Wakuu zangu, kama habari hiyo ni ya kweli...Hapana, sipendi kuamini kuwa tumefika huko...,
Mkuu
Kalamu1, habari hii ni ya kweli...Hapana, sipendi kuamini kwamba hatujafika huko...
lakini kama ni kweli na kuna watu wanashangilia ...!
Ni kweli na kuna watu wanashangilia...!
Kila nikiijaribu kuliwaza tendo kama hilo, katika nchi yetu hii nzuri...! Hivi kweli inawezekana?
Naam, usiwaze sana tendo kama hilo, katika nchi yetu hii ya leo...inawezekana sana tu.
Hivi kweli ndio tumefika huko?...
Si tu tumefika huko, tumevuka huko na tunazidi kusonga mbele.
Mkuu
Kalamu1, kuna Mbunge, mwakilishi aliyepigiwa kura na wananchi, aliwahi kumiminiwa risasi risasi zaidi ya 30 na kati ya hizo 16 zikatua mwilini. Kitendo hicho kilifanyika mchana kweupe akitoka bungeni an akiwa anarejea nyumbani kwake sehemu yenye ulinzi na ambapo wanakaa watumishi wakuu wa serikali. Wakati Wasamaria wema wakimsaidia asikate roho, si Bunge wala Serikali ilikuwa tayari kugharamia matibabu yake lakini kwa neema ya Mwenyezi Mungu, aliweza kunusurika na kifo na hadi leo hii yuko mzima akiendelea na matibabu kwa msaada wa ndugu, marafiki na Wasamaria wema.
Naam, katika hii nchi yetu unayoiita nzuri, tendo la ukatili kama huo liliwezekana na washangiliaji walikuwepo na wanaendelea kuwepo. Nashangaa tu kwamba umeshtushwa na kushushwa kwa bendera, sijui ulizungumziaje hili! Sijui unaongeleaje kupotea kwa wananchi na miili yao kuokotwa kando ya bahari. Sijui unaongeleaje kuhusu kutekwa, kuteswa na wakati mwingine kuuliwa kwa Watanzania kwa sababu tu ya kuwa na msimamo tofauti kiitikadi. Najua wapo wanaoshangilia! Naam, tumefikia huko...na bado! Yapo makubwa zaidi yanatusubiri huko mbele ya safari...kumbuka aliyeonja nyama ya binadamu haachi!