DC Bukoba aamuru walimu wachapwe mboko!

Yupo timamu kabisa, inaonekana hiki kitendo kimemsikitisha sana na dawa ya karibu aliyoiona ni kuwatandika tu viboko badala ya kuunda tume kama watanzania tulivyozoea.

Manake uundaji wa tume na utekelezaji wa majukumu yake aliona yangemchukulia muda mrefu pengine bila majibu ambayo angeyapenda yeye.

Hii ni aibu kubwa si kitu cha kukisifia wala kukishabikia kuwa DC kafanya la maana.Si ujinga tu bali ni upumbavu usiopaswa kuvumiliwa.Anapaswa achishwe kazi.
Walimu waliocharazwa viboko, tisa wanatoka Shule ya Msingi Katerero, 11 wa Shule ya Msingi Kanazi ambao walichapwa viboko viwiwili kila mmoja na walimu 12 kutoka Shule ya Msingi Kansenene walichapwa viboko vinne vinne kila mmoja.
Fikiria kiini cha tatizo la msingi ni kutokana na wilaya hiyo kuwa ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba.
Hivi Lindi ilipokuwa ya mwisho walimu walizomewa?achana nahilo la kupigwa VIBOKO mbele ya kadamnasi.
Ona kiburi cha mawazo yaliyoganda ya DC katika fikra zake, Alisema uzembe huo umesababisha wilaya ya Bukoba kuwa ya mwisho kimkoa katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka jana na kuwa uamuzi huo utasaidia kuwakumbusha walimu wajibu wao.
Kama kweli viboko vinamkumbusha mfanayakazi mwajiriwa nani aliyewahi kumpiga viboko yeye DC ili aweze kukumbuka wajibu wake.Yeye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya, mbona mazeruzeru wanakatwa viungo na kuuliwa wilayani kwake?
Huyu jamaa kwanza si kweli kuwa hajui hapo wilayani kuna ofisi ya elimu ya Wilaya. Tena katika idara ya elimu kuna wakaguzi wa elimu wa kuanzia ngazi ya kanda kushuka chini hadi kata ambako tunawakuta waratibu elimu kata.
Hajaonyesha amefanya jitihada gani kusoma ripoti zao.Matatizo ya shule nyingi za msingi tchanzo si walimu bali ni serikali yenyewe.Walimu wanavunjwa moyo na namna serikali inavyoshughulikia matatizo yao.Soma zile articles za mwanzo mwanzo ambazo Haki Elimu walikuwa wanatoa, wakitazama kwa jicho la pili hali ya ELIMU YA MSINGI Tanzania, utajua ni kwanini serikali ya Mkapa ilizipiga vita.
Mwalimu siyo mhuni wa Katerero wala wa Kansenene.Ni mfanayakazi aliyeajiriwa kwa mujibu wa sheria inayozingatia taaluma yake. Ziko taratibu za kumwadhibu mtumishi/mwajiriwa.Nani kasema DC ni mwajiri wa Walimu katika Wilaya yoyote Tanzania hata awe na haki ya kuwaadhibu, si kihuni kama ivyo bali hata kwa mujibu wa sheria?
DC kawadhalilisha walimu naam si walimu tu bali watanzania wote wanaoiwazia mema tanzania.Niko hapa nilipo kwa sababu ya mwalimu,wako hapo walipo kwasababu ya walimu.
Nasisitiza hii ni fedheha kuu isiyopaswa kuvumiliwa.Ni sawa na mtoto aliyesomeshwa na mam yake kwa kufanya kazi ya kupika na kuuza pombebaada ya kumaliza kidato cha sita akapata kazi shirika la bandari.Kwa kiburi cha pesa akaja nyumbani akamwona mama yake kachafuka na machicha ya pombe akaanza kumpiga kwanini anakuwa mchafu-mchafu na kwanini anaendelea kupika pombe; mbele ya wadogo zake ambao bado wako shule ya msingi.
 
Hii imetulia sanaaa. Walimu wetu nao wamebweteka sana. Anyway hata Julius Nyerere aliwahi kumchapa waziri wake sembuse mwalimu? Mzee Mkuu Wa Wilaya wakirudia tena kutufanya tuwe wa mwisho tunawapa mboko mbele ya wanafunzi wao. BIG UP DC
 
Hii imetulia sanaaa. Walimu wetu nao wamebweteka sana. Anyway hata Julius Nyerere aliwahi kumchapa waziri wake sembuse mwalimu? Mzee Mkuu Wa Wilaya wakirudia tena kutufanya tuwe wa mwisho tunawapa mboko mbele ya wanafunzi wao. BIG UP DC

kama mie mzazi wangu angekuwemo ktk lile kundi la walimu walochapwa viboko,basi vita yangu na huyo DC ingekuwa kuliko ya HAMAS na FATAH kule PALESTINE.
 
Nampongeza sana huyo mkuu wa wilaya waache watandikwe....si majuzi 2 wametoka kugoma hapa oooh hawajalipwa pesa zao,wakalipwa, sasa kwanini wasitekeleze wajibu wao.Hongera sana mkuu wa wilaya endelea hivyohivyo watandike tena ikibidi mbele ya wanafunzi!!!!!!!

Wewe bwana mdogo unaonekana hujui kabisa na wala huna hata fununu za maisha halisi ya walimu wetu wa shule za msingi! Laiti ungeyajua maisha yao, ungeweza hata kuchukua uamuzi wa kujinyonga kwa COMMENT zako za KIFISADI!
 
Lakini tusimlaumu pekee huyu mkuu wa wilaya, hata hawa walimu kukubali kwanza kulala chini kupigwa bakora nadhani ni ishara ya mambo mengi kutoka kwa hawa walimu,

1. Hawajiamini
2. Hawajui taratibu zao za kazi
3. Hawawezi hata kujitetea na kuhoji

Kwa hayo tu machache hapo juu inaonyesha ni jinsi gani aina ya wanafunzi watakaotoka chini ya usimamizi au mafunzo toka kwa walimu wa aina hii. Na hili ndio tatizo letu kubwa watanzania, tunarithishana kwa kiasi kikubwa upumbazi, ulegelege n.k. iwe kutoka kwa wazazi au mashuleni.
 
Last edited:
Kinachonisikitisha ni kuwa walimu hao WALIKUBALI kuchapwa viboko! Halafu sasa wanabembeleza serikali iwaone huruma! Hivi huko Bukoba hakuna mawakili? Wanangoja nini kumburura mahakamani huyo DC na serikali? Haki haupewi, inabidi uihangaikie.

Amandla...........
 
kama mie mzazi wangu angekuwemo ktk lile kundi la walimu walochapwa viboko,basi vita yangu na huyo DC ingekuwa kuliko ya HAMAS na FATAH kule PALESTINE.

Sasa sawa Engineer...unajua mijitu mingine inashabikia tuuuuuuuuuu! hata hawajui the real life ya hawa walimu, pia hawaanalyse issue iliyo sababishwa wachapwe..eti kuwa wa mwisho....sheet! wilaya inaweze kuwa ya mwisho lakini imefaulisha vijana wengi just wakatofautiana viwango vya ufaulu au wanaweza kuwa wamefeli sana, je tunajua mazingira ya kazi ya hawa walimu? Je, wanavitendea kazi vyote, je, wanalipwa mafao yao in time, je, suala la miundo mbinu nalo limekaaje(barabara, simu,hospital etc), je, wanafunzi maisha yao yakoje huko?je, na wazazi wao wanamwako kiasi gani huko, je,kuna uhusiano mzuri kati ya walimu na wananchi kwenye shule hizo?

Mimi ninauhakika majibu kwenye maswali hayo, moja wapo yatailenga serikali (kijiji,kata,tarafa,wilaya-kwa huyu Albert,mkoa na taifa), sasa na yeye ajitandike viboko basi na kama kuna uzembe ulitoke ktk ngazi ya taifa akawachape viboko mawaziri husika na Raisi!

Yaani huyu jamaa natamani nizitafune p***u zake hata kama waliofanyiwa hivyo si ndugu zangu kabisa but ni watanzania wenzangu walala hoi!
 
Yes,hii ni kali,jazba ya DC imepanda mpaka kaamua kuchukua sheria mkononi mwake.Hii inaonyesha wazi aina ya viongozi tulio nao!Unajua, ni kama wewe ukiwa una oga mtoni, halafu ghafla kichaa akaja na kuchukua nguo zako, halafu wewe ukatoka mtoni na kuanza kumfukuza kichaa yule kwa nia ya kumnyanganya nguo zako,sijui nani ataonekana kichaa.Nadhani jibu liko wazi.Serikali kama bado ipo,maana sina hakika ,imchukulie DC huyo hatua kali za kinidhamu,ikiwa ni pamoja na kumfukuza kazi.Haijalishi kama waalimu wana makosa au hawana!

Nimesoma kwenye gazeti la mwananchi. Kuna walimu 32 wamechapwa. Mkuu wa wilaya aamuru polisi kucharaza bakora walimu 32. Ni kutokana na matokeo mabaya ya mtihani darasa la saba. MKUU wa Wilaya ya Bukoba, Albert Mnali aliamuru polisi mmoja kuwachapa viboko walimu katika shule tatu za msingi zilizo Bukoba, kutokana na wilaya hiyo kuwa ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba.

Jamani tumefika huko?
 
Lakini tusimlaumu pekee huyu mkuu wa wilaya, hata hawa walimu kukubali kwanza kulala chini kupigwa bakora nadhani ni ishara ya mambo mengi kutoka kwa hawa walimu,

1. Hawajiamini
2. Hawajui taratibu zao za kazi
3. Hawawezi hata kujitetea na kuhoji

Kwa hayo tu machache hapo juu inaonyesha ni jinsi gani aina ya wanafunzi watakaotoka chini ya usimamizi au mafunzo toka kwa walimu wa aina hii. Na hili ndio tatizo letu kubwa watanzania, tunarithishana kwa kiasi kikubwa upumbazi, ulegelege n.k. iwe kutoka kwa wazazi au mashuleni.

Usitegemea hayo kabisa kutoka kwa ''typical'' walimu wetu wa shule za msingi hasa za huko vijijini......! hawajiamini, hawajui taratibu zao kazi, hawawezi kujitetea kwa sababu wao wenyewe ni vilaza wa kutupwa...most of them ni failures wa f4...sasa what do you expect from them! So hawa inabidi watetewe na wengine wanaojua haki zao kama wewe! We still need them, cause hatuna option for now...hiyo ndo hali halisi ya elimu ya tanzania!
 
Yes,hii ni kali,jazba ya DC imepanda mpaka kaamua kuchukua sheria mkononi mwake.Hii inaonyesha wazi aina ya viongozi tulio nao!Unajua, ni kama wewe ukiwa una oga mtoni, halafu ghafla kichaa akaja na kuchukua nguo zako, halafu wewe ukatoka mtoni na kuanza kumfukuza kichaa yule kwa nia ya kumnyanganya nguo zako,sijui nani ataonekana kichaa.Nadhani jibu liko wazi.Serikali kama bado ipo,maana sina hakika ,imchukulie DC huyo hatua kali za kinidhamu,ikiwa ni pamoja na kumfukuza kazi.Haijalishi kama waalimu wana makosa au hawana!

Mkuu,
Huyu Albert na mwenzake Yule DC wa Mbarali aliyempiga kibao mwanakijiji tena mbele ya kamati ya Bunge ya Ardhi na Kilimo wanaonyesha kuwa tuna baadhi ya viongozi ambao ni mbumbumbu kweli.
Nadhani wanastahili kufundisha ngumi na ubabe kule Keko au segerea.
Pia wawahi kuwapeleka hospitali ya Milembe Dodoma kabla afya ya akili haijaathirika yote.
 
Wana JF kuchapwa kwa walimu hawa ni ishara kuwa walimu ni wadhaifu? Kwanini chama cha walimu mkoa kisimpeleke mkuu wa wilaya mahakamani? Kwanini walimu wasiungane kukomesha hili? Usizhangae ukasikia mkuu wa wilaya chunya kachapa maana viongozi wengi huiga hasa kama huyu mkuu wa wilaya kahamishwa.
napingana na wote wanaoafiki kitendo cha mkuu wa wilaya. Ni bora angewafukuza. Kumchapa mwalimu eti kafelisha ni kosa kubwa. Kuna sababu nyingi za mwanafunzi kufeli. Ingawa mwalimu nae anaweza kuwa ni sababu, ila mzazi, mkuu wa wilaya (serikali), mazingira, mwanafunzi mwenyewe n.k ni baadhi tu ya vitu vinavyoweza mfelisha mwanafunzi. Akachape mwanafunzi, akachape mazingira na yeye ajichape. Kushabikia kitendo cha mkuu wa wilaya si vizuri. Eti zamani Nyerere alimchapa waziri, kwahiyo tunaiga.
Mimi imenisikitisha sana, mzazi/mlezi/kaka/dada/shangazi/n.k wako mwalimu akachapwa utajisikiaje?
Walimu wanamasrahi duni, bado unawanyanyasa. Inauma sana, inasikitisha sana na inazalilisha sana. Anyway, kunasiku sauti hizi za chini zitakuja sikika maana liubiliwalo uvunguni kunasiku litaubiliwa paani.
I hate this downtrodden, oppression, suppression, dehumanization.
kama wewe unafahamu mazungira ya walimu, kama wewe ni mwalimu, kama wewe mpenda maendeleo basi huwezi kuchekelea uamzi wa mkuu wa wilaya. Ni kweli kila mtu anamtazamo wake lakini kuna mitazamo mingine inawalakini.
Poleni sana walimu kwa kuzalilishwa, poleni sana watanzania. Walimu shirikianeni muondoe hii dhana ya kuwa wanyonge. It is possible to make changes
 
What is required is Mild Dictatorship. DC amepata uchungu nadhani kwa sababu mbili. Moja wilaya yake kuwa wa mwisho mkoani. Hii ina maana katika KPI zake zinamuharibia. Pili wanafunzi wanaharibiwa future yao kwa sababu waalimu hawakutimza wajibu wao. Waalimu wamekuwa wakidai malipo yao na wamepewa basi ni zamu yao kutekeleza wajibu wao.
 
What is required is Mild Dictatorship. DC amepata uchungu nadhani kwa sababu mbili. Moja wilaya yake kuwa wa mwisho mkoani. Hii ina maana katika KPI zake zinamuharibia. Pili wanafunzi wanaharibiwa future yao kwa sababu waalimu hawakutimza wajibu wao. Waalimu wamekuwa wakidai malipo yao na wamepewa basi ni zamu yao kutekeleza wajibu wao.

Heri, kufeli kwa wanafunzi kumesababishwa na walimu?
Hakuna sababu zingine zinazomfanya mwanafunzi afeli?
 
What is required is Mild Dictatorship. DC amepata uchungu nadhani kwa sababu mbili. Moja wilaya yake kuwa wa mwisho mkoani. Hii ina maana katika KPI zake zinamuharibia. Pili wanafunzi wanaharibiwa future yao kwa sababu waalimu hawakutimza wajibu wao. Waalimu wamekuwa wakidai malipo yao na wamepewa basi ni zamu yao kutekeleza wajibu wao.

Unajua unachokiongea au unasema tu mnadi uonekane na wewe umechangia.....no facts no right to talk!
 
Usitegemea hayo kabisa kutoka kwa ''typical'' walimu wetu wa shule za msingi hasa za huko vijijini......! hawajiamini, hawajui taratibu zao kazi, hawawezi kujitetea kwa sababu wao wenyewe ni vilaza wa kutupwa...most of them ni failures wa f4...sasa what do you expect from them! So hawa inabidi watetewe na wengine wanaojua haki zao kama wewe! We still need them, cause hatuna option for now...hiyo ndo hali halisi ya elimu ya tanzania!

Umesema kweli, lakini sio kila mara ni kusubiri kutetewa tu na watu wengine, inabidi wao binafsi kuchukua hatua na kutaka kuzijua haki zao. Kwa tukio hili unaweza kuwa mwanzo kwa wao kufunguka akili.....lakini wakilala wakitegemea kuwa watakuja kutetewa na activists wakati mwingine wanaweza wasije au wakaja wamechelewa sana na wao wameshaathirika vibaya.
 
Hii imetulia sanaaa. Walimu wetu nao wamebweteka sana. Anyway hata Julius Nyerere aliwahi kumchapa waziri wake sembuse mwalimu? Mzee Mkuu Wa Wilaya wakirudia tena kutufanya tuwe wa mwisho tunawapa mboko mbele ya wanafunzi wao. BIG UP DC

I did not expect this disappointing comment from Eeka Mangi!
 
Je Mheshimiwa Kikwete nae aamuru kumchapa mkuu huyo wa Wilaya ? Maana tunatakiwa kuishi kwenye utawala wa Samaki mkubwa kumla mdogo ,ndio maana yake !
 
Hivi jamani mnao watetea hao walimu kwa misingi ya haki za binadamu mnaju na hao wanafunzi pia wana haki zao? mkuu wa wilaya kaamuru walimu 32 tu ndio wachapwe viboko kwani mnajua wilaya yake ina walimu wangapi? na sababu zilizotolewa kwa kuchapwa hao 32 tu hamkuzielewa? JK huyu ni mfano wa viongozi wenye uchungu na watoto wa taifa hili mpandishe cheo. Tena ikibidi awe waziri mkuu ili viboko viwashukie mawaziri.
 
Bazazi anauliza inakuwaje mtu mzima na akili yake akubali kutandikwa viboko bila amri halali ya Mhe Hakimu kwani ndio mtu pekee kwa mujibu wa katiba anayewezal kutoa adhabu ya VIBOKO kwa mtu ambaye sio mwanafunzi wa kuanzia chekechea hadi kitado cha sita. Nadhani pamoja na DC huyo kuadhibiwa, waalimu nao waadhibiwe kwa kukubali kudhalilishwa.
 
BIG-UP DC! wamzidi mbona wao huwa wanawacharaza wantu pale wanapofeli so mkuki kwa nguruwe..... kumbukeni enzi za mwalinhu tulipokuwa shule za msingi jinsi tulivyokuwa tunachapa ukichelwa kushika namba fimbo, ukifeli mtihani ama testi fimbo tena bila hata ya huruma... Jamani waliosomba Muhimbili enzi hizo mwamkumbuka Mwl. Ndosi yule baba siku akikuvalia jinsi na tshirt ujue siku hiyo kiama akiwa zamu balaa, mkifeli hisabati mmnae sasa hawa kuchapwa ni haki yao maana wameshindwa kuwafundisha wanetu. Wanachojua ni kuwapa wanafunzi miradi yao wawauzie mwanafunzi akikataa ana chapwa walimu wa vijijini wao ni kuwachukua wanafunzi wakawafanyie kazi zao za nyumbani kipindi cha kilimo wanafunzi wananda pia kufanya kazi ktk mashamba ya walimu . DC kanifurahisha sana wnye kuchukia wachukie but narudia tena na tena DC BIG UP kazi nzuri wengine waige mfano wako.
 
Back
Top Bottom