Kweli hali ilivyo ni kuwa Wakristo wana nafasai ya kutoa wasomi wengi kuliko Waislamu, lakini kumbuka kuwa University ya kwanza kujengwa nchini ingekuwa ya Waislamu kama si EAMWS kuwekewa zengwe, ule mradi wa chuo kikuu Changombe ungefanyika kabla ya hizo Uni zote za wakristo unazozitaja na kuzijua wewe! ni nini kilichowafanya wapenda elimu Waislamu wawekewe zengwe kufungua Uni zao na shule zao huku Wakristo wakirahisishiwa?!Pili,ukisema "MFUMO KRISTO"Inamaana unongelea udini,kuhusu elimu,sisi waislam tuna vyuo vikuu vingapi hapa Tanzania?sekondary ngap?na za msingi ngap?mimi nakifaham chuo kimoja cha morogoro niambie vingine,wakristo wanavyo hiv:Tumain iringa,mwanza,Augustine mwanza,arusha,dar,ST.JOSEPH,Morogoro,n.k,na sekondary zao ni nying,hata sisi watoto wa wakiislam tunasoma ktk shule zao,huoni kwamba wanafursa kubwa ya kuwa na wasom wengi?
Ni Waislamu lakini ilikuwaje Makamba Snr Muislamu kwenda kushiriki kumwaga damu ya Waislamu wenzie Mwembechai kama si kutekeleza matakwa ya mfumo Kristo ambao mtumishi yoyote yule wa serikali kutoka dini yoyote ile hana budi kuufuata?Steang said:Katika uongozi,Rais wako dini gan?makam Rais pia?mawaziri wote hawa ni waislam utabisha nalo?mfano:
Adam malima naibu waziri kilimoDr.,Shukuru kawambwa,waziri elim,Dr.Aly mwinyi,wazir afya,Shamshi vuai nahodha,waziri wa ulinzi,hao ni baadh yao pamoja na manaibu wao,unajua wewe usichokoze watu kwa udini na kabila zao.
Silioni kuwa ni stupid question! kimtazamo wangu ni kuwa swali linalenga ku identify the problem halafu tuna offer solution, wakitaka kusikiliza na kufuata ushauri basi ni vizuri wasipotaka ndio hivyo tena, liwalo na liwe.Steang said:NB:The stupid qustion make sens than stupid words,
Samahan kama nitakua nimekukera ila liwe fundisho kwa wenye UBAGUZI, kama wewe,kazi njema.
Naam zengwe bado tunawekewa angalia sheria ya ugaidi na mfumo inavyozisitisha taasisi za kimataifa za kuwasaidia waislamu kushindwa kuwekeza katika miradi mikubwa kama ya Elimu, afya n.k.Miaka 50 baada ya uhuru bado mnawekewa zengwe?
hahaaaa na Syria,afaghainistani,libya.shida ya watu wengi hasa waislam ni walalamishi mno,please tufanye kazi tugu szanguni.huwezi kueneza dini kwa fitna na matusi,na ubaqguzi pia.Si waangalie nchi zinazoongozwa na mfumo Islam zilivo huku Afrika. Somalia, Zanzibar n.k.
Naam zengwe bado tunawekewa angalia sheria ya ugaidi na mfumo inavyozisitisha taasisi za kimataifa za kuwasaidia waislamu kushindwa kuwekeza katika miradi mikubwa kama ya Elimu, afya n.k hii inawafanya kilichobakia kwao ni kutoa misaada kama ya tende tu, misaada kama hii nikikumbuka mmoja wao akinielezea kuwa wanatoa hali wakisikitika kwa sababu kuna mengi wanayoweza kuwafanyia waislamu ila ndio wamebanwa.
Usisahau pia Waislamu baada ya kukandamizwa kwa muda mrefu wamepoteza hali ya kujiamini kama ilivyorekodiwa kuwa mkuu fulani wa taasisi ya umma ambaye ni Muislamu alishindwa kuidhinisha upanuzi wa Shule ya Sekondari ya Waislamu kwa kuogopa kuonekana kuwa anaipendelea dini yake!.....hii ndiyo hali waliyofikia Waislamu sasa!
Hili ni suala pana! kimtazamo wangu ni kuwa waliotayarisha huu ukusanyaji wa pesa kwa ajili ya kuanzisha TV wameangalia hali ya jamii yenyewe, zama na wakati ndio wakaona ni bora waanze na habari, baada ya waislamu kupata melezo ya kutosha kurudisha kujiamini kwao kinachofuata ni hayo uliyoyataja wewe tofauti na hali ya Waislamu wa Zanzibar, wakati, zama na hali zao haviakisi kuwakusanya na kuwachangisha kwa ajili ya chombo cha habari, unatizama lile linaloakisi na hapana shaka itakuwa ni muungano.Ndiyo maana nikauliza , kama mnaweza kukusanyana uwanja wa taifa na kuchangishana fedha kuanzisha TV Imaan, mnashindwa nini kukusanyana na kuchanga fedha za kujengea shule? Kwanini hamjiamini kuchangia kuanzisha shule lakini kwenye kuanzisha TV mnjiamini na mnashikamana pamoja na kuchangia??
Wakuu.
Acheni hizi mada za ukristo na uislamu.
Mnacheza mchezo wa CCM.
Mmeshasahau kauli za CUF, uislamu, CHADEMA, ukristo....Mnajiingiza katika siasa chafu za CCM.
Kwanza elekezeni nguvu zenu katika kupigania Tume huru ya Uchaguzi na katiba mpya....haya yanawaathiri wakristo,waislamu na wasio na dini...wenye vyama na wasio na vyama, walio wananchama na wasio wanachama wa vyama vya siasa.
Umaskini, uduni wa maisha,ujinga na maradhi ndio matatizo yetu makuu, tena hayachagui mwenye dini au ambaye hana dini. CCM au mpinzani,Mla halal au unayekula kitimoto.
Adui yenu ni yule "Mwenye Magamba"....dont loose sight! Dont be distracted!
Malumbano haya hayaleti tija....kuna member hapo ameyaita *****...kawaida ya ***** ukiutawanya na unayemrushia akikurushia mtaishia nyote kuwashwa.
Hizi dini mmezikuta na mtaondoka mtaziwacha!!!
Nadhani sasa hivi kuna Ukweli kuwa CUF ni chama cha Waislaam na Chadema ni chama cha Wakristu.. Yalisemwa na CCM kutugawa na imeshakuwa..Tumeshakubali matokeo hivyo kila mmoja wetu atafute pa kutokea au tuungane kupoteza mgawanyo huu..Well said. Tuna matatizo mengine ni social and economic inherent na mengine ni global oriented. Tunachoihiataji ni proper skills, knowledge, tools and empowerement to wrestle with such incumborances na sio religious differences. Uzuri ni kwamba wote tunaamini katika kuumbwa na Mungu Mmoja na tunapotofautiana ni kwenye doctrines. Wakristu wanaamini katika Utatu Mtakatifu na Waisalamu wanaamini katika Allah lakini mwisho wa siku we all claim originality from one Creator. Ugomvi wa nini.
Ebu jiulize kwanini nchi ambazo Waisalamu na Wakristu ni minority hawagombani hususani India na ambayo uchache wa Wisalamu ni kwamba wanalinganishwa na huge population ya Hindus. Lakini ugomvi uko kati ya Wahindu na Waisalamu na sio Wakristu na Waislamu. Nenda Palestina Waisalamu na Wakristu wanapendana sana na sijawahi kusikia Mwisalamu amelipua makazi ya Wakrstu au Mkristu amempiga Mwisalamu. Hawa wanashirikiana ili kuna wanaleta ukombozi wa kweli wa Palestina. Tunajifunza nini hapa. Ni kwamba tofauti zetu kiimani zinakuzwa na wanasiasa na watu wabinafsi ili waweze kufikia malengo yao lakni shida zetu za kijamii na kiuchumi haziwezi kutatuliwa kwa sababu ya ugomvi na kukashiiana
Wakuu.
Acheni hizi mada za ukristo na uislamu.
Mnacheza mchezo wa CCM.
Mmeshasahau kauli za CUF, uislamu, CHADEMA, ukristo....Mnajiingiza katika siasa chafu za CCM.
Kwanza elekezeni nguvu zenu katika kupigania Tume huru ya Uchaguzi na katiba mpya....haya yanawaathiri wakristo,waislamu na wasio na dini...wenye vyama na wasio na vyama, walio wananchama na wasio wanachama wa vyama vya siasa.
Umaskini, uduni wa maisha,ujinga na maradhi ndio matatizo yetu makuu, tena hayachagui mwenye dini au ambaye hana dini. CCM au mpinzani,Mla halal au unayekula kitimoto.
Adui yenu ni yule "Mwenye Magamba"....dont loose sight! Dont be distracted!
Malumbano haya hayaleti tija....kuna member hapo ameyaita *****...kawaida ya ***** ukiutawanya na unayemrushia akikurushia mtaishia nyote kuwashwa.
Hizi dini mmezikuta na mtaondoka mtaziwacha!!!
jukwaa la dini would have been appropriate.. hapa kwenye jukwaa la siasa naona unataka kuchafua hewa tu!!
Thursday, 27 May 2010 10:21 0diggsdigg
Mussa Mkama
MAASKOFU waliohudhuria mkutano wa siku moja wa Jukwaa la Wakristo, juzi walifanya kazi ya ziada kupata nakala ya waraka ulioandaliwa na mwenyekiti wa Chama cha Kidemokrasia (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ambaye alitumia mkutano huoo kuusambaza.
Mkutano huo ulikuwa wa kuzindua chombo hicho kikubwa cha mshikamano baina ya Wakristo, lakini Mchungaji Mtikila, ambaye anaongoza kanisa la Full Salvation, aliutumia kugawa takriban nakala 60.
Alikuwa akigawa waraka ambao ulisababisha polisi kuvamia nyumba yake iliyo Mikocheni na kufanya upekuzi kabla ya kuondoka na mwanasiasa huyo ambaye pia ni kiongozi wa kiroho na kwenda kumuhoji kituo cha polisi kwa saa kadhaa zaidi ya mwezi mmoja uliopita.
Waraka huo wenye kurasa 24 ambao Mwananchi ina nakala yake, unazungumzia harakati za kuwaamsha waumini wa dini ya Kikristo kuamka kutetea dini yao dhidi ya utawala wa sasa ambao mchungaji huyo anautuhumu kuwa unawabagua.
Waraka huo pia unawataja watu mbalimbali, kuanzia Rais Kikwete, viongozi wengine wa kisiasa na watu maarufu ukiwahusisha na tuhuma mbalimbali kubwa.
Maaskofu kadhaa walionekana kumfuata Mtikila ili kupata nakala ya waraka huo ambao mchungaji huyo alikuwa amebeba nakala zake kwenye mkoba wa mkononi.
Nilikuja na nakala chahe sana... 60 tu, zikaisha na wengine wakawa wanautaka tena," alisema Mtikila mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa kuzindua chombo hicho ambacho kazi yake kuu itakuwa ni kutetea haki za Wakristo.
"Nimegawa hapa kwa sababu viongozi wenyewe waliutaka ndiyo nikaona niwape; nisiwe mchoyo, alisema Mtikila.
Mtikila alisema kuwa kuzinduliwa kwa jukwaa hilo ni kuzaliwa kwa tatizo kubwa kwa Rais Jakaya Kikwete na kumtaka ajihadhari, akidai kuwa ajira yake sasa ipo kwenye "danger zone (sehemu ya hatari).
Mtikila, ambaye ana ujasiri wa kutoa kauli zisizo na simile, alisema jukwaa hilo ni gharika kubwa kwa Rais Kikwete kwa sababu alizodai kuwa kiongozi huyo wa nchi ni adui mkubwa wa Ukristo.
Wakristo nchini tupo milioni 27 hivyo ajira ya JK hivi sasa ipo shakani," alisema.
Viongozi wa makanisa ambayo yalishirika katika kuunda jukwaa hilo ni pamoja na Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (Tec), Jumuiya ya Makanisa ya Kikristo (CCT) na Umoja wa Makanisa ya Kipentekoste (PCT).
Ndugu mtanzania upo sahihi theoretically lakini practically hicho hapo juu nilichohighlight kwa red ndo kinachotendeka. tafakari, chukua hatua.