Nafikiri nahitaji kuzungumza kiasi juu ya Dhana hizi mbili za Vua Gamba na Vaa Gwanda.... **Miezi kadhaa iliyopita CCM ilikuja na dhana ya VUA GAMBA falsafa hii ilipigwa vita na kupingwa na CHADEMA kwa hoja kuwa nainukuu.."HATA KAMA WATAJIVUA GAMBA BADO MWILI NI ULEULE NA SUMU NI ILEILE-Kama nyoka.."mwisho wa kunukuu LAKINI hivi sasa kuna dhana ya VAA GWANDA VUA GAMBA..nashindwa kuelewa Je!Mtu akivaa GWANDA mwili nao unabadilika??na Je!sumu nayo inapotea?? **Ninachoamini mimi kwa kutumia kauli na tafasiri ya CHADEMA juu ya dhana ya vua gamba ni wazi kuwa hata wale wanaovaa Gwanda bado wana miili ileile na sumu ileile...sasa basi Hatuoni kuwa Chadema inawapokea watu ambao iliwakataa mwanzo??hatuoni kuwa Chadema inapokea watu walewale...wenye miili ileile...na sumu ileile...ni ipi dhana halisi na udhati wa vaa Gwanda dhidi ya vua Gamba???....mmmh Politics!