DC Bukoba aamuru walimu wachapwe mboko!

DC Bukoba aamuru walimu wachapwe mboko!

yule Raisi wa wilaya ya Bukoba kasimamishwa kazi!kwa kuwachambanga walimu viboko
 
Je! kitendo kilichofanywa na Mkuu wa Wilaya BUKOBA Albert Mnari, naogopa kumuita mheshimiwa kwa kitendo cha aibu alichokifanya cha kuwacharaza bakora walimu wa shule za msingi Katerero, Kanazi na Kansenene kwa wanafunzi kufeli mtihani wa darasa la saba kilikuwa ni kitendo cha busara?. Je adhabu hiyo ipo kwenye mkataba wa kazi wa walimu hao? Na je walimu wanaruhusiwa kuchapwa bakora wafanyapo makosa? Sheria inasemaje? Imekuwa ikielezwa kila siku kwamba wanafunzi wasichapwe bakora? Je kwa walimu inakubalika?

Kwa mawazo yangu hicho kilikuwa ni kitendo cha udhalilishaji na ni kitendo cha aibu na cha kinyama. Iwapo wanafunzi watapata habari kuwa walimu wao walichapwa bakora kutakuwa na implication gani? Wanafunzi hawatawatii wala kuwaheshimu walimu wao. Pili walimu watakosa na wamekosa imani na serikali yao. Kweli walimu wamedhalilishwa kiasi kwamba fildi ya ualimu haina mvuto tena.

Mimi ni mwalimu, nimeongea na walimu wenzangu jinsi walivyoliona suala hili? Wengi wamesema walimu hawaheshimiwi/hatuheshimiwi tena. Pia wapo waliosema kuna haja ya kufanya maandamano ya amani kuonyesha serikali kwamba kitendo hicho cha kuchapa walimu bakora hakikuwa kitendo cha busara. Na sidhani kama kitasaidia wanafunzi kufaulu. Je walimu hao kuchapwa bakora kimeondoa aibu ya wilaya hiyo kuwa ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba? Ninafikiri mkuu huyo wa Wilaya angekutana na walimu hao na kuangalia sababu za kufeli kwa wanafunzi kuliko kuanza na bakora. Ninafikiri sasa nitafute kazi nyingine kwani ipo siku nami nitachapwa bakora?

Walioguswa na kitendo hiki mna maoni gani?
 
Nitashangaa kusikia DC huyo akiwa bado kwenye nafasi hiyo ifikapo kesho jioni. Inabidi asimamishwe kazi haraka iwezekanavyo!!!! Ebo!!!!!!!.

Rais Jakaya Kikwete amemvua mamlaka ya ukuu wa wilaya na kumfukuza kazi mara moja bwana Mnali kwa sababu kitendo alichokifanya ni cha udhalilishajiw a hali ya juu
 
Mara baada ya kutuma maoni yangu kuhusu kitendo alichokifanya Mkuu wa Wilaya ya Bukoba lilipita tangazo katika Telelvision ITV sambamba na taarifa ya habari kuhusu kusimamishwa kazi kwa Mkuu huyo wa Wilaya na Raisi Jakaya Mrisho Kikwete. Ninampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kitendo cha kumfukuza kazi Mkuu wa Wilaya ya Bukoba. Apewe adhabu kali ikiwezekana achapwe bakora sawa na idadi ya fimbo alizoamuru walimu wote 32 wachapwe.
 
Yaani na hao walimu kweli walikubali kucharazwa mboko? Ingekuwa mimi wangeniua tu....
Kwanza bado nina hasira sana na walimu wote waliowahi kunicharaza mboko na nimeshaapa kila nitakayekutana naye mimi ni kibano tu.
 
Rais Jakaya Kikwete amemvua mamlaka ya ukuu wa wilaya na kumfukuza kazi mara moja bwana Mnali kwa sababu kitendo alichokifanya ni cha udhalilishajiw a hali ya juu

really? some more info please?
 
Rais Jakaya Kikwete amemvua mamlaka ya ukuu wa wilaya na kumfukuza kazi mara moja bwana Mnali kwa sababu kitendo alichokifanya ni cha udhalilishajiw a hali ya juu

Mpita Njia tunashukuru, pia nimesoma/nimeona kwenye michuzi
"""JK amemvua madaraka na kumtimua kazi Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Albert Mnali kutokana na kitendo chake cha kuamrisha kuchapwa bakora hadharani waalimu wa shule za msingi za Katerero, Kanazi na Kasenene juzi kwa sababu zilizoelezwa kushindwa kuwajibika na kufanya shule hizo zidorore katika masomo.
Taarifa kutoka O fisi ya Waziri Mkuu iliyotolewa sasa hivi nasema kwamba serikali imepokea kwa kwa masikitiko makubwa na kitendo hicho na kukitaja kuwa hakikubaliki na ni cha kudhalilisha."""
 
yule Raisi wa wilaya ya Bukoba kasimamishwa kazi!kwa kuwachambanga walimu viboko

Sasa hivi CCM lazima wafukuzane makazi maana upepo wa mabadiliko unajongea,ila wacha wafukuzane kadiri watakavyoweza lakini wakumbuke kuwa muda wao wa kukaa madarakani kuiongoza Tanzania unakaribia kufikia upeo ,hakuna watakaemueka maana wote wameoza ,si unajua ile methali isemayo akioza samaki mmoja ndio wameoza wote ,sasa tunangojea nini kama hatujatafuta samaki wepya wakati wavuvi ndio siesie tunaopiga miayo,lazima CCM wang'olewe wakitaka wasitake muda waliokaa umeitosha kabisa,sasa wale wasio wahi kuchukua chao mapema ndio wasijaribu kwani sa mbaya itawabidi wakae chonjo.
 
Rais Jakaya Kikwete amemvua mamlaka ya ukuu wa wilaya na kumfukuza kazi mara moja bwana Mnali kwa sababu kitendo alichokifanya ni cha udhalilishajiw a hali ya juu

Pamoja na hiyo hatua ambayo hakika ndiyo iliyotakiwa, kitendo cha hawa waalimu kukubali kuchapwa viboko kinatoa ushahidi wa kutosha juu ya ukondoo wa mtanzania ninayemfahamu. Utiifu wetu kwa viongozi hata pale tunapodhulumiwa na kunyanyaswa wazi wazi, hauelezeki kwa lugha yoyote ile - ni ujinga. Hivyo hata CCM inapotuswaga kuelekea shimoni kwenye umasikini na balaa, tunafuata tu - si ndiyo jadi yetu ? Na tunatii kwa majigambo ya amani na utulivu, masikini, hatuna tofauti na waalimu hawa !!
 
Yaani na hao walimu kweli walikubali kucharazwa mboko? Ingekuwa mimi wangeniua tu....
Kwanza bado nina hasira sana na walimu wote waliowahi kunicharaza mboko na nimeshaapa kila nitakayekutana naye mimi ni kibano tu
.

Nyani washukuru hao walimu, mpaka leo hii ungalikuwa unaishi na ndugu zako, gorilla, apes, chimpanzee, tumbili and the like. Nyani usiniue, ni utani tu mwanawane. wabeja!
 
Rais Jakaya Kikwete amemvua mamlaka ya ukuu wa wilaya na kumfukuza kazi mara moja bwana Mnali kwa sababu kitendo alichokifanya ni cha udhalilishajiw a hali ya juu

hanks for info mkuu nimeona pia kwa MICHUZI blog!
 
Mpita Njia tunashukuru, pia nimesoma/nimeona kwenye michuzi
"""JK amemvua madaraka na kumtimua kazi Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Albert Mnali kutokana na kitendo chake cha kuamrisha kuchapwa bakora hadharani waalimu wa shule za msingi za Katerero, Kanazi na Kasenene juzi kwa sababu zilizoelezwa kushindwa kuwajibika na kufanya shule hizo zidorore katika masomo.
Taarifa kutoka O fisi ya Waziri Mkuu iliyotolewa sasa hivi nasema kwamba serikali imepokea kwa kwa masikitiko makubwa na kitendo hicho na kukitaja kuwa hakikubaliki na ni cha kudhalilisha."""

Serikali ilikuwa haipo ? leo ni siku ya tano toka kufanyika kwa tendo hili ,je serikali ilikuwa inanisubiir mpaka pale nilipowazungumza kwamba si kweli Raisi,PM na waziri wake hawana habari ndio wamekurupuka aidha walikuwa wanasubiri mshindo wa WaTanzania, kwa kweli ni aibu kwa serikali hii ambayo inajisifu kuwa imejikita kila pembe ya Tanzania,naamini kabisa hao niliowataja hapo walisikia once kitendo kilipofanyika maana ni kitendo kisichostahili kufanyiwa wafanyakazi wa serekalini na hata wale wasekta binafsi, kwani kuchelewa kazini kunafuatiwa na onyo la barua rasmi na ikiwa onyo hilo halikufua dafu ni kufukuzwa kazi vilevile kwa barua rasmi ,DC aliziona taratibu hizo zote hazifai na ni kucheleweshana.

Viongozi hao wakuu kuanzia Mkuu wa Mkoa ichunguzwe nae alichukua hatua gani ,je alitaarifu uongozi wa juu pale aliposikia kioja hicho ? Au alikaa nae kusikiliza mshimndo ? Tunaweza kusema Raisi alisikia kutoka kwa mashushu lakini akangoja ushahidi kamili wa Mkuu wa Mkoa ,aidha Mkuu wa Mkoa sina uhakika kama anaweza kumsimamisha kazi ,lakini kwa upande fulani ikiwa amehakikisha tendo hilo limefanywa angeweza kabisa kumsimamisha kazi na japo sio kumfukuza bila ya shaka aliona atamvunjia heshima mwenziwe kwa kumsimamisha kazi ,anaogopa ,atakuwa hana adabu ,ndio maana yake viongozi waliopewa madaraka wanashindwa kukemea wanashindwa kuwawajibisha wababe anangojewa Raisi ndipo pale niliposema kuwa hawa wote wameoza na kunahitajiwa Chama cha uongozi chengine CCM hawafai kwani wanaogopana ,mi nakuaminia kabisa Mkuu wa mkoa anamwogopa hata balozi wa nyumba kumi kumi ,sasa hapa unafikiri kuna utawala wa kufuata sheria ni mazonge tu ,Kikwete nae amakerupuka baada ya siku kibao kupita ameona joto linaanza kupanda kwa kasi ,kwani Kikwete anaielewa vizuri maana ya kasi ,sasa afahamu tu anaposikia udhalilishaji kama huu basi ampigie simu muhusika moja kwa moja na kumuuliza ,eti jamani kama huyo DC baada ya kufanya mauzauza hayo ,na Mheshimiwa Raisi kusikia basi Mheshimiwa angeweza kumhoji direct na baada ya kupata uhakika kuwa jamaa amekiri ,hapohapo angekata simu na kutangaza kumsimaisha kazi na sheria ya kunyanyasa au kudhalilisha ichukue mkondo wake aidha na walimu walipwe fidia na mwajiri aliewadhalilisha mambo ya kufukuzana kazi halafu jamaa akawa anapeta uraiani hayatoshi tunataka kusikia kuwa amekwenda jela mwaka mmoja na kila asubuhi anachapwa kiboko kimoja tu, ubabe tu ,ndio maana yake.
 
Serikali ilikuwa haipo ? leo ni siku ya tano toka kufanyika kwa tendo hili ,je serikali ilikuwa inanisubiir mpaka pale nilipowazungumza kwamba si kweli Raisi,PM na waziri wake hawana habari ndio wamekurupuka aidha walikuwa wanasubiri mshindo wa WaTanzania, kwa kweli ni aibu kwa serikali hii ambayo inajisifu kuwa imejikita kila pembe ya Tanzania,naamini kabisa hao niliowataja hapo walisikia once kitendo kilipofanyika maana ni kitendo kisichostahili kufanyiwa wafanyakazi wa serekalini na hata wale wasekta binafsi, kwani kuchelewa kazini kunafuatiwa na onyo la barua rasmi na ikiwa onyo hilo halikufua dafu ni kufukuzwa kazi vilevile kwa barua rasmi ,DC aliziona taratibu hizo zote hazifai na ni kucheleweshana.

Viongozi hao wakuu kuanzia Mkuu wa Mkoa ichunguzwe nae alichukua hatua gani ,je alitaarifu uongozi wa juu pale aliposikia kioja hicho ? Au alikaa nae kusikiliza mshimndo ? Tunaweza kusema Raisi alisikia kutoka kwa mashushu lakini akangoja ushahidi kamili wa Mkuu wa Mkoa ,aidha Mkuu wa Mkoa sina uhakika kama anaweza kumsimamisha kazi ,lakini kwa upande fulani ikiwa amehakikisha tendo hilo limefanywa angeweza kabisa kumsimamisha kazi na japo sio kumfukuza bila ya shaka aliona atamvunjia heshima mwenziwe kwa kumsimamisha kazi ,anaogopa ,atakuwa hana adabu ,ndio maana yake viongozi waliopewa madaraka wanashindwa kukemea wanashindwa kuwawajibisha wababe anangojewa Raisi ndipo pale niliposema kuwa hawa wote wameoza na kunahitajiwa Chama cha uongozi chengine CCM hawafai kwani wanaogopana ,mi nakuaminia kabisa Mkuu wa mkoa anamwogopa hata balozi wa nyumba kumi kumi ,sasa hapa unafikiri kuna utawala wa kufuata sheria ni mazonge tu ,Kikwete nae amakerupuka baada ya siku kibao kupita ameona joto linaanza kupanda kwa kasi ,kwani Kikwete anaielewa vizuri maana ya kasi ,sasa afahamu tu anaposikia udhalilishaji kama huu basi ampigie simu muhusika moja kwa moja na kumuuliza ,eti jamani kama huyo DC baada ya kufanya mauzauza hayo ,na Mheshimiwa Raisi kusikia basi Mheshimiwa angeweza kumhoji direct na baada ya kupata uhakika kuwa jamaa amekiri ,hapohapo angekata simu na kutangaza kumsimaisha kazi na sheria ya kunyanyasa au kudhalilisha ichukue mkondo wake aidha na walimu walipwe fidia na mwajiri aliewadhalilisha mambo ya kufukuzana kazi halafu jamaa akawa anapeta uraiani hayatoshi tunataka kusikia kuwa amekwenda jela mwaka mmoja na kila asubuhi anachapwa kiboko kimoja tu, ubabe tu ,ndio maana yake.

Mwiba, tusipende kila wakati kulaumu tu, hata pale tunapoona kuna ukweli. Hutakiwi unaposikia jambo mara moja unamchukulia mtu hatua, kwanza ni vizuri kupata ukweli. Yaweza kweli kuwa siku zimepita tangu tukio litokee, lakini nadhani kuna mambo yalikuwa yanafuatiliwa kwanza.

Unaposema Mkuu wa Mkoa alichukua hatua gani,kwa mujibu wa magazeti alishapeleka taarifa kwa Waziri Mkuu, soma hapa HabariLeo: Gwiji la habari Tanzania | DC aliyechapa walimu ashitakiwa kwa Pinda.

Mimi nadhani kufukuzwa tu haitoshi, hawa waalimu wanahitaji ushauri, manake mmoja niliyemsikia akihojiwa na BBC yaonesha kuna kudhalilika kukubwa mbele ya wanafunzi wao. Pia wanaweza kwenda mahakamani.
 
yule Raisi wa wilaya ya Bukoba kasimamishwa kazi!kwa kuwachambanga walimu viboko

Yeees First Ledi, Jk amemvua U-DC na kumfukuza kazi Bw. Albert Mnali aliyejuwa DC wa Bukoba kwa kudhalilisha walimu.
Anakaribishw akatika dunia ya kujitafutia riziki kwa jasho.
 
Nyani washukuru hao walimu, mpaka leo hii ungalikuwa unaishi na ndugu zako, gorilla, apes, chimpanzee, tumbili and the like. Nyani usiniue, ni utani tu mwanawane. wabeja!

Hahahahaah Mwanamalundi hahaha inamaana ndugu yetu anagekuwa porini akijinafasi?
 
Yeees First Ledi, Jk amemvua U-DC na kumfukuza kazi Bw. Albert Mnali aliyejuwa DC wa Bukoba kwa kudhalilisha walimu.
Anakaribishw akatika dunia ya kujitafutia riziki kwa jasho.

Huyo jamaa inaonyesha ameshajichukulia chake mapema sasa akitafuta njia ya salama kuondoka serikalini ,si unajua ukiwacha kazi kwa kufuata sheria CCM wenzako hawakuwachi watakufilisi kila kitu,lakini kwa njia alioondokea atakuwa akipeta tu mitaani.
 
Yaani na hao walimu kweli walikubali kucharazwa mboko? Ingekuwa mimi wangeniua tu....

Mbona watanzania kwa ujumla wetu kila siku tunalala chini na kuchapwa viboko na MAFISADI wa CCM. Hao waalimu ni reflection ya watanzania walio wengi - si ndivyo tulivyo ? Afadhali huyo DC kawajibishwa - CCM itawajibishwa na nani ?
 
Back
Top Bottom