DC Mrisho Gambo wa Arusha amhujumu mkuu wa mkoa

DC Mrisho Gambo wa Arusha amhujumu mkuu wa mkoa

Hivi kumbe chato ni eneo la adhabu kwa watumishi?
hii kasumba sijui itaisha lini, ni ukweli usippingika kuwa kuna maeneo Tanzania hii ni maeneo ya Adhabu kwa watumishi hasa mikoani kusiko na Majiji! imbalance level of development ndo adhabu yenyewe hiyo unatolewa Lamini unapelekwa vumbini utasaga kiatu kwenye vumbi raha yake utakivaa miaka na miaka usigundue kuwa kimepitwa na fashion kama si kuchanika
 
Dc wa Arusha hajui mipaka ya kazi yake.Hii ndio maana CHADEMA tulisema tungeondoa nafasi ya DC kwenye mfumo wa utawala,maana hiki ji cheo cha enzi za mkoloni ambacho hakina tija kwa wakati huu wa sasa.
Mtu hupanda cheo kwa kuwa muadilifu,mwaminifu,heshima,na kuwa humble sio vinginevyo
 
Huyu Dc kazuia posho ya madiwan wa Chadema kwasasa wanashinda mitandaoni kumtusi tuu hawana kazi nyingine kwasasa
 
Huyu Dc kazuia posho ya madiwan wa Chadema kwasasa wanashinda mitandaoni kumtusi tuu hawana kazi nyingine kwasasa
Dada pesa sio yake...na kuzuia hawez,...na Arusha sio yake ni yetu....hakuchaguliwa na wananchi ameteuliwa.........na akae akijua hapa Arusha,sio kule korogwe alipokuwa anawasweka ndan ,walimu kisa hawajachangia fedha za maabara.......ataelewa tu ..........
 
Huyu Dc kazuia posho ya madiwan wa Chadema kwasasa wanashinda mitandaoni kumtusi tuu hawana kazi nyingine kwasasa
Ficha ujuha wako...DC hana mamlaka ya kuzuia posho za Halmashauri,mamlaka yake katika Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa hazina meno.Muwe mnasoma hata kanuni,sheria na taratibu kabla hamjadanganya.
DC hana ubavu huo,zaidi atatumia hoja hiyo kujiongezea umaarufu,ndio maana siku ile Waziri Jaffo alisema...kila mtu afanye kazi kwa mipaka yake,maana Jaffo anajuwa kuwa DC si lolote katika kusimamia na kutoa amri kwenye baraza la Madiwani.Tatizo ni kuwa hivi vyeo vya u-DC havina kazi tena,sasa ili mtu aonekane anafanya kazi anaamua kuingilia majukumu ambayo ni nje ya mipaka yake ya kazi.

Umewahi kusikia mkuu wa Mkoa wa Dodoma anazuia posho za Wabunge?Eti kisa yeye ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma??Hata kijiwe cha Wazee wa Kirangi pale cha kahawa wameanza kumshitukia...alikuwa anaenda kupandikiza ukabila na chuki,anawananga wazee kuwa wamehama Kondoa kuja Arusha mpaka sasa hawana nyumba.R-Chuga ni kitu ingine....
 
Katika hali ambayo haikutarajiwa mkuu wa wilaya ya Arusha Mrisho Gambo ameanza kumhujumu mkuu wa mkoa Bwana Ntibenda. Hali hiyo imetokea leo eneo la nane nane Arusha,leo ndio siku ya uzinduzi rasmi wa siku ya nane nane ambako ilitegemewa watumishi wa halimashauri kuhudhuria sherehe hizo ambazo mgeni Rasmi ni Mkuu wa mkoa

Katika banda la halimashauri ya jiji la Arusha hakukuwa na mtendaji hata mmoja baada ya kuitwa kwenye kikao kingine na mkuu w wilaya ya Arusha bwana Gambo katika ukumbi wa chuo cha ufundi Arusha. Haikuweza kufahamika mara moja sababu ya mkuu wa wilaya kumtoroka bosi wake na kuitisha kikao kisicho na tija wakati akijua kuwa sherehe za nane nane ni za muhimu zaidi.

Baadhi ya watumishi walioenda kwenye kikao cha DC wamekerwa na tabia ya DC kujisifu kuwa yeye ndie mteule sahihi wa Rais na kuwa siku si nyingi atapandishwa cheo kuwa RC hivyo watumishi wote wamsikilize yeye vinginevyo atawahamishia Tandahimba au Chato.

Kitendo cha leo ni mwendelezo wa mgogoro wa chini kwa chini unaondelea kati ya mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa unaosababishwa na tabia ya DC kumuhujumu waziwazi RC na wakati mwingine kuongea maneno ya kashfa dhidi ya RC

Mkuu ukijikita kuandika hadithi fupi fupi utauza sana....
 
Sasa hapo ndio umeandika ujinga gani jebu hoja kwanini anaujumu


Arusha is too big for this guy na wananchi wa Arusha hawaitaki ccm kwa hiyo ajitajidi kushirikiana na mbunge na madiwani kwani ndiyo wenyeji wake. Kwa sasa Arusha iko poa na mafisadi waliojimilikisha halmashauri ya Jiji wametoweka.
 
Arusha atashikishwa adabu,ngoja ajichanganye huyo DC.mkuu wa mkoa yupo vizuri kajipanga na anaonekana kuiwezea Arusha
 
Huyu Dc kazuia posho ya madiwan wa Chadema kwasasa wanashinda mitandaoni kumtusi tuu hawana kazi nyingine kwasasa
Uvccm imekushinda umehamishia mjadala kwenye kuwapigia debe mafisadi waliolihujumu jiji la Arusha
 
Katika hali ambayo haikutarajiwa mkuu wa wilaya ya Arusha Mrisho Gambo ameanza kumhujumu mkuu wa mkoa Bwana Ntibenda. Hali hiyo imetokea leo eneo la nane nane Arusha,leo ndio siku ya uzinduzi rasmi wa siku ya nane nane ambako ilitegemewa watumishi wa halimashauri kuhudhuria sherehe hizo ambazo mgeni Rasmi ni Mkuu wa mkoa

Katika banda la halimashauri ya jiji la Arusha hakukuwa na mtendaji hata mmoja baada ya kuitwa kwenye kikao kingine na mkuu w wilaya ya Arusha bwana Gambo katika ukumbi wa chuo cha ufundi Arusha. Haikuweza kufahamika mara moja sababu ya mkuu wa wilaya kumtoroka bosi wake na kuitisha kikao kisicho na tija wakati akijua kuwa sherehe za nane nane ni za muhimu zaidi.

Baadhi ya watumishi walioenda kwenye kikao cha DC wamekerwa na tabia ya DC kujisifu kuwa yeye ndie mteule sahihi wa Rais na kuwa siku si nyingi atapandishwa cheo kuwa RC hivyo watumishi wote wamsikilize yeye vinginevyo atawahamishia Tandahimba au Chato.

Kitendo cha leo ni mwendelezo wa mgogoro wa chini kwa chini unaondelea kati ya mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa unaosababishwa na tabia ya DC kumuhujumu waziwazi RC na wakati mwingine kuongea maneno ya kashfa dhidi ya RC



Mmmmmmmmmmhhhh....sijui bwana, isije kuwa habari hii imelenga kumhujumu huyo DC....hivi kweli DC anaweza kusema hivi karibuni nitateuliwa kuwa RC???!!!
 
DC hana uwezo wa kubania posho za vikao...acheni mentality za kifukara,hivi posho ya laki na nusu kwa vikao vya mara kadhaa kwa miezi kadhaa nayo ni ajabu?
Ndio anawadanganya kuwa kaja kupambana na Chadema Arusha?Anawekwa katikati huyo,hachukui muda...Alizoea kuwatisha Uvinza,kwamba wengi wa wakazi kule "wakimbizi",ukimkosoa kidogo anakuita ofisini akiwa na Afisa Uhamiaji anaanza kuhoji Uraia

Huyu dogo na kijiwe chake pale cha kahawa kwa wale wazee wa kirangi wanamvutia kasi,anafika pale anaanza kupandikiza chuki na uhasama...Nyendo zake za kujenga chuki kwa jamii ya Arusha kwa manufaa ya kisiasa tunazifuatilia.Arusha damu ilishamwagika sana sbb ya watu wa aina ya Mrisho Gambo...Tunaomba aache mji utulie,tumezika sana wahanga wa siasa za chuki hapa Arusha inatosha...
Tena mkuu pale kwa wale wazee wa kirangi wengi wameshamchukia ila yeye hajui tu, wanamshangaa kwa nini anadharau namna hii? Eti anawauliza wazee kwa nini hamrudi kijijini kama hapa mjini hamna hata nyumba za maana au hamjajenga kabisa? Kweli mtu hajakuomba masaada unamuuliza kwa nini usirudi mjini? Kama kila mzee arudi kijijini kwake kwa nini asianze na viongozi wake wa chama wastaafu walioko Dar awaambie waende wengine mtwara huko wengine unguja? Dogo akijiharibia mapema sana mbele ya wale wazee maskini.
 
Dc Gambo piga kazi brother..asikuyumbishe yeyote wala haya maneno ya ealioshindwa kazi na vibaraka wao..hakuna swali hapa ukweli ni kwamba ume outshine kwa mda mfupi sana...na wanaotengeneza fitina hizi za akili fupi mda wao unahesabika...

Unaheshimika na vry soon wanaokuunga mkono utawaona hadharani wakikutetea...
Wewe hujui usemalo. Wanaompinga ni mbunge na madiwani wake. Unaposema wataondoka waende wapi wakati ndiyo wenye Jiji?
 
Back
Top Bottom