- Kwa muda mrefu sana sasa nimeliona sana tatizo la kukosa ukomavu wa Demokrasia hasa kwenye kuvumuliana na mawazo tofauti kutoka Viongozi wa Chadema, mpaka kuepelekea hata wanachama na wapenzi wao kuiga tabia hiyo mbovu sana ya Viongozi wao hasa wa Taifa. Kuacha Mheshimiwa Zitto, viongozi wengi wa Chadema wana tabia mbaya sana ya kuonyesha hasira za binafsi pale unawapowakosoa au kuikosoa Chadema as I always do in the public!
- Ukikutana nao utawaona wanavyopata taabu ya kukusalimia, watajaribu kila njia kukukwepa na wakishindwa utaona wanajilazimisha sana kukusalimia, huwa inanishangaza sana kwani wengi wao nakumbuka sana jinsi zamani walivyokuwa wanamtukana matusi ya nguoni mzazi wangu na sijawahi hata siku moja kuwaonyesha kwamba nina tatizo nao, I mean badilikeni ndugu zangu siasa sio uadui kupingana mawazo ni kitu chema na chenye afya sana kwa maendeleo ya taifa letu. Tunapopingana kitikadi in the public halafu kuonekana pamoja pia in the public tunajenga imani kwa wananchi wetu kwamba kutofautiana kiitikadi ni kwa sababu wote tuna nia njema na Taifa lakini sio kwamba hatupendani au ni maadui, ila wote tuna uchungu na taifa letu na ni muhimu tukipingana maana ndio njia pekee inayokubalika Duniani kisiasa katika kutafuta njia iliyonyoooka kwa Taifa.
- Viongozi wa Chadema badilikeni au fanyeni semina za kuelemishana kuhusu hii tatizo kubwa sana ambalo linawasumbua na kuwatafuna sana, sio ustaarabu kwani huwa mnawatukana sana viongozi wengine lakini hatuwakimbii wala kuwaogopa kwa sababu tunajua kuna siasa na kuna sisi as binadam na wananchi wa Tanzania ambao tunahitaji kuwaongoza wananchi wengine, sasa tusiwafundishe kuwa kutofautiana kiitikasi ni uadui.
- MUNGU AIBARIKI TANZANIA!!
Le Mutuz