Agogwe
JF-Expert Member
- Feb 20, 2013
- 2,742
- 3,009
Nyani Ngabu tafadhali hii mada inakuhusu
Watu wa hali ya chini huku uswazi kwetu hua hawanaga stress. Stress ziko Masaki, Mbezi Beach na huko Ununio. Sisi huku tembele, vibua, dagaa tukitoka nje Ni mnanda, mchiriku na taarabu za mafumbo.Tunarudi pale pale, wenye pesa, elimu nzuri na maisha mazuri huwa wana handle stress tofauti na masikini. Unaweza kwenda mapumziko, kubadili muonekano wa nyumba nk.
Maisha ni mapambano Kuna kupata na kukosa na pia huwezi kumlazimisha MTU ajenge TZ,acheni chuki za kishamba bongo hata mtu akiongea kingereza mnamwona anaringaAcha wasemwe.... ni nani asiyesemwa ....watu wanamsema Mwenyezi Mungu sembuse maiti?
Ila tukiacha utani tu na kujua jua kwingi.
Ni aibu.... umeishi nje kila mwaka unasafiri unakuja nyumbani na mbwembwe kibao unafikia Lodge halafu msiba unachangiwa na marafiki na wanarudisha kabegi tu na Iphone 11.
Tuache mengine hata watoto utawaachia aibu [emoji23][emoji23][emoji23]
Kikwetu....kuna msemo tunasema hizi ndizo zile aibu walizokuwa wanajinyongea babu zetu. Watu wa zamani walikuwa na aibu bwana....
Mkuu hizi sio chuki ni sheria zisizo rasmi za maisha tu.Maisha ni mapambano Kuna kupata na kukosa na pia huwezi kumlazimisha MTU ajenge TZ,acheni chuki za kishamba bongo hata mtu akiongea kingereza mnamwona anaringa
Kwa nini unawachukia wote wakati ni mmoja tu aliyekuhusu.Mimi siwezi kucheka msiba lakini siwapendi maana kuna diaspora mmoja alikuja kutoka marekani na vingereza viingi hadi kanibebea sikudhani wangu
Mrs kama Mrs!Yale mapicha mnayopiga pale Oslo s na kule Aker bridge yanawatoa roho
[emoji38][emoji38]Maskini huwa achukulii stress kama tatizo. Na hapo ndio tatizo linapoanzia.
Wapo wizarani[emoji38]Masikini hutamani watu wote wawe masikini kama wao,
Huyo marehemu hata kama angezikwa huko alipofia pia wangesema,wangesema "Unaona amezikwa nchi za watu,amekosa hata hela yakuja kuzikiwa Nyumbani" Binadamu hawakosi maneno hata ufanyaje huwezi kuwaridhisha,muhimu mtu ni kupambana kivyako tu na kuziba masikio kwa hawa masikini waliokwisha jikatia tamaa nakuamua kujiajiri kwenye wizara ya chuki na masimango.
Wala shida siyo kuwa Diaspora.Habarini za muda huu waungwana
Majuzi kati kuna msiba ulitokea kuna jamaa mmoja alifariki lakini yeye alikuwa anaishi nchi za Scandinavia, umauti ulimkuta hukohuko lakini mwili wake ulisafirishwa kuja kuzikiwa huku, kitu kilichonishangaza ni kuona kuna baadhi ya watu walikuwa wanaonesha kufurahia kwa msiba huo kutokana na baadhi ya watu nilivyokuwa nikiwasikia wakizungumza.
Nanukuu mmoja nilimsikia akisema "" unaona sasa hata ukijifanya kukimbia ulikotoka mwisho wa siku utafukiwa tu hukuhuku, kiko wapi sasa si huyu karudi"" kwakweli nilistaajabu sana. Kuna mwingine pia alikuwa anasema "" wanaenda huko mwisho wa siku hamna lolote wakifa kazi kuchangiwa nauli si bora wabaki makwao tu""
Ama kweli ni maneno ambayo yalionesha waziwazi si mazuri hasa ukizingatia kwa mtu ambaye amekwishakata roho, ilipaswa aombewe anakokwenda apokelewe vizuri na muumba.
Sijajua tatizo ni nini kwa watu wa jamii ya huku ( bongo) ni kwamba hawawapendi diaspora au hawataki vijana watoke nje kuangalia fursa za maisha..ni nini kibaya kafanya yule kijana mpaka wamuongelee maneno ya namna ile.
Aliyewasahau nyie ni Zitto Kabwe, alikuwa anawavuruga akili tu huku akiwapa ahadi nyingi tu za kijinga.Diaspora nao wana nyondo sana na wanasahau sisi walio tuacha huku manyovu kigoma ndo wachimba makaburi wao
MTU, SABABU, MAJIRAInategemea na nini
Niliishi Mkoa wa Mbeya kama miaka mitano hivi, Wilaya ya Rungwe. Kwa kweli issue kama hii kule ni kama ugonjwa hivi. Wastaafu wanaoamua kurudi kwao wanasemwa sana mpaka wanazeeka kabla ya wakati wao. Inasikitisha kwa kweliSio kila diaspora ana good life unless labda awe ana professional career huko abroad. Otherwise unakuta tu mtu ameamua kubadili mazingira ya ku hustle huko anafanya kazi za kawaida zenye kipato chakuweza kujikimu yeye na familia yake kama waliopo hapa bongo tu.
Tatizo tumekariri kuwa ukisikia mtu anaishi mamtoni basi ni milionea fulani au ana good life sana labda anaringa na presumption nyingine kibao.
Kikubwa tuache wivu na kupenda kuchukia maendeleo ya wengine. Kisa mtu katoka kaishi nje ya nchi watu wanakuwa na wivu kiasi cha kufurahia kifo cha mwenzao?