Dk. Masaburi ameonesha ukomavu wa kisiasa

lusaka city

Senior Member
Mar 17, 2015
146
116
ALIYEKUWA Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk Didas Massaburi hivi karibuni alijitoa rasmi kwenye kinyang'anyiro cha kuwaniaUspika kupitia Chama Cha Mapinduzi na bila kutafuna maneno alieleza kumuunga mkono Job Ndugai akisema ndiye kiongozi mwenye sifa.

Lakini pia Dk Massaburi alisema hatua yake hiyo ilikusudia kujenga umoja na mshikamano ndani ya chama hicho ambacho kimekuwa kikikumbwa na migogoro wakati wa uchaguzi unapowadia.

Ndugai (Job) alikuwa Naibu Spika wa Bunge na sasa ameomba kugombea nafasi ya Uspika kwa hiyo katika muktadha huo huo wa kuhakikisha Bunge linakuwa na kiongozi mahiri na mzoefu nitakuwa tayari kumuunga mkono Ndugai ili aweze kushinda nafasi hiyo na kuliongoza Bunge ambalo chini ya Rais Magufuli, Watanzania wote wanahamu ya kuona kuwa anapatikana Spika anayeweza kwenda na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano,? alikaririwa Dk Massaburi.

Kuhusu nini atakifanya baadaye baada ya kujitoa na kumuunga mkono Ndugai, Dk Massaburi alisema anaweza kulitumikia Taifa akiwa nyumbani kwake Chanika na si lazima kuwa Spika au Mbunge kuwatumikiwa Watanzania.

Kwangu mimi binafsi wakati leo Bunge linapata Spika, lakini nimelazimika kumpongeza Dk Massaburi kwa hatua yake hii ambayo ni lazima iwe mfano wa kuigwa kwa wagombea wa CCM na vyama vingine kwa kutong'ang'ania madaraka.

Dk Massaburi kwa kumuunga mkono Ndugai tena kwa kueleza bayana kwamba ana uwezo mkubwa na uzoefu unaotosha katika kuongoza Bunge ni kitendo kinachomdhihirisha kuwa ni kiongozi asiye mbinafsi na anayejali maslahi mapana ya chama chake na nchi yake na si maslahi yake binafsi na familia yake.
 
Aende huko chanika zingiziwa akafundishe wanafunzi kwenye
ile shule yake ya Dr . Didas Masaburi secondary school.....
 
Unaweza kumuona ni kiongozi wa aina gani kama ukitumia akili kufuatilia siasa zake. Unaweza kuona namna alivyojitoa mwanzoni na kumuunga mkono Ndugai na muda mfupi ujao Ndugai atakuwa spika, sasa mwanasiasa kama huyo si wa kumbeza kirahisi rahisi.
 
Hakika tunaitaji viongozi kama masaburi .nashangaa serikali imuache mtu kama yeye ni mtu muhimu kwa serikali ya tanzania.hakika ametumia elimu,busara yake na ukomavu wa kisiasa katika hili. Kweli ccm wana watu.
 
Inawezekana ni chuki binafsi lakini Dk Massaburi ni aina ya kiongozi anayehitajika kwa Tanzania ya leo.

Mwanasiasa ambae anatumia mwamvuli wa siasa kufanya maovu ndo unasema taifa linamuitaji?

Mwanasiasa ambae anaminya demokrasia kwa kuandaa maandamano fake eti akidai ni wanachadema hawamtaki lowasa

Wewe unaweza kuwa hawara wa masaburi sio bure
 
Inawezekana ni chuki binafsi lakini Dk Massaburi ni aina ya kiongozi anayehitajika kwa Tanzania ya leo.

Wewe nawe akili yako ipo kama ilichelewa kukomaa. Kenge kama Masaburi unathubutu kumpamba kijinga hivi!!
 
Hakuna haja ya kupaniki na kuwaita wenzio hawara, hapa tunajenga hoja, karibu kwa hoja si matusi.Hoja kwamba anaua demokrasia hiyo ni kazi ya mwanasiasa. We unadhani maneno yaliyokuwa yanasemwa na Lowassa, Sumaye, Mbowe na wengine kwa kutumia vijana kuidhibiti CCM hiyo sio uuaji wa demokrasia?
 
Suala la promo halipo, yeye mwenyewe umemsikia anasema ataijenga nchi akiwa Chanika, na kuanguka kwake si jambo la ajabu. Kumbuka aliwahi kugombea Ubunge wa Afrika Mashariki mara ya kwanza kura hazikutosha, mara ya pili akaibuka na ushindi mkubwa sana, hata sasa ameanguka kwenye ubunge anaweza kujipanga upya. Lakini pia kumbuka ni mshauri wa Benki ya Dunia kwa masuala ya Ugavi na Ununuzi, amekuwa Meya, amekuwa Mwenyekiti wa ALAT Taifa, amekuwa Mwenyekiti wa Serikali za Mitaa Afrika na Dunia. Unawezaje kusema huyo ni mtu mwepesi?????
 
Hakuna haja ya kupaniki na kuwaita wenzio hawara, hapa tunajenga hoja, karibu kwa hoja si matusi.Hoja kwamba anaua demokrasia hiyo ni kazi ya mwanasiasa. We unadhani maneno yaliyokuwa yanasemwa na Lowassa, Sumaye, Mbowe na wengine kwa kutumia vijana kuidhibiti CCM hiyo sio uuaji wa demokrasia?

Masaburi ni babako au ni wewe mwenyewe?
 
ni mwepesi kwani anaongoza taasisi nyepesi...mshauri wa benki ya dunia huyo mpiga dili...ushauri wake ni kwa msalhi yake binafsi...anapewa vibarua na watu wa benki ya dunia wanaotaka chochote toka kwake...wewe hujui jinsi alivyokuwa mtaalamu wa kupiga dili...vyeo vingi alivyovipata ni thru friends...hana mashiko ni sawa na jina lake na anafikiri kwa kutumia jina klake ...
 
Mtoa hoja nakubaliana na wewe moja kwa moja. Kwa mwanasiasa kuanguka ni ajali ya kisiasa, vinginevyo ingekuwa ukianguka huwezi inuka, mbona wakina Lowassa bado wapo kwenye game ingawa wamewahi kuanguka mara kibao.Mimi kilichonifurahisha Zaidi ni hatua ya yeye kumuunga mkono Ndugai na kuamua kujitoa. Dk Massaburi hakukatwa bali amejitoa huu ni ukomavu wa kisiasa tena wa hali ya juuu.
 
Si lazima ndani ya jamii forum tuwe negative kwa kila jambo. Why watu wapaniki. Hoja ni kujiondoa kwa Dk Massaburi kwa kumuunga mkono Ndugai ambaye leo anakuwa Spika wa Bunge la 11. Mnaompinga Dk Massaburi hamtazami mbele. Huyu mtu amesifiwa hadi na Kamati Kuu kwa kitendo hiki, sasa why tusimpongeze.?
 
Si lazima ndani ya jamii forum tuwe negative kwa kila jambo. Why watu wapaniki. Hoja ni kujiondoa kwa Dk Massaburi kwa kumuunga mkono Ndugai ambaye leo anakuwa Spika wa Bunge la 11. Mnaompinga Dk Massaburi hamtazami mbele. Huyu mtu amesifiwa hadi na Kamati Kuu kwa kitendo hiki, sasa why tusimpongeze.?

Kamati kuu ya nini? Mlete Ubungo uone hata kamati ndogo kama itamchagua. Kaogopa bakora huyo
 
Suala la promo halipo, yeye mwenyewe umemsikia anasema ataijenga nchi akiwa Chanika, na kuanguka kwake si jambo la ajabu. Kumbuka aliwahi kugombea Ubunge wa Afrika Mashariki mara ya kwanza kura hazikutosha, mara ya pili akaibuka na ushindi mkubwa sana, hata sasa ameanguka kwenye ubunge anaweza kujipanga upya. Lakini pia kumbuka ni mshauri wa Benki ya Dunia kwa masuala ya Ugavi na Ununuzi, amekuwa Meya, amekuwa Mwenyekiti wa ALAT Taifa, amekuwa Mwenyekiti wa Serikali za Mitaa Afrika na Dunia. Unawezaje kusema huyo ni mtu mwepesi?????

Hizi kampeni unazomfanyia hapa sijui anagombea nini yaillah toba
 
  • Thanks
Reactions: amu
Back
Top Bottom