Dkt. Bashiru akiwa Bungeni

Dkt. Bashiru akiwa Bungeni

Huwa mnatuambia role model wenu kwa democrace ni USA, UK, SWEDEN ETC. Sasa najiuliza je huko wanakuwaga na mipasho na kejeli kama hizi?
Yaani huwa na husuda mpaka kwa marehem!
Sasa huyu Bashiru:, ni mtu ambaye anakula marupurupu ya ukatibu mkuu wa CCM, Ukatibu mkuu kiongozi japo kwa siku 33, Ubalozi, na bado ana kinuwa mgongo cha UDSM - Na kumbuka hapo ameisha hakikishiwa hela za bunge. Ya kila sitting na akiwa kwenye zile Kamati zake! Na mwisho kiinua mgongo cha ubunge! Je! Unaweza kujilinganisha na mtu huyo? Mpende mchukie hamumuwezi ameisha tangulia kwa muda mfupi tu! Acha husuda. Akipewa kazi Bashiru, anafanya kazi hiyo kwa kiwango cha juu sana - kazi yoyote hata ikiwa ni umesenger! Anauwezo mkubwa wa kupanga, kuongoza na kupata matokeo ambao huwezi kumuondelea kichwani.

De
Sasa hizo kazi za kuiba kura ili kupata ushindi ndo sifa hiyo?
 
Umeonaeeeeee?
CCM haijawahi kupata Katibu Mkuu mahiri zaidi ya Dk. Bashiru tangu baada Mzee Kawawa. Na bahati nzuri, ukweli huu unaoneshwa na wavimba macho wa upinzani ambao wanaijua kazi yake hasa wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2020. Na hao ndio wanaoshangilia wakifikiria ya kwamba labda 2025 watapata unafuu.
 
Mitano tena kwake , yaani kashindwa kutumia dola kubaki Ikulu , hahaaa hatareeeee
 
Hhahahahahaha nimecheka mno..hahaaa kuna mtu alisema juz huyu kazi yake kuuliza maswali ya nyongeza jaman nilichekaaaaa🤣🤣🤣
Yani apo anasikia sauti nyororo ya madame Mama la Mama akisema ukinizingua tutazinguana!
Nina wasalimia kwa jina la Jamuhuri!
Mapigo ya moyo wake yana piga kama swala aliyeko kwenye mikucha ya chui!
 
Huu ni wakati wa kumpa maneno ya faraja kwa mamneno "hili nalo litapita".
 
Anaweza hata kujinyonga kwa sonona
Amepigwa comeback ya kisanga kutoka kuapishwa ubalozi sijui katibu kiongozi mpaka uchimba chumvi ni hatari mno Mazee huyo jamaa kuendelea kukomaa bungeni ni kiboko aisee sema akwende zake huko walikua wanaongea chochote na slow slow wake mpaka eti alinunua ubao kupiga hesabu za tofauti ya trillion 1.5 yaani wanatuona sisi makolo kweli...
 
Back
Top Bottom