Diamond umetuangusha wanaume hatufanyagi hivyo!

Diamond umetuangusha wanaume hatufanyagi hivyo!

Mwanaume anayeangushwa na Diamond anafaa kujipanga katika shindano la kutaka kuolewa na Diamond.

Diamond hajachaguliwa kwa kura za wanaume kuwa muwakilishi wa wanaume.

Atakuangushaje wewe mtu ambaye hakujui, humjui?
 
Malipo hua ni hapahapa Duniani. Ulimtenda vibaya Ivan akapata depression na kupelekea umauti wake. Leo yako wapi!
Unamwambia mtoa mada au zari .....kama zari mfate insta hapa sio mahala pake
 
Mna poteza muda wakati wenzenu clouds na management ya WCB wamesha ingiza hela ndefu YouTube na matangazo yaliyo tangazwa wakati hiko kipindi kipo hewani

Jiulizeni kwanini kipindi kilirushwa live kwenye media za clouds almost zote? Lkn pia refer kwa kauli ya Saidi Fela siku ambayo Diamond alikuwa clouds fm anaongelea swala la Ommy dimpoz na Q-boy.

Shame on them maana hawajali watu walioumia ili wao wapate hela. Victims hapo ni Zari na Hamisa.

Na kweli wameingiza hela
 
Both Zari na Hamisa ni waislam.
Na Nassib hajaoa.
Cha kufanya awaoe tu ili wazae watoto wa halali.
Maana wale watoto 3 alozaa na hao wanawake kisheria si wa Nassib ni wa hao wanawake.
Awaoe ili waanze kuwazaa watoto wa halali
 
Kuna jamaa yangu anakanuni yake, halazi mwanamke kwenye kitanda anacholala na mkewe (anafanya kazi nchi tofauti na mkewe) . Pili, anasisitiza hakuna kosa kubwa kama mwanaume kukubali kwa mkeo kwamba umemsaliti. Haitatoka kwenye kumbukumbu zake maisha yote.

Ikumbukwe kua Diamond hajafunga ndoa bado msimuonee
 
Both Zari na Hamisa ni waislam.
Na Nassib hajaoa.
Cha kufanya awaoe tu ili wazae watoto wa halali.
Maana wale watoto 3 alozaa na hao wanawake kisheria si wa Nassib ni wa hao wanawake.
Awaoe ili waanze kuwazaa watoto wa halali

Wasimsahau na Wema jamani amuoe na yeye
 
Najua Diamond ataonekana mjinga ila kwa watu waelewa wenye utashi wa kutambua mambo, kamwe unapothibitisha mtoto ni wako huna cha kuficha zaidi ya kupokea hayo majukumu, watu wengi wanasema Zari atamtimua Diamond lakini wanasahau Zari kaja bongo kamkuta Diamond anatafuta na alikuwa vizuri tu,


Diamond ana historia ya kukosa malezi ya baba yake kutokana na tofauti za wazazi wao na kila mtu anafaham na hakuna aliyefurahia hilo lakini hajapenda hilo litokee kwa mwanae.


Sasa Diamond ambacho hakupenda kufanyiwa na mzazi wake na mpaka leo hawaelewani hajapenda kimtokee mwanae na hii inathibitisha kuwa usichopenda kufanyiwa basi usimfanyie mwenzio.


Diamond ameteleza kuzaa na mwanamke mwingine zaidi ya Zari lakini hilo halimpi haki ya kukana mtoto asiye na hatia amabalo wengine walikuwa wanashabikia.


Kila la kheri Diamond, lea damu yako! Hujui kesho mwanao baada ya haya maisha yenu ya ustaa yanayopita atakuwa mtu gani katika Jamii!
Mondi mnafiki tu na kamchoka Zarina.
Huwez kaa kimya muda wote huo bila kumuweka mwenzako sawa na gafla unakimbilia media. Kama sio kumvua mwenzako nguo hadharani ni nini!?
Kaboa sana
 
Diamond kaamua kuwa accountable, japo hakutakiwa ku disclose kila jambo to that extent kwenye media lakini hii imedhihirisha kiasi gani amethamini mwanamke aliyekubali kubeba ujauzito wake mpaka kuzaa, wangapi wangeweza ku abort?

Mimi siyo fan wa Diamond but for this he has draw my attention! I support him
Kapuyanga mbayaaaa
 
View attachment 591899

Katika vitu ukisikia umepuyanga ni hili la leo kukubali hadharini kuwa ulimcheet Zari hata kama presure ya ku-konfesi imetoka kwa Zari ungekataa kabisa na kama ulishamwabia ndo ungekaa kimya haya ya mitandao yanaisha tu na baadae ungemwambia dada yako Esma amuite kimya kimya anakuja anakukuta bila ya yeye kutarajia hivyo hanakuwa hana mtu wambea mnakuwa watatu namnayazungumza hata bila ya picha mnamaliza kimya kimya, kuliko leo ulivyoenda kwenye Media ndo umetia boko maana kama umemvua nguo mkeo Zari kwa sidechick! Kisa mtoto umebugi.

Sasa unamkosa Zari hata kama utaendelea naye jiandae kisaikolojia utateseka tu, makosa umeyafanya lazima akulipizie maana sasa hakuamini labda nasema labda kama na wewe ulikuwa unalipiza kama unakitu alikufanyia hapo mmeenda sawa ila kama siyo umebugi.

Ni hayo tu.

Umebugi kawaida wanaume tukomaa tunakataa katakata hata kama umekutwa chumbani.
Hakuna mwanaume mwenye ubavu wa kuwa na mwanamke mmoja tu hapa duniani, jambo hili liliwashinda babu zetu, wanyama, ndege na hata wadudu. Kumbukeni kuwa katika uumbaji Mungu alikusudia wanawake wawe wengi kuliko wanaume, hivyo mwanaume amekusudiwa kuwa na wanawake wengi sawa ilivyo kwa jogoo, beberu, fahari (dume la mbegu), n.k. Mwanaume kuonekana ana mwanamke mmoja tu ni nidhamu ya woga na unafiki, kufanya hivyo ni sawa na kuamua kwenda against nature sawa na kuamua kuacha kwenda haja ndogo, kula chakula au kulala usingizi. Diamond ni nani hadi aweze kwenye against nature? Kama mitume (Mohamed, Seleimani, Ibrahim, n.k) wafalme, marais, mawaziri, na watu maarufu walishindwa kuwa na mke mmoja Zari ni nani hadi mshinde Queen of Sheba aliyekwenda kuolewa na nabii Suleiman mwenye wake wengi? Zari asepe tu kama akitaka lakini Diamond kumkubali mtoto wake hadharani ni sawa na sahihi kabisa, maana hakuna mtoto asiyekuwa na baba. Huyo mtoto ni damu ya Diamond ana haki ya kutambulishwa na kutambuliwa kama mtoto wa Diamond. Diamond alikwepa kufanya kosa la pili wakati wa kurekebisha kosa la kwanza alilofanya. Kumfisha huyo mtu kwa kumuogopa Zari atasema nini ingekuwa sawa na kutenda kosa la pili.

Asiyekuwa na babu, baba, mjomba, au kaka asiyekuwa na hawala nje ya ndoa anyooshe kidole tumuone, maana mimba ni matokeo ya kujamiani, hivyo kila anayefanya ngono ana uwezekano mkubwa wa kupata mimba. Diamond alikwepa kosa lingine la tatu la kutoa mimba, kwani angetaka angeweza kuitoa hiyo mimba kimyakimya.

Tusilikuze hili jambo ni kitu cha kawaida tu kwenye jamii na hata kwa Mungu. Kama wanaume wangekuwa wengi duniani basi huyo msichana asingezaa na Diamond, angeshaolewa na kuwa na mume wake ndani.

Hata wewe hapo ulipo saidiana na Diamond kuwahudumia wanawake ambao hawana wanaume, maana wanaume ni wachache sana kuliko wanaume, kila mtu na wake haijawahi kutosha na haitatosha.
 
Mondi mnafiki tu na kamchoka Zarina.
Huwez kaa kimya muda wote huo bila kumuweka mwenzako sawa na gafla unakimbilia media. Kama sio kumvua mwenzako nguo hadharani ni nini!?
Kaboa sana

Na kweli it seems keshamchoka anataka kubadilisha ladha,bt wanaume jamani hamkawiagi kutuchoka hata tuwafanyiaje
 
Back
Top Bottom