Dkt. Mwaka akinukisha nini tena?

Dkt. Mwaka akinukisha nini tena?

Bi Eshe katetea dini zote, katetea Uislamu na katetea Ukristo sasa tusikie fyoko fyoko tena
 

Au duniani ya kwake Kisiwandui.
Ni nani huyu? Binafsi simfahamu na anadai Dunia nzima inamfahamu...mimi nipo Duniani sijaenda hata sayari ya karibu tu hapo. Nadhani pia anapaswa apunguze jazba. Ajielezee kwa utulivu mzuri. Amani haichafuki kirahisi kama anavyodhani. Na pengine anataka kuza jambo hilo analolizungumzia. Huyo Mwaka ni nani mpaka achafue amani? Some people are just to be ignored.
 
Kwani Mama hajawahi kusikia ulawiti, ubakaji, wizi nk ambao viongozi wa dini baadhi wanaufanya?.

Dr Mwaka amezungumzia utapeli wa baadhi ya viongozi wa dini sio wote, sasa kutetea viongozi wa dini, Ijulikane wale wahuni watajifichia hapohapo.

Mama alipaswa kukemea viongozi wa dini wale waovu baadala ya kuja mbele na kutetea matokeo yake itasababisha watu wamchafue zaidi huyo huyo anayemtetea maana mitandaoni na hizi technolojia vinaweza kuweka wazi mambo ya ajabu na kuzidi kuleta shida.
 
Tumsikie na huyu kuhusu wachungaji Feki

 
Dr Mwaka amezungumzia utapeli wa baadhi ya viongozi wa dini sio wote, sasa kutetea viongozi wa dini, Ijulikane wale wahuni watajifichia hapohapo.

=
Naungana na ufafanuzi uliotolewa na Mch. Hananja🙌
=

1663659654726.png

=
1663659716120.png
 
Hiki kibibi kina akili mbovu, yaani katukanwa shehe chenyewe kinang'ang'aniza justification eti maaskofu wametukanwa. Eti kesho takbri wao wanasema Mungu mmoja......nahisi kimekula michembe ikakizidi kimo. Ngoja nikale zangu kitimoto mie.
 
Huyo Dr kakosea sana, kwanza ni dr wa nini ??? tuanzie hapo. Huyu mama kaongea busara sana kumuomba huyo Dr aombe msamaha. Ila kuna upumbavu fulani hii nchi imeuruhusu na kujidai ni uhuru wa vyombo vya habari ila huko mbeleni utakuja kuleta mushkeli, wa mtu yoyote tu kukurupuka na kuongea haiwezekani vyombo vya habari vina mipaka. Dr kuingilia viongozi wa dini hilo ni kosa kubwa sana. Viongozi wa dini wanaongoza mamilioni ya watu , sasa huyo dr kapata wapi ujasiri huo?? Kama mama alivyosema hapo awaombe radhi viongozi wa dini asap.
 
Wanaofahamu huyu Mwaka kakinukisha nini tena wafunguke hapa, maana mpaka Bi Eshe aseme maneno haya, huyo Mwaka lazima kafanya madudu ya mwaka:

View attachment 2358428


Kama Dr Mwaka alimtaja shekhe alikosea. Sababu ni moja kwamba kiongozi wa dini ana umma watu wanaomuamini nyuma yake kuna maneno yanayoweza kuharibu amani na kuleta mtafaruku bila sababu

Tangu enzi za mitume na manabii Mwenyezi Mungu alikemea hili la kuwasemea vibaya wawakilishi wake.

HESABU 12:1-16​

Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi.​

Wakasema, Je! Ni kweli Bwana amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? Bwana akasikia maneno yao.​

Bwana akanena ghafula na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia, Tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje.​

Bwana akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili.​

Kisha akawaambia,Sikizeni basi maneno yangu;Akiwapo nabii kati yenu,Mimi,Bwana,nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto.​

Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?​

Hasira za Bwana zikawaka juu yao; naye akaenda zake.​

Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe kama theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma.​

Kisha Haruni akamwambia Musa, Ee bwana wangu nakusihi sana usituwekee dhambi juu yetu, kwa kuwa tumefanya ya upumbavu, na kufanya dhambi.​

Nakusihi, asiwe kama mmoja aliyekufa, ambaye nyama ya mwili wake nusu imelika hapo atokapo tumbo la mama yake.​

Musa akamlilia Bwana, akasema, Mpoze, Ee Mungu, nakusihi sana.​

Bwana akamwambia Musa, Je! Kama baba yake angalimtemea mate usoni tu, hangaliona aibu muda wa siku saba? Na afungwe nje ya kambi muda wa siku saba, kisha baada ya hayo ataletwa ndani tena.​

Basi Miriamu alifungwa nje ya kambi muda wa siku saba; wala watu hawakusafiri hata Miriamu alipoletwa ndani tena.​



Sisi tunachotakiwa ni kuwaombea katika hali zote za furaha na amani.

Ila mimi leo ndio nimemjua Huyu bi Eshe
 
Hivi Bwana yule ni Shekh wa Mkoa au mwenezi wa chama tozo
 
Back
Top Bottom