DC Bukoba aamuru walimu wachapwe mboko!

Sikonge, nimeshawahi kusema kuwa sioni mantiki ya kuwa na Wakuu wa Mikoa (RCs) na Wakuu wa Wilaya (DCs), hivyo vilikuwa vyeo vya kikoloni na vilitumiwa na wakoloni na si ajabu huyo DC kuamuru Waalimu wachapwe viboko! Vyeo vya RCs na DCs huwa ni vyeo vya kuwasaidia 'wenzetu' ambao hawana pa kwenda na ndo maana utakuta sehemu kubwa ya RCs na DCs ni Wabunge waliopoteza Ubunge, walioondolewa kazini bila sababu za msingi na ili kuficha ukweli au kuepusha kesi anateuliwa kuwa RC au DC (Mfano Col. Simbakalia-RC wa Kigoma alikuwa DG wa NDC, akaondolewa baada ya kukataa matakwa ya Wakubwa kuhusu Mgodi wa Mchuchuma au Liganga).

Kuna DC wa Wilaya ya Hai- Husna Mwilima, huyu alikuwa Katibu wa Tawi moja la CCM Arusha Mjini, baada ya Muungwana na kundi lake kushika hatamu sasa ni Dc wa Hai tena ni bomu kweli! Mkuu wa Wilaya ya Tabora-Moshi Chang'a ulizia elimu yake, utachoka. Lakini alikuwa ni Mkereketwa huko Iringa na Mshereshaji kwenye matukio ya CCM! wako wengi na ni vituko vitupu na wote wamekabidhiwa Mashangingi!

Ingekuwa vema vyeo vya RC na DC vikafutwa wakabaki Maafisa Tawala (RAS na DAS) ambao ndio professionals na si hawa wanasihasa.

Na kweli kazi ya hawa jamaa sasa hivi ni ubangaizaji tu. Wanakimibizana na Wakurugenzi na Mameya kwa kuonyeshana ubabe. Wengine mhhh, mambo yao yanatisha. Ila namuhusudu mrembo wangu mmoja hapo Korogwe (Betty), yeye mambo yakiwa magumu analia tu na kuomba wananchi wamuonee huruma kwa kutekeleza anachokitaka:)
 
Walimu Kuchapwa Viboko Yawezekana Mkuu wa Wilaya alikuwa Sahihi!



Kwa vyovyote mtu mpaka akafika kuteuliwa kuwa mkuu wa wilaya mambo mengi kuhusu utendaji wake wa kazi yanakuwa yamepitiwa ikiwa ni pamoja na uadilifu katika utendaji wake wa kazi. Mimi ningependelea kwanza kujua kwa nini mkuu wa wilaya husika huko Bukoba alifikia hatua ya kuamua hivyo? Halafu walimu walio charazwa viboko watueleze kama kuna mmoja wao atarudia kosa lililopelekea wao kucharazwa aidha kama maishani mwao watasahau tukio hilo!



Kwangu mimi naona hatua kama hizi zinatakiwa kuchukuliwa na si kwa walimu tu bali hata katika sekta nyingine za serikali ambapo watu wamejisahau kabisa kwamba utendaji wao wa kazi ni dhamana kubwa kwa wananchi wote wa Tanzania na wanalipwa mshahara kutokana na jasho la walipa kodi. Hivi ukichukua daftari la mahudhurio ya walimu vs daftari la mahudhirio ya wanafunzi ukakuta wanafunzi ndio wanaudhuria darasa kuliko walimu hii inakupa picha gani? Lazima kuwepo na sababu za kutosha za walimu kukosa kufundisha kama vile wanapofuatilia mishahara yao kule NMB (Benki ya Makabwela), lakini kama mambo hayo yote yamekwisha fanyika nab ado mwalimu haudhurii madarasa yake nap engine amekwisha onywa mara kadhaa hataki kusikia inabidi siasa tuziweke pembeni na njia yoyote ya kuwaadabisha kama vile tukio laviboko itafutwe.



Kumbuka wakati utaratibu wa kuondoa kiti kwa wafanyakazi wa serikali ulipoanzishwa wote walijikuta wakiwahi kazini na aliyekuta kiti kimetolewa siku hiyo atakuwa alishinda vibaya sana kazini mpaka hata siku inayofuata akajitahidi kuwahi, hii japo haikuwa viboko sijui kama ingepelekea waziri aliyehusika na amri hiyo kwenda kupimwa akili.



Inaonekana kwamba matokeo mabaya ya wanafunzi aidha wawe wa shule za msingi au zile za sekondari yanatokana na siasa ambazo kwa sasa tunatakiwa kuziacha na kuingia katika kazi kikwelikweli. Naomba kuanisha mambo ambayo nafikiri yatatoa changamoto na kupelekea fani ya ualimu kuwa miongoni mwa sekta muhimu na zenye mvuto wa kufanya watu wapende kufanya kazi mle.



Kwnza kabisa wachaguliwe watu wenyekujisikia kuwa ualimu ni wito wao.
Wawe ni watu ambao wamefaulu vizuri tofauti na sasa ambapo wale waliofanya vibaya ndo wanachukuliwa kuwa walimu, mfano waliofanya vibaya Form VI ndo wanachukuliwa kwenda kujiandaa kuwa walimu,tena wa shule za sekondari kama sikosei, yaani wanarudishwa kufundisha wenzao vitu ambavyo wao walishindwa kuvifaulu!!!
Mazingira yao yaboreshwe, ikiwa ni pamoja na mishahara mizuri na ambayo kulipwa kwake hakusumbui.
Kuwepo na motisha kwa walimu ambao wanafunzi wanafaulu vizuri katika masomo wanayofundisha.


Kwa machache hayo na mengine mengi yanayoweza kuboresha fani ya ualimu yatafanya walimu wawe katika mazingira bora ya kufundishia na kurdisha heshima ya fani ya ualimu, hii itaondoa hali inayopelekea walimu kukosa uelekeo na matokeo yake wanafunzi wanafanya vibaya mashuleni kwao ambacho ndicho pengine chanzo cha hasira ya mkuu wa wilaya kuwacharaza viboko
 
Huyu jamaa amewadhalilisha walimu, naungana na Mama Mahiza, apimwe afya ya Akili, inawezekana si mzima duh!
 
Sawa sawa MK, ili kila mmoja ahukumiwe kufuatana na cheo, nafasi yake pamoja na matendo yake!

Kama kuna jina ambalo ungestahili kwa kigeugeu hiki cha hoja basi ni MALAYA ni kipi haswa unachosimamia ndugu yetu? mara kuchapwa sio sawa mara iwe sawa? au analysis yako isiyo poor haina principles inazo zisimamia? im out here, my grade three daughter will respond to your next st*p*d post.
 
Ni kweli kuna-duplication ya uongozi mkoani na wilayani, tazama kuna RC na RAS; DC na DAS. Hivi nani wako chini ya RC au DC? kwani watumishi wote wapo chini ya RAS na DAS. Nami nilishawahi kuandika hapa JF kwamba hatuna haja ya kuwa na hawa awili ofisi moja.

Nchi yetu ni masikini, tunapaswa kuwa na bajeti ndogo kwenye mambo ya utawala ili tutekeleze miradi ya maendeleo. RAS na DAS wanaweza kutimiza majukumu yote bila kuwepo RC au DC. Hata jirani zetu Kenya Secretary ndiye bossi wa Mkoa (RAS) au Wilaya (DAS).

Hii duplication inawafanya hata hawa ma-RAS na DAS kufanya kazi chini ya kiwango kwa kuwaogopa RC na DC.
 
Lakini kama walimu wamepewa nyenzo zote na mitoto ina feli inapaswa walimu wale mboko.Lakini kama walimu hawana nyenzo zote zinazo takiwa kufundishiwa huyu mkuu wa wilaya inabidi naye ale mboko kwa nini hajapeleka mahitaji ya msingi katika shule husika?
 
Lakini kama walimu wamepewa nyenzo zote na mitoto ina feli inapaswa walimu wale mboko.Lakini kama walimu hawana nyenzo zote zinazo takiwa kufundishiwa huyu mkuu wa wilaya inabidi naye ale mboko kwa nini hajapeleka mahitaji ya msingi katika shule husika?

Na kama Rais amepewa nchi yenye kila kitu mf. maji, madini, watu, ardhi nzuri sana n.k; na anashindwa kuwaletea wananchi wake maendeleo tumfanyeje? Kama kwa kosa la wanafunzi kushindwa mtihani wa taifa walimu wanalambwa bakora, nadhani hawa wakulu walioshindwa karibu kila kitu watahitaji adhabu kubwa zaidi. Kwa mnyambuliko huo, itabidi tuwe na kiwanda cha kutengeneza vitanzi vya kutosha:eek:!
 
Rimkuu ra wiraya hiyo rimerogwa....rinaramba waarimu mboko bira soni...kwani hao 32 ndio warioferishwa mitoto ya huko katerero?
 
Walimu huenda wakawacha kazi ikiwa adhabu ni bakora.

Mbona wao wanaadhibu wanafunzi pindi wanapo kosea!
Kwa hiyo wao hawakosei na wao wanastahili adhabu kama hizo pia tena mbele ya wanafunzi kesho wawe makini na kazi zao.
 
Kama kuna jina ambalo ungestahili kwa kigeugeu hiki cha hoja basi ni MALAYA ni kipi haswa unachosimamia ndugu yetu? mara kuchapwa sio sawa mara iwe sawa? au analysis yako isiyo poor haina principles inazo zisimamia? im out here, my grade three daughter will respond to your next st*p*d post.

Is better if you have decided to shout down your ignorant bowl! But if you are among those DCs we shall haunt you for the rest of ur life......for betterment of our nation!
 
Na kama Rais amepewa nchi yenye kila kitu mf. maji, madini, watu, ardhi nzuri sana n.k; na anashindwa kuwaletea wananchi wake maendeleo tumfanyeje?
huyo nae anapaswa kuadhibiwa si uliona ya mwaka jana hapo Mbeya rais alikoswa koswa na mawe...asichezee watu kama ameshindwa kazi si anaaachia ngazi tuna watu kibao wanaweza kufanya hivyo.Angalia kule Thailand kiongozi akileta za kuleta nchi nzima watu wanachachamaa.
nadhani hawa wakulu walioshindwa karibu kila kitu watahitaji adhabu kubwa zaidi.
Watu kama hawa kwa wenzetu wavimba macho Wachina wangekuwa long time wamenyongwa au wanaoza tu gerezani mtu mmoja anakwiba kiujanja ujanja mabilioni ya pesa bado mnamchekea chekea eti tukimshitaki nchi haita tawalika nani kakwambia????
weka selo huko apumnzike wengine watajifunza kupitia hawa watakao nyongwa na kuwekwa selo na kutaifishwa mali zao uone kama ajira za serikalini watu kama watakuwa wanazikimbilia kama hivi sasa.
 
Kitu cha ajabu kabisa katika mjadala huu ni kwamba kuna watu wanaunga mkono kitendo hiki. Sawa, lakini je mkuu wa wilaya naye achapwe viboko kwa kuchelewesha mishahara yao? kwa sababu katika waliochapwa kuna walimu hawajalipwa mishahara kwa miezi sita? Waziri wa elimu achapwe viboko kwa kuvuja mitihani ? Kama ndiyo hivyo hata Muungwana naye anastahili viboko kwa kujenga shule bila walimu na maabara !! Masha atachapwa sana kwa kuingilia mchakato wa vitambulisho !!
 
Kitu cha ajabu kabisa katika mjadala huu ni kwamba kuna watu wanaunga mkono kitendo hiki. Sawa, lakini je mkuu wa wilaya naye achapwe viboko kwa kuchelewesha mishahara yao? kwa sababu katika waliochapwa kuna walimu hawajalipwa mishahara kwa miezi sita? Waziri wa elimu achapwe viboko kwa kuvuja mitihani ? Kama ndiyo hivyo hata Muungwana naye anastahili viboko kwa kujenga shule bila walimu na maabara !! Masha atachapwa sana kwa kuingilia mchakato wa vitambulisho !!

Ndio maana yake, hii nchi inahitaji viboko kwa kwenda mbele. Tubadilike na kufuata nyayo za mkuu huyo wa wilaya. Punda haendi bila viboko.

Wengine wanaotakiwa kuwajibishwa kwa viboko ni mabwana na bibi afya, madaktari na manesi, waratibu wa elimu. Hizi adhabu zitolewe kwa ranks, yaani boss wako ndio anakutandika viboko. Rais atachapwa viboko na yule aliyemwapisha.

Na pia adhabu iendane na ukubwa wa kosa. Mafisadi wote wanyongwe, hata kama fisadi huyo ni mwalimu mkuu, afisa elimu au mkuu wa wilaya. Cha muhimu ni kutaka ushahidi tu kama alivyotaka ushahidi mkuu wa wilaya kama hajaamrisha hao walimu watiwe mboko.
 
Last edited by a moderator:
The teachers union in Tanzania is considering legal action after 19 school teachers were given the cane.

The primary teachers were caned by a police officer after an inquiry into poor exam results at three schools.

The report blamed teachers for being late or not showing up for work and not teaching the official syllabus.

The deputy education minister has condemned the caning but asked the teachers not to take action until the case has been investigated.

The union is thinking of taking action against District Commissioner (DC) Albert Mnali, who ordered the caning in the northern region of Bukoba.

The BBC's Vicky Ntetema in Dar es Salaam says the case comes at a time when parents and human rights groups in Tanzania have been calling for a ban on flogging of schoolchildren throughout the country.

Deputy Education Minister Mwantumu Bakari Mahiza told the Tanzanian Broadcasting Corporation that the DC's action was "abnormal".

She said the DC and the police commissioner should "have their heads examined" and called for a commission to investigate the case.

Soma hapa
 
Kuna mtu mmoja muhimu anasahaulika katika mjadala huu - yule askari aliyetekeleza hiyo adhabu. Mimi si askari na najua askari wanapaswa kutii amri. Lakini kuna anayeweza kunihakikishia kwa hakika kuwa aliyetekeleza amri ya DC 'mwenye matatizo ya akili' kama huyo wa Bukoba kwa vipi anakuwa safe katika sakata hili?
Nina hakika huyo askari angeambiwa amchape mama yake mzazi angemgeukia DC mwenyewe. Iweje aliona raha kutekeleza amri hiyo kwa walimu?
Huyo ni miongoni mwa askari wengi wanaotumiwa kufanya ujambazi, kunyanyasa na hata kuua raia kwa kisingizio cha kutii amri! Ni kundi moja na wale askari walioua wafanyabiashara wa Madini kutoka Morogoro.
Huyo naye ashughulikiwe.
 
The primary teachers were caned by a police officer after an inquiry into poor exam results at three schools.


The deputy education minister has condemned the caning but asked the teachers not to take action until the case has been investigated.

The union is thinking of taking action against District Commissioner (DC) Albert Mnali, who ordered the caning in the northern region of Bukoba.


Deputy Education Minister Mwantumu Bakari Mahiza told the Tanzanian Broadcasting Corporation that the DC's action was "abnormal".

She said the DC and the police commissioner should "have their heads examined" and called for a commission to investigate the case.

Soma hapa

Jeuri ya madaraka inapomkaa mtu kichwani.
 
Punda haendi bila viboko.
Tatizo kubwa nilililo liona viongozi na wafanyakazi au watumishi wengi wa serikalini wamezoea kujifanyia kazi kwa kusua sua na kusukumwa mtu anafanya kazi anavyo taka.
Ndo maana ufanisi unapungua sana.Hii style ya viboko ndo inawafaa mambo ya kuunda tume tumechoka hayafai tena.Mtu akikosea ni papo kwa papo mnamalizana kama sector binafsi zinavyo fanya.
 
Lakini tusimlaumu pekee huyu mkuu wa wilaya, hata hawa walimu kukubali kwanza kulala chini kupigwa bakora nadhani ni ishara ya mambo mengi kutoka kwa hawa walimu,

1. Hawajiamini
2. Hawajui taratibu zao za kazi
3. Hawawezi hata kujitetea na kuhoji

Kwa hayo tu machache hapo juu inaonyesha ni jinsi gani aina ya wanafunzi watakaotoka chini ya usimamizi au mafunzo toka kwa walimu wa aina hii. Na hili ndio tatizo letu kubwa watanzania, tunarithishana kwa kiasi kikubwa upumbazi, ulegelege n.k. iwe kutoka kwa wazazi au mashuleni.

Haswa!!! hata mimi swali la kwanza nilijiuliza- ivi? hao walimu waliokubali kulala chini na kutandikwa mboko, akili zao zikoje????
 

Haswa!!! hata mimi swali la kwanza nilijiuliza- ivi? hao walimu waliokubali kulala chini na kutandikwa mboko, akili zao zikoje????

Mkuu kama ndo hivyo kila mtu angekuwa anajivunjia sheria.
Ndo maana wewe ukisimamishwa na trafic utasimama au polisi akija kukukamata utatii amri kwa nini usikatae na yule ni boss wao.
 
Unajua toka jana niliposoma hii habari najiuliza maswali mengi sipati majibu. Je hao polisi kwa nini hawakukataa kuwachapa viboko hawa waalimu? Je ni sehemu ya kazi yao kuadhibu Watanzania wasiofanya vizuri kazi zao? Kwa nini hawa waalimu hawakukataa kuchapwa na kuomba chama chao cha wafanyakazi kiingilie? Mwishowe kwa nini huyu DC bado yuko kazini? Naomba awe jela au hospitali ya wagonjwa akili. Je wazazi wa wanafunzi wa hii shule au hizo shule wanasema nini kuhusu hili?
Nisaidieni maana sielewi kinachoendelea kuhusu hili.
 
Back
Top Bottom