Diaspora amekufa wengine wanachekelea, kwanini?

Diaspora amekufa wengine wanachekelea, kwanini?

Diaspora nao wana nyondo sana na wanasahau sisi walio tuacha huku manyovu kigoma ndo wachimba makaburi wao
Huu ni usemi wa kijinga mno. Nakumbuka kijijini kwetu kulikuwa na kikundi cha vijana waliokuwa wanachimba kaburi kwenye misiba mbali mbali. Kazi ya kuchima ni ya kujitolea na hufanywa na vijana wa kijiji husika.

Wengi ya waliokuwa kwenye hiki kikundi ni wanywa gongo na mara nyingi walikuwa wanatoa maneno kama uliyotoa wewe. Walifikia hatua ya kutishia watu walikuwa wanatoka mjini kwa kuwaambia ''angalia sana siku ukifariki hatutachimba kaburi lako''
 
Mimi siwezi kucheka msiba lakini siwapendi maana kuna diaspora mmoja alikuja kutoka Marekani na vingereza viingi hadi kanibebea Sikudhani wangu
 
Mimi siwezi kucheka msiba lakini siwapendi maana kuna diaspora mmoja alikuja kutoka marekani na vingereza viingi hadi kanibebea sikudhani wangu
Sasa kumbe ni mmoja inakuwaje useme huwapendi? Wengine wamekukusea nini?
 
Diaspora wengi wanarudi na iPhone tu, shenzi kabisa nyodo kibao kwa wachimba makaburi yao!
 
Wivu unatusumbua wabongo.

Roho mbaya tu hiyo, mtu asipige picha kidogo maneno yanawatoka watu

Sasa sijui wanataka mtu aishi kinyonge[emoji848]
 
Diaspora wakija likizo wanatusanif sana kumbe hawana lolote. Utasikia wakisema kule Ulaya, au kule kwa wenzetu hiki au kile, uchaguzi kule hauchakachuliwi, kule shit lakini wakifa michango ya kusafirisha maiti inatokea huku. Wengi hata nyumba nyumbani hawana. Wengi sana ni BBC au British bottom cleaners yaani wanaovalisha vikongwe wa Ulaya nepi lakini maringo kibao. Ukute sasa kaja na kigari left hendi toka ujerumani. Toyota zote wanaziona takataka.
 
Chanzo cha hayo yote ni CCM, hususani CCM ya Magufuli ndio imeongeza chuki kubwa dhidi ya Diaspora.

Taratibu tutaelewa tu, athari ya siasa za fikra za chuki dhidi ya wale wenye mitizamo tofauti na watawala wa Tz.
 
Tunarudi pale pale, wenye pesa, elimu nzuri na maisha mazuri huwa wana handle stress tofauti na masikini. Unaweza kwenda mapumziko, kubadili muonekano wa nyumba nk.
Maskini huwa achukulii stress kama tatizo. Na hapo ndio tatizo linapoanzia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom