DC Muro Matatani kwa kushusha Bendera za CHADEMA Arumeru

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
749
1,797
Mkuu wa wilaya ya Arumeru ,Jerry Muro huenda akaingia kwenye msuguano mkali na chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema wilayani humo kwa hatua yake ya kushusha bendera zake pindi anapokuta zikipepea kwenye maeneo ya biashara zilizosimikwa na wapenzi wa chama hicho.

Mapema leo Muro wakati alitoka kuangalia majeruhi wa ajali katika hospital ya Selian ,Ngaramtoni,alifika katika Duka moja la mfanyabiashara wa Makochi na alipoiona Bendera ya Chadema ikipepea aliamuru Dereva wake asimame na kuifuata bendera hiyo.

Alipofika Muro alimwamuru mfanyabiashara huyo wa Makochi ambaye hakufahamika jina lake Mara moja, aamue moja kufanya biashara ama kuendeleza siasa ,Hata hivyo kabla ya kijana huyo kujibu alimtaka ashushe bendelea hiyo Mara moja.

"Arumeru hii si ile ya zamani msinijaribu lazima tuheshimiane chagua moja kazi ama siasa" Alisema Muro

Jambo hilo liliwashangaza wananchi mbalimbali waliokuwepo eneo hilo huku ikielezwa kuwa linaweza kuleta mtafaruku wa kisiasa kwa hatua yake ya kushusha bendera za Chadema huku za CCM zilizopo vijiweni kwenye biashara akiziacha ziendelee kupepea.
 
Kiburi chote hicho anakipata kwa Bosi wake Jiwe

Kwa vile ndiye bingwa wa kusigina Katiba ya nchi

Kwa kuwa inajulikana wazi kuwa nchi hii ipo kwenye mfumo wa vyama Vingi, kwa maana hiyo kitendo cha kushusha bendera ya chama chochote cha siasa, ni tendo ambalo ni kosa la jinai.......

Kwa kuwa kama kweli huyo Bosi wake angekuwa hajazipa "blessings" huo upuuzi, ungesikia kuwa keshamtumbua!
 
Kama ni kweli huu ni ulevi wa madaraka. Na nimemsikia Jerry Muro akisema kwenye luninga eti Arumeru wao wanampango maalum kwa makosa fulani, mkosaji hapewi dhamana. Nikajiuliza sana hivi yeye ndio mahakama!

Hiyo amecopy toka kwa jiwe, si unakumbuka wapinzani kunyimwa dhamana kwenye suala linaloruhusu dhamana? Ukimuuliza walikubaliana na nani utakuta ni yeye na wenzake walioko juu ya sheria.
 
Mkuu wa wilaya ya Arumeru ,Jerry Muro huenda akaingia kwenye msuguano mkali na chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema wilayani humo kwa hatua yake ya kushusha bendera zake pindi anapokuta zikipepea kwenye maeneo ya biashara zilizosimikwa na wapenzi wa chama hicho.

Mapema leo Muro wakati alitoka kuangalia majeruhi wa ajali katika hospital ya Selian ,Ngaramtoni,alifika katika Duka moja la mfanyabiashara wa Makochi na alipoiona Bendera ya Chadema ikipepea aliamuru Dereva wake asimame na kuifuata bendera hiyo.

Alipofika Muro alimwamuru mfanyabiashara huyo wa Makochi ambaye hakufahamika jina lake Mara moja, aamue moja kufanya biashara ama kuendeleza siasa ,Hata hivyo kabla ya kijana huyo kujibu alimtaka ashushe bendelea hiyo Mara moja.

"Arumeru hii si ile ya zamani msinijaribu lazima tuheshimiane chagua moja kazi ama siasa" Alisema Muro

Jambo hilo liliwashangaza wananchi mbalimbali waliokuwepo eneo hilo huku ikielezwa kuwa linaweza kuleta mtafaruku wa kisiasa kwa hatua yake ya kushusha bendera za Chadema huku za Ccm zilizopo vijiweni kwenye biashara akiziacha ziendelee kupepea.
Viongozi wa awamu ya 5 pasua kichwa !! Bendera zinamzuiaje kufanya kazi zake za ukuu wa wilaya ?!. Mungu aisamehe nchi hii, imetunukiwa viongozi wa hovyo kabisa kuwahi kutokea Africa . Ni kinyaa hasa
 
Piga kazi Murro , hao wanafiki na watetezi wa Mafisadi chadema hatuwahitaji tena huku Arumeru.
 
Je mfanya biashara huyo ana leseni ya biashara anayo ifanya? au kuwa na kitambulisho cha ujasiriamali?kama hivyo na sifa nyingine za kufanya biashara hizo anazo basi Mh Dc atakuwa kakosea sana
 
Hiyo amecopy toka kwa jiwe, si unakumbuka wapinzani kunyimwa dhamana kwenye suala linaloruhusu dhamana? Ukimuuliza walikubaliana na nani utakuta ni yeye na wenzake walioko juu ya sheria.
Hawa jamaa hawajui hata katiba ya nchi inafananaje, wanajua jinsi wanavyofikiri ndani ya vichwa vyao,basi hiyo ndiyo sheria.
Huyu anatuhumiwa kuonekana Dodoma siku ile Lissu anashambuliwa,sijui alifuata nini huko Dom?
 
Kwa sisi tunaojua siasa kumsimamisha Jerry Muro kwenye Jimbo la Mbowe ni kumtengenezea Mbowe njia ya kushinda kirahisi. Muro bado hajakomaa na ni mgeni kwenye siasa, kumshindanisha na Mbowe ni kumsafishia Mbowe njia.
Tulishauri hivyo hivyo jimbo la Kibamba, kumsimamisha Mama Fenera Mkangara na John Mnyika ni kumtengenezea njia Mnyika sana ccm wenzangu hawakuelewa,matokeo yake Mama was watu amepotea kwenye siasa. Yapo majimbo ambayo wabunge wake kuwatoa inabidi tu litumike jeshi LA polisi, lakini kwa uchaguzi wa mwakani so rahisi kama watu wanavyofikiria , wizi inategemea na mazingira.
 
Back
Top Bottom