Dk. Masaburi ameonesha ukomavu wa kisiasa

Dk. Masaburi ameonesha ukomavu wa kisiasa

Suala la promo halipo, yeye mwenyewe umemsikia anasema ataijenga nchi akiwa Chanika, na kuanguka kwake si jambo la ajabu. Kumbuka aliwahi kugombea Ubunge wa Afrika Mashariki mara ya kwanza kura hazikutosha, mara ya pili akaibuka na ushindi mkubwa sana, hata sasa ameanguka kwenye ubunge anaweza kujipanga upya. Lakini pia kumbuka ni mshauri wa Benki ya Dunia kwa masuala ya Ugavi na Ununuzi, amekuwa Meya, amekuwa Mwenyekiti wa ALAT Taifa, amekuwa Mwenyekiti wa Serikali za Mitaa Afrika na Dunia. Unawezaje kusema huyo ni mtu mwepesi?????
Jamani huyu masaburi anaishi wapi? Mbona alivyokuja kugombea ubunge ubungo watu walimkataa wakamwambia tunataka mkazi wa ubungo hatutaki wa chanika akajibu yeye haishi chanika anaishi ubungo?
 
Dr Masaburi ni kiongozi mzoefu na mkomavu ktk siasa ya nchi yetu.Hakika tunahitaji viongozi wa aina hii
 
suala la UDA lipo wazi Dk Massaburi ameongeza bei ya uuzwaji kutoka Bilioni 1 hadi bilioni 5.7, na akaivunja Bodi ya UDa kwa wizi, halafu akafichua Sh milioni 300 kuwa zimeingia kwenye akaunti binafsi ya Iddi Simba. Huyu ni shujaaa. Uda ilikuwa inakufa kama yalivyokufa mashirika kibao ya umma. Uda ipo mtaani na tunapanda kila siku, kosa hapo liko wapi hebu tuwe specific.
Hahaha! Promo at work, kamuulize masaburi anamiliki asilimia ngapi ya hiyo uda ndio utapata jibu, halafu masaburi alisema wabunge wa dar wanafikiri kwa kutumia makalio iweje agombee dar
 
Samahani,ukiwa jimboni Ubungo,Chanika inapatikana sehemu gani?

sasa chanika na ubungo wapi na wapi???? huko ulizia gongola mboto au pugu kajiungeni ndo sehemu za karibu na chanika.
 
sasa chanika na ubungo wapi na wapi???? huko ulizia gongola mboto au pugu kajiungeni ndo sehemu za karibu na chanika.

Nilidhani Ubungo kuna mtaa unaitwa Chanika,sasa huyu mgombea mstaafu wa jimbo la Ubungo kumbe si mkazi wa jimbo la Ubungo?
 
sasa chanika na ubungo wapi na wapi???? huko ulizia gongola mboto au pugu kajiungeni ndo sehemu za karibu na chanika.

Nilidhani Ubungo kuna mtaa unaitwa Chanika,sasa huyu mgombea mstaafu wa jimbo la Ubungo kumbe si mkazi wa jimbo la Ubungo?
 
huu ni usanii tu kama mwingine.kama alijua ana uwezo kwanini aligombea.angeenda akamwuliza kabla vpi mwenzangu utagombea maana una uwezo au amshawishi ili yeye asichukue fom.kaona maji ya shingo ndo anaweka mpira kwapani
 
Kwa wanaojua kucheza na siasa duniani kote watajua jamaa ni mzuri sana kichwani na anakubalika. Siku Mbili kabla anajitoa na kutangaza kumuunga mkono Ndugai. Then Ndugai huyo huyo anashindwa kwa kura za CCM na za Ukawa pia maana Ole Medeye kapata kura 109 kati ya wabunge 122 wa Ukawa. Unawezaje kumbeza mtu makini kama huyo, ipo siku wapinzani wake wote mtamuamkia Shikamooooo.
 
UDA si hoja tena maana kila anayetoa hiyo hoja anazungumzia mambo ya kufikirika au alfu lela ulela. Eti Massaburi ana hisa UDA mara aliuza shirika, jamani angalieni historia.Ukweli ni kwamba vinega tunataka nchi iongozwe na mapoyoyo na tunadhani ni sifa na wakati huo huo tunataka tuendelea kama watu wa Dunia ya Kwanza. Ni ndoto ya Mchana.
 
Ya hata mimi katika hilo nimegundua jamaa mtandao wake bado ni very strong katika siasa. kilichotokea Ubungo ni ajali ya kisiasa tu. Ni kama yaliyomkuta Lowassa, Hashim Rungwe, Kafulila, Machali na wengine wengi. Dk Massaburi si wa kubeza aisee.
 
And then suala la yeye kukaa Chanika si issue, si lazima mtu awe na makazi sehemu moja. Ndio maana unaona leo Pinda anaishi Pugu lakini alikuwa anaishi pia Masaki na anagombea Katavi na wengi wako hivyo. Hivi Kubenea ni mkazi wa Ubungo? nafahamu Dk Massaburi ameishi sana Ubungo kuliko mahala pengine popote Dar. Ni basi tu upepo wa mabadiliko umepita basi watu wameacha vichwa wakachagua magalasa. Subirini miaka mitano itakuwa 20.
 
Si kweli wale vijana ni wa Chadema, hivi dunia ya leo utamtuma kijana gani na akubali kufanya jambo la hatari? vijana wameelimika na ndio maana Ukawa walipopanga maandamano kupinga matokeo wakaambulia patupu. Kosa lake nini; kwamba hakupaswa kuwapongeza wakati wameandamana kumuunga mkono Dk Slaa ambaye alisema kweli na ukweli umejidhirisha kwenye matokeo ya kura. You guys msimuonee huyu mtu bwana.
 
Kwamba akiwa Meya hajafanya lolote hilo ni kawaida, si umesikia kila siku marais wanaambiwa hawajafanya kitu, lakini wanaosema hivyo wanaenjoy jasho la hao viongozi wanaosema hawajafanya kitu.Hata Sumaye na Lowassa Mawaziri Wakuu walidiriki kusema hakuna kilichofanyika na tuliwashangilii jukwaani. sijui tumerogwa na nani
 
Masaburi hafai hata kuwa monita darasani hafai hafai
 
Waulize madiwani wa Dar watakwambia uzuri wa Dk Massaburi. Watanzania wenye akili fupi wanadhani kila anayefanikiwa kimaisha ni fisadi au mwizi. Huo ni wendawazimu tufanye kazi jamani ili maisha yetu yabadilike. Dk Massaburi ni mtaalamu wa ugavi na manunuzi aliyebobea. Kichwa chake ni msaada kwa Afrika na Dunia. Subirini mtamsikia wadhungu watakavyomgombania kama mpira wa kona.
 
sasa yale makovu ya uhasama aliyotuachia ubungo itakuaje?? Namkubali sana Masaburi maana hata juzi alikiri kuwa fitna ni mbaya na hakuamini kuwa hata wana ccm wenyewe kwa wenyewe wanaweza kufitiana....yani alidhani yale maovu aliyoyatenda kwa Chadema yatabaki huko huko tu.
 
Aondoke zake kwanza hana busara, alitumika kuwapandikiza vijana wa CCM kufanya fujo kwa kivuli cha CDM. Hana hekima Masaburi wa masaburi
 
Back
Top Bottom