Diaspora amekufa wengine wanachekelea, kwanini?

Diaspora amekufa wengine wanachekelea, kwanini?

hannibali

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
468
Reaction score
428
Habarini za muda huu waungwana.

Majuzi kati kuna msiba ulitokea kuna jamaa mmoja alifariki lakini yeye alikuwa anaishi nchi za Scandinavia, umauti ulimkuta hukohuko lakini mwili wake ulisafirishwa kuja kuzikiwa huku, kitu kilichonishangaza ni kuona kuna baadhi ya watu walikuwa wanaonesha kufurahia kwa msiba huo kutokana na baadhi ya watu nilivyokuwa nikiwasikia wakizungumza.

Nanukuu mmoja nilimsikia akisema: "Unaona sasa hata ukijifanya kukimbia ulikotoka mwisho wa siku utafukiwa tu hukuhuku, kiko wapi sasa si huyu karudi"

Kwakweli nilistaajabu sana. Kuna mwingine pia alikuwa anasema: "Wanaenda huko mwisho wa siku hamna lolote wakifa kazi kuchangiwa nauli, si bora wabaki makwao tu"

Ama kweli ni maneno ambayo yalionesha waziwazi si mazuri hasa ukizingatia kwa mtu ambaye amekwishakata roho, ilipaswa aombewe anakokwenda apokelewe vizuri na muumba.

Sijajua tatizo ni nini kwa watu wa jamii ya huku (Bongo) ni kwamba hawawapendi diaspora au hawataki vijana watoke nje kuangalia fursa za maisha..ni nini kibaya kafanya yule kijana mpaka wamuongelee maneno ya namna ile.
 
Sio kila diaspora ana good life unless labda awe ana professional career huko abroad. Otherwise unakuta tu mtu ameamua kubadili mazingira ya ku hustle huko anafanya kazi za kawaida zenye kipato chakuweza kujikimu yeye na familia yake kama waliopo hapa bongo tu.

Tatizo tumekariri kuwa ukisikia mtu anaishi mamtoni basi ni milionea fulani au ana good life sana labda anaringa na presumption nyingine kibao.

Kikubwa tuache wivu na kupenda kuchukia maendeleo ya wengine. Kisa mtu katoka kaishi nje ya nchi watu wanakuwa na wivu kiasi cha kufurahia kifo cha mwenzao?
 
Suluhisho, msiruhusu watu wasio na uhusiano na marehemu kuhudhuria mazishi, iwe kama harusi ambaye hajaalikwa asije, kwani atakayekuja ni yule tu ambaye atakuwa ameguswa, na siyo kila takataka matokeo yake ndiyo hayo.
 
Suluhisho, msiruhusu watu wasio na uhusiano na marehemu kuhudhuria mazishi, iwe kama harusi ambaye hajaalikwa asije, kwani atakayekuja ni yule tu ambaye atakuwa ameguswa, na siyo kila takataka matokeo yake ndiyo hayo.
Utakataza mtu asiende kuzika?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom