Diamond kaiba wimbo?

jobseeker

Member
Feb 25, 2012
70
7
Ndugu zangu kwa muda sasa toka niusikie ule wimbo wa diamond nimpende nani nimekuwa na
hakika kuwa ameiba mapingo ya nyimbo ile kutoka kwa mpiga tarumbeta yami sax. Naomba
muusikilize huu muziki hapa halafu muniunge mkono au kunikosoa. Inaniudhi sana kuwa waimbaji tele
nyumbani wanajiita wasanii kumbe usanii wote ni wa kuiba iba nyimbo za watu tu. Link ni hii hapa:
Yemi Sax - E No Easy (Original by P-Square) - YouTube
 
Inakuhusu nini hata akiiba kakuibia wewe? ebu wacha roho mbaya furahia mafanikio ya kinaja mwenzio na omba mungu na wewe akupe,usisahau kua alie pewa kapewa........
 
Inakuhusu nini hata akiiba kakuibia wewe? ebu wacha roho mbaya furahia mafanikio ya kinaja mwenzio na omba mungu na wewe akupe,usisahau kua alie pewa kapewa........
No, sikubaliani na wewe. Kama aliiba wimbo we should not support him.
Hatuwezi ku-encourage tabia kama hizo, huo ni ufisadi pia. Shame!
But kabla ya kum-condemn moja kwa moja, tu-investigate kwanza
Maybe aliununua kwa p-square au aliimba kiwa na authorization yao.
 
Inakuhusu nini hata akiiba kakuibia wewe? ebu wacha roho mbaya furahia mafanikio ya kinaja mwenzio na omba mungu na wewe akupe,usisahau kua alie pewa kapewa........

Kijana fumbuka macho! usiwe na mapenzi kiasi hata unashindwa kuona ukweli. Hawa hawa wasanii wamekuwa wakipita wakilia kuwa watu wanawaibia nyimbo zao, wanasikitika kuwa kuna watu wanafanya cd zao na kuuza. Ni hivi karibuni tu wamefika hata kuhusisha polisi kukamata watu wanao fanya copy za cd zao, sasa kwa nini wao wakasirike ilhali na wao wenyewe wanaiba?

Toa tongo za macho ndugu uone dunia!!!!
 
Ndugu zangu kwa muda sasa toka niusikie ule wimbo wa diamond nimpende nani nimekuwa na
hakika kuwa ameiba mapingo ya nyimbo ile kutoka kwa mpiga tarumbeta yami sax. Naomba
muusikilize huu muziki hapa halafu muniunge mkono au kunikosoa. Inaniudhi sana kuwa waimbaji tele
nyumbani wanajiita wasanii kumbe usanii wote ni wa kuiba iba nyimbo za watu tu. Link ni hii hapa:
Yemi Sax - E No Easy (Original by P-Square) - YouTube

Mimi ni mpenzi mkubwa wa Yemi na sio msikilizaji wa nyimbo za diamond na wenzake, hata hivyo baada ya sekunde chache tu za kusikiliza nyimbo hiyo ya diamond nilijua kabisa ni copy ya Yemi!!!!
 
Hamna uhusiano wa ki-beat wala ki-ala za muziki... Siyo kweli hata kidogo...!
 
Kwanini isiwe huyo mpiga Sax kamuibia diamond?

Naweza kuweka kulipa hadi senti yangu nyekundu ya mwisho kuwa Yemi hakukopi kutoka kwa Diamond.
Ushuhuda wa haraka ni lini yemi na diamomd walipotowa nyimbo zao. Waimbaji wa bongo wanalilia copyrights
lakini wakati huo huo wanashindwa kuheshimu sheria hizo hizo.
 
No, sikubaliani na wewe. Kama aliiba wimbo we should not support him.
Hatuwezi ku-encourage tabia kama hizo, huo ni ufisadi pia. Shame!
But kabla ya kum-condemn moja kwa moja, tu-investigate kwanza
Maybe aliununua kwa p-square au aliimba kiwa na authorization yao.

May be Diamond ndio kaibiwa pia hivyo investigation iangalie hilo pia maana wengi wanawaona wanamuziki wetu kama hawawezi toa kitu wengine waka copy
 
Inakuhusu nini hata akiiba kakuibia wewe? ebu wacha roho mbaya furahia mafanikio ya kinaja mwenzio na omba mungu na wewe akupe,usisahau kua alie pewa kapewa........

Kwa namna tanzania ilivyojaa watu wenye mentality kama yako, tanzania ni kweli tambarare!!!! Mentality za watu kama wewe ndio maana kila leo watu wanaiba serikalini na kujijengea majumba ya mafahari kila pembe ya tanzania, wanapeleka watoto wao kusoma ng'ambo, wanakula bata kila leo wakati watanzania walio wengi wanakufa na njaa, lakini watu kama wewe mnabaki ah haituhusu sisi kama wanaiba tuache roho mbaya!!!!!

Diamond ameiba beats za wimbo na ananufaika na hilo kwa nini wapenzi wa muziki wasiseme au kulijadili hilo? Niombe mola anipe? kila siku naomba mola anipe na nashukuru kwa alivyonipa, ikiwemo afya, akili, determination ya kujipatia riziki kihalali na kujua tafauti ya jema na baya. Vipi mwenzangu unaomba kwa mola nawe upewe?
 
jobseeker, sikia huu ushauri. Hakuna mwimbaji fleva yeyote ambaye ni mwanamuziki wa kweli, wote beats zao ni za kuiba. Maproducer wananunua ama kuiba beats kwenye internet then kina diamond wanatia sauti tu. No talent at all there.
 
Last edited by a moderator:
Kijana fumbuka macho! usiwe na mapenzi kiasi hata unashindwa kuona ukweli. Hawa hawa wasanii wamekuwa wakipita wakilia kuwa watu wanawaibia nyimbo zao, wanasikitika kuwa kuna watu wanafanya cd zao na kuuza. Ni hivi karibuni tu wamefika hata kuhusisha polisi kukamata watu wanao fanya copy za cd zao, sasa kwa nini wao wakasirike ilhali na wao wenyewe wanaiba?

Toa tongo za macho ndugu uone dunia!!!!



Umeongea ukweli ila tatizo la sie wabongo mtu ukisema ukweli unaonekana adui. Wengi wetu tuna tabia ya kuchukia ukweli. 99% ya beats za fleva ni za wizi.
 
Kwa namna tanzania ilivyojaa watu wenye mentality kama yako, tanzania ni kweli tambarare!!!! Mentality za watu kama wewe ndio maana kila leo watu wanaiba serikalini na kujijengea majumba ya mafahari kila pembe ya tanzania, wanapeleka watoto wao kusoma ng'ambo, wanakula bata kila leo wakati watanzania walio wengi wanakufa na njaa, lakini watu kama wewe mnabaki ah haituhusu sisi kama wanaiba tuache roho mbaya!!!!!

Diamond ameiba beats za wimbo na ananufaika na hilo kwa nini wapenzi wa muziki wasiseme au kulijadili hilo? Niombe mola anipe? kila siku naomba mola anipe na nashukuru kwa alivyonipa, ikiwemo afya, akili, determination ya kujipatia riziki kihalali na kujua tafauti ya jema na baya. Vipi mwenzangu unaomba kwa mola nawe upewe?
Roho mbaya haijengi wala haija husu wezi wa serekalini na waimbaji narudia tena ALIE PEWA KAPEWA......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom