Dk Aman kuvuliwa Umeya Bukoba anguko la Waziri Kagasheki

Yeye Kagasheki amekubali kufanyia mkutano wa Halmashauri kuu ya CCM ya Wilaya kwenye UKUMBI UNAOMILIKIWA NA KANISA!!!.

Wenzake wa Muheza walikataa katakata kufanyia mkutano kwenye ukumbi unaomilikiwa na kanisa. Lakini ajabu wanakubali kufanya kazi na kutibiwa kwenye hospitali ya wilaya ambayo ni mali ya kanisa inaitwa TEULE. Wahenga waliosema Baniani mbaya kiatu chake dawa walikuwa na AKILI.

Mkuu Bobuk!

Wewe Umenena!!!

Bonde bado kabisa Mkuu! Kumbuka shule ya kwanza kabisa Tanganyika ilijengwa Muheza Magila. Leo hii Muheza ndiyo imekuwa Bongo lala.
 
Kilichomleta Kagasheki sio hicho kikao bali ni Mauaji yaliyofanywa na mwanae maeneo ya Kibeta. Mtoto wa Kagasheki amemgonga mzee mmoja kwa gari na kufariki papo hapo.Kagasheki ilimlazimu afike Bukoba kuweka mambo sawa.
Mzee hizo ni nusanusa cum intelligentsia, kumbe wanawapa watoto magari na wanauwa watu sio????
 
Haya mambo ya uchaguzi si yanafuata katiba ya chama??? Tusubiri wakati ukifiak wa kugombea watu watupe karata zao, tuache kupakaza kabla ya wakati!!!!

Mkuu sawa hoja yako inamashiko,lakini kumbuka kuwa rwakatare ameshashindwa chaguzi kuu mbili zilizopita,unataka ushahidi gani zaidi ya huu!!
 
Madiwani nao wakimvua Umeya ni wajinga kama kagasheki.

Mparaganyiko wa Magamba.
 

Mkuu sawa hoja yako inamashiko,lakini kumbuka kuwa rwakatare ameshashindwa chaguzi kuu mbili zilizopita,unataka ushahidi gani zaidi ya huu!!

Mkuu huu uchaguzi wa mwisho si alinganganiwa na mtandao wa Mhe Kagasheki akiwa Mkuu wa mapolisi CCM????Tueleze kama Wilbrod Rwakatare ana kashifa yoyote tuelewe!!!
 
Mkuu huu uchaguzi wa mwisho si alinganganiwa na mtandao wa Mhe Kagasheki akiwa Mkuu wa mapolisi CCM????Tueleze kama Wilbrod Rwakatare ana kashifa yoyote tuelewe!!!
Hana kashifa yeyote mkuu,lazima ufahamu siasi ni upepo,siyo watu wote wana busara kama wewe,wapigakura wengi hufuata upepo unapoelekea,kwa sasa upepo wake siyo mzuri kisiasa ukilinganisha na ule wa mwaka 2000.
 
Hana kashifa yeyote mkuu,lazima ufahamu siasi ni upepo,siyo watu wote wana busara kama wewe,wapigakura wengi hufuata upepo unapoelekea,kwa sasa upepo wake siyo mzuri kisiasa ukilinganisha na ule wa mwaka 2000.
Basi Mkuu kama mnaona hivyo anzeni kumjenga mapema kama sio yeye look for some one else maana udongo uhuwahi ungali maji!!!! Kama zege mkuu hailali!!!

 
Basi Mkuu kama mnaona hivyo anzeni kumjenga mapema kama sio yeye look for some one else maana udongo uhuwahi ungali maji!!!! Kama zege mkuu hailali!!!
Kweli kabisa ni lazima tuwe flexible,rwakatare anaweza kuendelea kutusaidia kwenye nafasi nyingine,bila ya hivyo kila siku tutaambulia misiba isiyokuwa ya lazima!!
 
Akina Kagasheki ndo wanatufanya Wahaya tudhalauliwe hata na watani wetu akina Mura. Bukoba haitakiwi uonekana masikini sana kama ilivyo. Ila walau tuna uwanja wa ndege unaozidi wa Singida
 
Mkuu huu uchaguzi wa mwisho si alinganganiwa na mtandao wa Mhe Kagasheki akiwa Mkuu wa mapolisi CCM????Tueleze kama Wilbrod Rwakatare ana kashifa yoyote tuelewe!!!
Dr Slaa aliongoza kwa kura Jimbo la Bukoba mjini akifuatiwa na Jakaya Kikwete, kama unajuwa hesabu vizuri nadhani unaelewa vyema kwamba nani alipaswa kuwa Mbunge wa Bukoba mjini and why not.
 
Dr Slaa aliongoza kwa kura Jimbo la Bukoba mjini akifuatiwa na Jakaya Kikwete, kama unajuwa hesabu vizuri nadhani unaelewa vyema kwamba nani alipaswa kuwa Mbunge wa Bukoba mjini and why not.


Mkuu Matola, siasa za bukoba haziendi haziko hivyo. Mwaka 2000 mgombea uraisi kwa tiketi ya CCM B.W.Mkapa alionogoza akifuatiwa na Prof Lipumba wakati Rwakatare akimgaragaza mgombea wa CCM Mjuni Kataraia. Pale wanachagua mtu kama mtu na siyo chama. Kagesheki anapendwa yeye kama yeye na wala siyo kupitia mgongo wa chama. Yawezekana likawa ndo jimbo pekee ambalo mgombea ubunge aliyeshinda ni CCM na rais akaongoza mgombea wa chadema. Hata mwaka 2000 CCM hicho kitu kiliwachanganya mpaka wakaamua kumvua mwenyekiti wa chama mkoa (A. Amani) uenyekiti na kusema kua siyo raia wa Tanzania.
 
Ni kweli mkuu nipo Bukoba Mjini nimeona baadhi ya Barabara zikikarabatiwa vizuri kabisa
bkb1.jpg

bkb2.jpg
bkb.jpg
 
Katika siasa lolote linawezekana. Dr. Aman (Medicine) anaweza kupokonywa Umeya lakini hili likitokea ccm Bukoba itavulugika na kusambaratika kabla ya muda wake 2015. Lakini katika mvulugano huu wote toka sasa Kagasheki na timu yake ndo hivyo inaondoka kwenye "Ngoma". Mzee Lwangisa kila mara anarejea usemi wake wa siku nyingi "Engoma, Eshuba Mbali Elagiile!"

Haya ni matokeo ya Fadhira za Kijima, kutaka ata uliyempangusa kamasi utotoni, kama amefanikiwa ukubwani basi akurambe miguu na kukuabudu. This is extremely too low for Kagasheki na his family. Kagasheki pamoja na elimu na kuishi nje, kitabia amebaki kuwa mjima wa kibepari. Yaani mbinafsi mwenye kutaka kuonekana mungu-mtu na kutukuzwa.

Kagasheki hana tofauti na USAID inayotengeneza utegemezi wa kifikra na kiutu kwa nchi za ulimwengu wa tatu maksudi ili iendelee kuwatawala kiulaini. Kazi za Mbunge zinafahamika bayana Kikatiba Ibara ya 63 lakini Kagasheki kang'ang'ana na misaada uchwara utadhani ndiyo kazi ya Mbunge ilihali yale ya msingi na muhimu hayatekelezi. Wanapotokea wenye uwezo wa kuyatekeleza, Kagasheki anageuka kikwazo. Angalia aina ya misaada ya Kagasheki ambayo ndiyo anaita maendeleo:


  • Kuchangia vikundi vya umoja wa Kijima wa Wanawake
  • Kuchangia harusi, sherehe ya walimu, kipaimara, maulidi, hijja (Nyakojoga na Mecca), misiba, kurekodi kaswida na gospel
  • Msaada hiace ya abiria kuwa emergency van-ngoma iko kwenye mgonjwa kupata kibali cha kuitumia!

Hizi ndizo kazi za Mbunge wetu mfano wa kuigwa Kagasheki! Hii ni misaada ya kifedhuli na kuhaibishana na kufanyana wategemezi wa kudumu. Mbaya zaidi utoaji wa misaada ya Kagasheki lazima iwe na kufehedheshana ama wakati inatolewa au baada ya kutolewa. Kagasheki akikusaidia atakunanga mpaka ukome. Hili ndili limipelekea hivi karibuni Wakatoliki kukataa tena msaada wa siku nyingi wa usafiri wa waumini wao kwenda kuhiji Nyakijoga.

Kagasheki anataka kuwa juu ya kila kitu na kila mtu ndani ya chama na nje ya chama Jimboni. Amefikia hatua ya kutaka hata wanaojadili suala lolote juu ya maendeleo ya Kagera iwe ni kwa idhini yake kwanza. Hataki mkusanyiko wa Watu wa Bukoba ambao yeye hana control nao. Nimeshangaa katika mazungumzo juzi akikandia hata group-mails na majukwaa ya alumni wa-Kagera. Inasikitisha anaposhindwa kutetea hoja analeta vioja na kuingiza mdudu hatari sana-Udini!
 
UPDATE

Nimejitahidi nikashuka faster maeneo ya St. Francis na kukuta mkutano ukiendelea na nikaweza kuwahoji baadhi ya makatibu tawi na kata wa CCM walioko nje ya Ukumbi. Maelezo ya Katibu tawi wa CCM ambaye amesema hataji jina la tawi bali akataja ukanda wake ambao ni Bukoba (Green Belt) amesema mpaka hivi sasa Manispaa ya Bukoba yenye kata 14 imegawanyika katika sehemu mbili. Sehemu hizo ni Green Belt na Town Proper. Green Belt ina kata 8 na Town proper ina kata 6.

Kiongozi huyo anasema kitendo cha Kumvua Umeya Dr. Amani.............kitaleta vurugu maana hadi hivi sasa wamebeba kadi zao. Wanasema watarudusha kadi kwa katibu wa Wilaya na Mwenyekiti wake. Kiongozi huyo amesema Green Belt wote wamesha ambizana wako pembezoni simu zao ziko hewani.....tayari kwa kutaarifiana ili kurudisha kadi. Wanasema wao wataenda na Meya then Town Proper wabaki na Kagasheki. Hata hivyo ni kwamba baadhi ya Kata za Town proper hazimuungi mkono Kagasheki.

Waandishi wamezuiwa kuingia ndani ila kuna baadhi ambao wamejificha nyuma ya jengo wananasa habari za ndani. Mie nimeenda na gwanda langu la CDM......nikaona baadhi wananiangalia kwa jicho la ajabu nikatoka fasta na kukaa pembeni ndipo nikaanza kufanya mahojiano na jamaa wa CCM.

Kiongozi huyo anadai wanaoleta mgogoro ni jamaa wa karibu na Kagasheki kwa sababu inasemekana walimsaidia sana kuwa hapo alipo. Amesema kuwa watu hao wa Karibu hawataki soko kuu la Bukoba libomolewe na kujengwa jingine kwa sababu watu hao wanamiliki meza zaidi ya 10 sokoni hapo. Hivyo wanapokea malipo ya hizo meza kila mwezi. Kwa hiyo wanasema soko likijengwa upya itakuwa ngumu mafisadi hao kumiliki meza nyingi kama ilivyo sasa maana watanzania wengi zaidi watapata nafasi za meza hapo sokoni.

Pia mtu aliyetajwa kuleta mgogoro huo ambaye ni Ndugu yake Kagasheki ametajwa kwa jina la Ibanda. Kabla sijapata details kuhusu huyu Ibanda akatokea jamaa amevaa nguo ya CCM niliyekuwa namhoji akasitisha maongezi na mimi nikaondoka maana nilikuwa niko ki gwanda gwanda. Najua wenzangu walioko Bukoba hapa watatupa details kuhusu who is Ibanda.

Mzito Kabwela........tuwasiliane kama uko Bukoba
 
Back
Top Bottom