John Mnyika
JF-Expert Member
- Jun 16, 2006
- 713
- 1,245
Kwa siku kadhaa nilikuwa nimetoweka hapa JF. Kabla ya kutoweka nilishiriki mjadala mrefu kwenye FOCUS 2010 na CHADEMA must reform. Mara baada yake ukazuka mjadala wa Kabwe Vs Wangwe- Kisa cha Mafahali wawili ambao nao umechangiwa na kwa kiasi cha kutosha na naamini ujumbe umefika kwa wahusika.
Baadaye kidogo ukazuka mjadala wa matokeo ya uchaguzi Kenya mintaarafu uchaguzi wa 2010 kwa Tanzania. Katikati ya mjadala huo, kumezuka hoja ya kuiondoa CCM madarakani- lakini swali la ziada limezuka- kwa ajili gani? Nini kifuate baada ya kuitoa CCM madarakani?
Swali hili ni la muhimu sana linalohitaji mjadala wa peke yake. Nafahamu kila chama cha siasa kina dira, malengo na mwelekeo wake ambao umefafanuliwa vizuri katika falsafa, itikadi, na ilani yake.
Lakini swali ambalo ni vyema tukajadili, na hili ni la wananchi wote kwa ujumla bila kujali itikadi. Nini iwe Dira(vision) na utume (mission)- au tunaweza kusema Kauli Mbiu (hapa kuna kazi ya kutofautisha na Slogan) ya chama ama ushirikiano wa vyama ambavyo kwa kuwa nayo wananchi wawe na imani na utayari wa kuwakabidhi mamlaka ya kuongoza dola mwaka 2010 kama mkataba katika ya umma na viongozi watakaochaguliwa?
Kwa mfano; chama cha Democrat cha Marekani:
The Democratic Vision
The Democratic Party is committed to keeping our nation safe and expanding opportunity for every American. That commitment is reflected in an agenda that emphasizes the security of our nation, strong economic growth, affordable health care for all Americans, retirement security, honest government, and civil rights.
Guiding Principles
Our Plan
We have a bold new direction for a secure America. We seek: 1) Honest Leadership & Open Government, 2) Real Security, 3) Energy Independence, 4) Economic Prosperity & Educational Excellence, 5) A Healthcare System that Works for Everyone, and 6) Retirement Security.
Mjadala huu ni muhimu kwa kuwa naamini kabisa ushirikiano wa vyama kama wa CHADEMA, CUF, TLP na NCCR Mageuzi unapaswa kusikiliza matakwa ya umma kwa kiasi kikubwa. Swali hili ni muhimu kwa kuwa linaweza kutoka na ajenda za msingi za uchaguzi wa mwaka 2010.
Na ni vyema dira na utume huo ukawa katika sentensi chache ambazo zinaweza kukumbukwa kwa urahisi na ujumbe kusambazwa kwa urahisi nchi nzima na kuwafikia wananchi mpaka wa ngazi ya chini kabisa.
Mjadala huu ni kwa yoyote ambaye ana Tanzania anayoitaka ambayo anaona bado utawala uliopo haujaweza kuileta. Kama Mahatma Ghandi alivyowahi kusema, "kuwa wakala wa mabadiliko unayotaka kuyaona. Kijua ndio hiki, tusipouanika, tutautwanga mbichi!"
JJ
Baadaye kidogo ukazuka mjadala wa matokeo ya uchaguzi Kenya mintaarafu uchaguzi wa 2010 kwa Tanzania. Katikati ya mjadala huo, kumezuka hoja ya kuiondoa CCM madarakani- lakini swali la ziada limezuka- kwa ajili gani? Nini kifuate baada ya kuitoa CCM madarakani?
Swali hili ni la muhimu sana linalohitaji mjadala wa peke yake. Nafahamu kila chama cha siasa kina dira, malengo na mwelekeo wake ambao umefafanuliwa vizuri katika falsafa, itikadi, na ilani yake.
Lakini swali ambalo ni vyema tukajadili, na hili ni la wananchi wote kwa ujumla bila kujali itikadi. Nini iwe Dira(vision) na utume (mission)- au tunaweza kusema Kauli Mbiu (hapa kuna kazi ya kutofautisha na Slogan) ya chama ama ushirikiano wa vyama ambavyo kwa kuwa nayo wananchi wawe na imani na utayari wa kuwakabidhi mamlaka ya kuongoza dola mwaka 2010 kama mkataba katika ya umma na viongozi watakaochaguliwa?
Kwa mfano; chama cha Democrat cha Marekani:
The Democratic Vision
The Democratic Party is committed to keeping our nation safe and expanding opportunity for every American. That commitment is reflected in an agenda that emphasizes the security of our nation, strong economic growth, affordable health care for all Americans, retirement security, honest government, and civil rights.
Guiding Principles
Our Plan
We have a bold new direction for a secure America. We seek: 1) Honest Leadership & Open Government, 2) Real Security, 3) Energy Independence, 4) Economic Prosperity & Educational Excellence, 5) A Healthcare System that Works for Everyone, and 6) Retirement Security.
Mjadala huu ni muhimu kwa kuwa naamini kabisa ushirikiano wa vyama kama wa CHADEMA, CUF, TLP na NCCR Mageuzi unapaswa kusikiliza matakwa ya umma kwa kiasi kikubwa. Swali hili ni muhimu kwa kuwa linaweza kutoka na ajenda za msingi za uchaguzi wa mwaka 2010.
Na ni vyema dira na utume huo ukawa katika sentensi chache ambazo zinaweza kukumbukwa kwa urahisi na ujumbe kusambazwa kwa urahisi nchi nzima na kuwafikia wananchi mpaka wa ngazi ya chini kabisa.
Mjadala huu ni kwa yoyote ambaye ana Tanzania anayoitaka ambayo anaona bado utawala uliopo haujaweza kuileta. Kama Mahatma Ghandi alivyowahi kusema, "kuwa wakala wa mabadiliko unayotaka kuyaona. Kijua ndio hiki, tusipouanika, tutautwanga mbichi!"
JJ