Huihui2
JF-Expert Member
- Jan 5, 2012
- 9,576
- 14,312
Siyo tu Nikki wa pili alimsomesha huyu binti, Bali huyu binti aliibuka mwanafunzi Bora wa uhasibu ngazi ya degree na Kwa Sasa ni CPA (certified Public Accountant) .
Huyu si mwingine ni Nickson Simon Mkuu wa wilaya wa kibaha, alimpenda Sana huyu binti mpaka akafikia hatua ya kuingilia majukumu ya wazazi akaamua kumsomesha yeye mwenyewe Kwa pesa anazo zipata kupitia mziki.
Lakini unaambiwa wamekuja kuachana baada ya Nikki wa pili kuwa mkuu wa wilaya, pata picha unakuja kuachwa kipindi ambacho kwenye maisha ndo umepanda zaidi juu.
Walizaa mtoto mmoja wakamwita jina la ZURI, Nikki wa pili alimwimbia hadi wimbo mke wake akaupa jina la zuri ambalo ndo likaja kuwa jina la mtoto wao.