DCI Manumba akata kauli

DCI Manumba akata kauli

Amesha danja huyo, wanatupotezaea tu ili kutujenga kisaikolojia ktk kupokea taarifa ya kifo chake.
wanahofu nini? Hakuna mzalendo atakayepata presha kwa kifo cha mtu huyo,mwangosi anamsubiri kwa hamu kujua maendeleo ya uchunguzi wa kesi ya wauaji wake,R.I.H
 
Muulize Samuel Sita na Mwakyembe watakueleza, wakigoma kukujibu iulize Familia ya Mwangosi, ila ana mchango mzuri tu wa kuwakamata wanaotuhumiwa walimuuwa Kamanda Liberatus Barlow wa Mwanza.

Ile timu ya JK ya EPA hakuwepo? Ya Said Mwema,Hosea,na wa mwingine nani tenaa..??!
 
Mungu mjalie mja wako apate nafuu.Arudi kutumikia Taifa
 
Amesha danja huyo, wanatupotezaea tu ili kutujenga kisaikolojia ktk kupokea taarifa ya kifo chake.

watujenge kisaikolojia akiwa kama nani hasa? Kwa uzito upi alionao?

Watu wamefiwa na wake/waume, watoto na ndugu zao wa damu na hawakujengwa kisaikolojia iwe huyo mtu baki...
 
Very sory for that DCI, Hata hivo tunamwomba mungu akuponye ili 2015 haki itendeke mbele yako baada ya ukombozi wa Tz yetu kutokea!!
 
Sidhan kama kuweka chembe ya siasa kwenye habar kma hii ni sawa....ifikie pahala tuthamini uhai wa mtu, huna haja ya kutokumnunulia viatu mwanao eti kwa 7bu we baba ake hukuvaa wkati unasoma....MUNGU amuafu MANUMBA
 
Ikiwa mkapa aliamua siku ya mchonga kuaga dunia. Kikwete anasubiri nini?
 
Kazi ya Mungu haina makosa, Jina la Bwana lihimidiwe.
 
Amesha danja huyo,
wanatupotezaea tu ili kutujenga kisaikolojia ktk kupokea taarifa ya kifo
chake.

Wanasubiri JK amalize safari yake ya kuzurula kule Paris & Zurich ndo watangaze kifo cha huyu jamaa, wakitangaza mapema si itamlazimu mkulu kakatisha safari...
 
AFYA ya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi nchini (DCI), Robert Manumba inazidi kuwa mbaya baada ya kuwapo taarifa kwamba amekata kauli na mawasiliano kwa siku tatu mfululizo, huku akiendelea kupumua kwa msaada wa mashine.
Hali hiyo tete ya afya yake imesababisha kuwapo kwa usiri mkubwa kutoka kwa maofisa wa Jeshi la Polisi, madaktari wanaomtibu na ndugu zake.
Akizungumza na waandishi wa habari kwa kifupi sana, Daktari Mkuu wa Hospitali ya Aga Khan alikolazwa, Jaffer Dharsee alisema kuwa atakuwa tayari kueleza maendeleo ya matibabu ya Manumba Jumatatu ijayo.
“DCI Manumba bado yupo katika chumba maalumu akiendelea na matibabu chini ya uangalizi maalum wa madaktari na wauguzi,” alisema Dk. Dharsee.
Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika viwanja vya hospitali hiyo jijini Dar es Salaam, umebaini kuwa hali ya DCI huyo inakatisha tamaa.
Hali hiyo ndiyo imeifanya serikali kushindwa kumsafirisha nje ya nchi kwa matibabu zaidi.
Hakuna mtu anayeruhusiwa kuingia kumwona isipokuwa kwa baadhi ya viongozi na ndugu wachache muhimu.
Manumba aliugua ghafla na kulazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, akipatiwa matibabu kwa kile kilichoelezwa kuwa na wadudu wengi wa ugonjwa wa malaria.
Hata hivyo, Januari 14, alihamishiwa katika Hospitali ya Aga Khan kwa matibabu zaidi na kuwekwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi.
Manumba aliteuliwa na Rais Kikwete kushika wadhifa huo mwaka 2006, akichukua nafasi ya Adadi Rajabu.

Mtanzania

Hivi kumbe alianzia Muhimbili ndo akapewa rufaa kwenda Aga Khan?!! Kati ya hizi mbili sijui ipi ya rufaa zaidi, tena kwa malaria (naamini serikali bado inawaamini madaktari wetu, hata baada ya ule mgomo).
Ila nakumbuka Zitto alianzia Aga Khan, akafu akapewa transfer kwenda Muhimbili
:confused2::confused2::confused2:
 
Mungu fanya muujiza manumba apone

Hivi ni malaria tu au kuna lingine??? Kama ni malaria basi ni kiboko... au wenzake hawakumpa technics za kubadili blad???
 
Back
Top Bottom