu ni wezi na majambazi tu, wao furaha yao ni kuona wa tz wanakufa kwa umaskini, ujinga maradhi na rushwa wanazozifanya. Ova;
 
Omar Elias,Zito Kabwe, alberto Mhando, George Kahangwa tulikuwa wote UDSM 2001-2005 siasa za Daruso. Ni one of the learned brother!
 
Nimeanza kuamini DR Slaa anavuta mshiko wa ubunge kama kawaida. Nilikuwa najiuliza inakuwaje Dr. Slaa atulie kimya baada ya matokeo tata ya uraisi!! Wanamageuzi tulitegemea atoe angalau tamko kufuatia matokeo baada ya kura kuhesabiwa, tofauti na tulivyozoea.


hawa wanakondoo wanaokubali kila kitu kwa imani ya upofu ndiyo tatizo Tz na ndiyo wanafiki zaidi hata ya wanasiasa. Siasa haina unafiki, siasa siyo exact science au kitu professional na kwa hiyo wanasiasa wako huru kubadilika badilika siku hadi siku ili wapate tu nguvu ya kuongoza na yale yote yanayokuja na hiyo nguvu.

wewe mwenzangu mimi unapokua huna matumaini au umechoka na CCM jiulize mbadala wake ni akina nani na je umewachambua sawa sawa hawa watu au unafuata tu kiupofu upofu?

Kama alivyosema Kim Kardash hapo juu kua Dr Slaa amejivika joho lisilomtosha, yeye ndiyo mnafiki anayejifanya mwanamageuzi kumbe ni mwanasiasa anayetegemea maisha kupitia siasa na siyo kiongozi atayekuja kumaliza matatizo ya kiuongozi na kiutendaji Tanzania. Bora hata Kamanda Mbowe kuliko huyu SLaa (aliyekosa "ulaji" CCM akabahatisha CDM ili aanze maisha mapya ya kudanganya watz na kupata kula kupitia migongo ya wananchi. Upadri ulimshinda, biashara zilimshinda sasa analazimisha mikopo, ajengewe nyumba, apewe mshahara wake wa ubunge na marupu rupu yake yote (wakati siyo mbunge na hivyo kukigharimu chama chake) huyu mnamuita mzalendo kweli na mwenye nia ya ukombozi wa kweli wa Tanzania?
 
Kwa mara nyingine CDM wamechemka kujibu hoja juu ya uhaba wa viongozi wakushika dola kwa kukosa uzoefu,hata katika ajira za kawaida mtu mwenye uzoefu ni bora zaidi ya yule anayeomba kwa mara ya kwanza...Ni kweli dr.SLAA anakipawa cha uongozi na anajitahidi kuandaa vijana wasomi ili waweze kuimarisha chama chake....lakini kumsifia MBOWE kuwa anaweza kuwa kiongozi wa juu ktk serikali amechemka vibaya......coz ataburuzwa na mataifa ya nje,hamjashika dola mmeshaanza kuwa omba omba kwa mataifa ya ulaya....binafsi naichukia ccm kwa kuwa bado ni tegemezi kwa wafadhili wakati tuna kila kitu hata mh.sitta analitambua hilo !!!!!!!!!!!!!!
Hata kama alitaka kuhamia CDM siyo kosa kama aliona ndani ya CCM hapati support ya kupambana na ufisadi,lakini aligundua na CDM kimejaa watu huni tupu isipokuwa wewe Slaa.....nadhani huo ndiyo ukweli anaotupa Mh.Sitta !!!!!!!!!!!!!!!!
CCM bado ina hazina ya viongozi waadilifu....CDM kaeni kimyaaaaaaaaaaaaaaa..endeleni kuipa changamoto serikali yetu huku mkiandaa viongozi makini lakini siyo majangili kama......
 
Back
Top Bottom