Mtini
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 1,487
- 2,344
Taarifa ya kwamba Mkuu wa wilaya Ikungi aliyeteuliwa jana Bw.Fikiri Avias, uteuzi wake umetenguliwa leo, (ndani ya saa 24) kabla hata hajaapishwa imeniacha na maswali mengi sana. Pamoja na kwamba tunaheshimu mamlaka ya uteuzi lakini nadhani ipo shida mahali fulani. Kama ndugu Fikiri hakupaswa kuwa kwenye nafasi hiyo ilikuaje haikujulikana mapema hadi akatangazwa? Nadhani hii si habari njema sana kwa mamlaka husika. Rais wetu mwema Magufuli anapaswa kuchukua hatua zaidi ili kujiridhisha na wateule wake kabla haja"publisize". Anyway namtakia majukumu mema DC mpya wa Ikungi Bw.Miraji Mtaturu ambae alikuwa Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza.!
Malisa G.J
Malisa G.J