Dini inaleta matabaka kwenye mahusiano

Dini inaleta matabaka kwenye mahusiano

thomas_360

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2015
Posts
1,456
Reaction score
1,436
Tanzania kuna Dini kuu mbili yaani kuna dini ya kikristo na uislamu...
Linapokuja kwenye maswala ya mahusiano huwa kuna matabaka au changamoto pale watu wawili wenye dini tofauti na wanapendana...
Watu wanaweza kuwa katika mahusiano ya kimapenzi lakini linapokuja kwenye swala la ndoa huwa ni changamoto kwani kuna upande unaweza ukapinga kabisa hilo swala.
Natamani Dini zote zingekuwa zinashirikiana katika kila jambo hasa kwenye mahusiano kusingekuwa na kipingamizi na ingewezekana iwekwe utaratibu ambao endapo watu wenye Dini tofauti wakiwa wanapendana na wanahitaji kuishi pamoja basi zifuatwe.
Leo hii unakuta mkristo anampenda mtu wakislamu au muislamu anampemda mkristu lakini unakuta MTU wakati mwingine anashindwa akiAnza kufikiria vikwazo vya hapo mbeleni!!

Natamani Kweli kusiwe na matabaka ambayo tunakutana nayo....I hope kuna watu walishakutana na hivi vikwazo na wanaendelea kuumia!!!
 
Watu wengi hawapendi ndoa za kiserikali halafu mzazi hayupo tayar mfunge ndoa ya hivyo au ndo ile anakuambia ukifanya hivyo ujue mm sio mzazi wako kuanzia sasa, kwa kauli kama hiyo unafikiri ni sahihi??
Kwa nini hawapendi wakati hata ukifungia kanisani kiapo unachoapa, ni cha kiserikali na hata cheti?
 
hakuna ndoa kati ya watu wa dini mbili tofauti bali ni uasi
 
Changamoto inakuja wakati mwingine nani atakaye kubali kubadilisha dini?? Na unakuta ilivyozoeleka ni kwamba mwnamke atamfuata mwanaume na ukute upande wa mwanamke hawapo tayar kwa hilo swala
Usilete Ujanja hapa badili dini umfuate Mwenzio la sivyo utamkosa.
 
Tanzania kuna Dini kuu mbili yaani kuna dini ya kikristo na uislamu...
Linapokuja kwenye maswala ya mahusiano huwa kuna matabaka au changamoto pale watu wawili wenye dini tofauti na wanapendana...
Watu wanaweza kuwa katika mahusiano ya kimapenzi lakini linapokuja kwenye swala la ndoa huwa ni changamoto kwani kuna upande unaweza ukapinga kabisa hilo swala.
Natamani Dini zote zingekuwa zinashirikiana katika kila jambo hasa kwenye mahusiano kusingekuwa na kipingamizi na ingewezekana iwekwe utaratibu ambao endapo watu wenye Dini tofauti wakiwa wanapendana na wanahitaji kuishi pamoja basi zifuatwe.
Leo hii unakuta mkristo anampenda mtu wakislamu au muislamu anampemda mkristu lakini unakuta MTU wakati mwingine anashindwa akiAnza kufikiria vikwazo vya hapo mbeleni!!

Natamani Kweli kusiwe na matabaka ambayo tunakutana nayo....I hope kuna watu walishakutana na hivi vikwazo na wanaendelea kuumia!!!

Dini ni mavi
 
Dini haileti matabaka, sisi watu ndio tunaleta matabaka. Kwani si kila mtu achukue anaempenda kutoka upande wa dini yake! Sasa ya nini uchukue kutoka upande mwingine!?

Unaona haya sasa?

Dini hizo hizo ndio zilizojengwa na mwanadamu huyohuyo halafu unasema dini hazina tatizo?

Dini inawekwa sehem ambapo haina kosa wakati mwanadamu mwenye mapungufu na makosa kibao ndio kaijenga yeye!

Hivi unatengaje kitu kilichojengwa na mjengaji?
 
Mm kuna binti wa kislamu nimemkubali kweli kweli lakini sasa nikianza kufikiria kuwa tupo dini tofauti nachoka kabisa!!
 
Back
Top Bottom