mpinga shetani
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 3,236
- 954
Uongozi wa mkoa wa Arusha umelazimika kumleta Bongo Fleva, Diamond ili asaidie kukusanya watu wakati Rais Kikwete atakapohutubia umma wa mji wa Arusha siku ya alhamisi mchana.
Kikwete atazindua rasmi jiji la Arusha siku hiyo.
Vyanzo vya ndani vimebainisha kuwa jitihada za viongozi kuhamasisha mahudhurio zimekuwa zikigonga mwamba katika ngazi za kata kwani watu wengi wamekuwa wakisema wazi kuwa hawatakwenda Stadium!
Diamond ambaye ni kipenzi cha wanawake wengi hususan mabinti wa shule atasaidiana na za komedi kujaza uwanja kabla ya hotuba.
Wakati huo huo wasanii wa Arusha wameandamana hadi ofisi za meya wa jiji kupinga kuenguliwa kwenye tamasha hilo huku uongozi ukiwakumbatia ma bongo fleva wa Dar.
Kikwete atazindua rasmi jiji la Arusha siku hiyo.
Vyanzo vya ndani vimebainisha kuwa jitihada za viongozi kuhamasisha mahudhurio zimekuwa zikigonga mwamba katika ngazi za kata kwani watu wengi wamekuwa wakisema wazi kuwa hawatakwenda Stadium!
Diamond ambaye ni kipenzi cha wanawake wengi hususan mabinti wa shule atasaidiana na za komedi kujaza uwanja kabla ya hotuba.
Wakati huo huo wasanii wa Arusha wameandamana hadi ofisi za meya wa jiji kupinga kuenguliwa kwenye tamasha hilo huku uongozi ukiwakumbatia ma bongo fleva wa Dar.