Demokrasia na Maendeleo ndani ya CHADEMA

Demokrasia na Maendeleo ndani ya CHADEMA

Haya mambo ya kukopi na kuweka hapa ni noma sana, utajua vipi kama CDM kuna demokrasia au la wakati, umeshindwa kutoka nje ya boksi la CCM??? wewe ni kama kifaranga akiwa ndani ya yai, anatamani kujua kama yeye ni kuku au kenge maana wote huwa ndani ya yai, ni mpaka watoke ndo hujitaambua.
mkuu soma upande wa pili wa shilingi usiwe unapende alwayz kusikia unachotaka kusikia utakuwa mlemavu wa ubongo
 
chadema ndio chama kubwa watu wanaendelea kujimbanza huku wengine wakijifanya wao ndio nguzo waende kwenye demokrasia
 
Nadhani mtoa mada angetueleza demokrasia ya kweli hapa tz inapatikana chama kipi, angekuwa ametufungua sana macho ili nasi tuweze kujifunza toka chama hicho. Lakini kwa sasa anabwabwaja tu ili kutimiza malengo yake binafsi.
 
mkuu soma upande wa pili wa shilingi usiwe unapende alwayz kusikia unachotaka kusikia utakuwa mlemavu wa ubongo

Asitoke hata kama unaandika pumba? Amekuwamsukule wa kula pumba zako? Jaribu kuandika kitu kinahovutia ingalau watu wa misimamo tofauti wanchangie kwa upeo not rubbish like this, unaonekana kama ni mzee wewe lakini mvi zinaongezeka na busara kutoweka!
 
Mkuu una taarifa za MZIGO wa Kinana kukamatwa pale Bandarini Dar, ni shehena ya pembe za ndovu. Hii ndio demokrasia ya kweli ndani ya CCM, katibu mkuu anaua Tembo lakini anaachwa anatamba tu
 
Hakuna demokrasia bila utawala wa sheria.
Hakuna demokrasia bila kuwajibika na kuwajibishwa.
Kinachotokea Chadema ni Sheria tu! Unawajibishwa kisheria na unapewa nafasi ya kujitetea! Anayehisi kaonewa basi ajitetee na demokrasia itafuatwa.
Kama huridhiki na jinsi mambo yanavyoenda ndani ya Chadema toa maoni positively kwenye vikao vya chama on how to improve na sio kufanya under ground movements na kutaka madaraka kwa pupa!

Ukiona haufurahishwi bado, basi uko huru kurudisha kadi na kujiunga na chama kingine na sidhani kama Chadema watakufuata na kukulazimisha! Na hiyo ndiyo demokrasia ya Kweli!
 
Kama unataka demokrasia ya kweli anzia CCM halafu uje utwambie ni lini nafasi ya mwenyekiti imewahi kugombewa na zaidi ya mwanachama mmoja. Ukimaliza huko ndo uje CDM.

Tiba
 
Hata upande wa pili wa wakoloni ulikuwa na faida, je ni nchi gani ungeishauri isidai uhuru kwa faida za ukoloni??? acha zako wewe.
 
Kuna watu wanaakili fupi kiasi kwamba nguo ya ndani ni ndefu, huwezi leo kung'ang'ania CCM bila kujua kama ingekuwa CHAMA kingine kingeifikisha wapi nchi. Lazima kubadili vyama hata kama tunavipenda vipi, zaidi ya hapo labda ni maslahi binafsi tu ndo yanawaweka CCM
 

Demokrasia kwake ni kuona press conferences za 'wanaCHADEMA' zinaandaliwa na kusimamiwa na CCM.

Au mikutano ya hadhara inayodaiwa kuwa ya kupigania demokrasia ndani ya CHADEMA kuandaliwa na CCM, ikiwemo kwa kuhonga vijana ili waje kwa wingi huku wahutubiaji wakijivika ngozi ya u-CHADEMA!

Au demokrasia kwake huyu mwandishi ni kutukana na kueneza propaganda za CCM dhidi ya CHADEMA za udini, ukabila na ukanda, hadharani na sirini.
 
Tz ilivyo nchi changa na maskini pia na demokrasia inakuwa changa pia. TANU ktk demokrasia zero hicho hakikuwa kikwazo cha TANU kuchukua dola kutoka kwa wakoloni. CDM ktk umri mdogo wa kuwepo kwake ty ipo vizuri kidemokrasia kuliko CCM. Kwa maneno CCM wanaonekana kuwa na mfumo unaoruhusu demokrasia lkn Ktk kutenda kwao demokrasia ni sifuri. Wenyeviti wa taifa ktk umri wao mkubwa bado wanateuliwa. Hakuwahi kuwepo ushindani. Ngazi nyingine zote zinapatikana kwa kunuliwa. Anayependwa anawekwa kando na wachache kwa kuwa hamna pesa ya kuhonga. Hata rais anapatikana hivyo. Sasa hivi wameisha anza kutoa rushwa makanisani, miskitini na bodaboda. Demokrasia ni mchakato. Unahitaji mengi ktk kuuimalisha pia ni ghali.
 
badala ya watu kujibu hoja wanakimbilia mleta uzi hii inaonyesha ni jinsi gani uwezo wa kupokea challenge ulivo mdogo kwa kupenda kusikia kila ukipendacho unaweza kuua minority wote ukipewa madaraka kwakuwa unamajority kwa thinking hizi
 
Humu kuna watu ambao mahaba yamekithiri...tutaona mwisho wake!!
 

Demokrasia kwake ni kuona press conferences za 'wanaCHADEMA' zinaandaliwa na kusimamiwa na CCM.

Au mikutano ya hadhara inayodaiwa kuwa ya kupigania demokrasia ndani ya CHADEMA kuandaliwa na CCM, ikiwemo kwa kuhonga vijana ili waje kwa wingi huku wahutubiaji wakijivika ngozi ya u-CHADEMA!

Au demokrasia kwake huyu mwandishi ni kutukana na kueneza propaganda za CCM dhidi ya CHADEMA za udini, ukabila na ukanda, hadharani na sirini.
hapo umejib hoja unaenda kulala eti kurugenzi ya habari!! hembu jibu hoja
 
Chadema. Chadema, ooh cdm,ooh Chadema,kama unaushahidi ni hamna demokrasia oh chama cha mtei hivi huwazii mengine muhimu katika nchi yetu umekalia kurorota tuu?
 
democracy is not about threatening and intimidating people is true u can sack people but u ucannot kill revolutionary ideas on them
 
Humu kuna watu ambao mahaba yamekithiri...tutaona mwisho wake!!

Kama una maanisha mahaba ya kukipenda chama fulani au itikadi fulani, basi ni sahihi kwamba hata wewe una mahaba ya dhati kabisa na itikadi na misimamo ndani ya huko uliko na usingependa ubadilishwe na yeyote, no matter what! U are right and I respect that and thats what we mean by true democracy!
 
Back
Top Bottom