DAWASA Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na ushauri

Ndugu wana JamiiForums,

Tunashukuru kwa maoni yenu mliyoweka hapa juu ya huduma mnazo pata kwenye matawi yetu yaliyo Jijini Dar es salaam , miji ya Kibaha na Bagamoyo Mkoani pwani. DAWASCO inapokea maoni na malalamiko yenu na tuna wahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki kwa haraka zaidi.

Ndugu wana jukwaa, DAWASCO inajipambanua kwa kusimamia maadili ,kutoa huduma iliyotukuka pamoja na kuhakikisha huduma ya Maji inapatikana kwa kila mwananchi.

Kama kutatokea kuharibika kwa bomba, wizi wa Maji, umepata huduma isiyo ridhisha au ufanyaji kazi usiofuata maadili, uaminifu na uadilifu, tafadhali toa taarifa kupitia njia zifuatazo:

1. Kupitia tovuti: DAWASCO - Welcome to new site
2. Kupitia mitandao yetu ya kijamii ikiwa ni pamoja na Twitter|DawascoOfficial..Facebook|DawascoOfficial ...Instagram|DawascoOfficial
3. Kwa mwananchiposta ; Unaweza kutuma barua kwa Afisa Mtendaji kama ifuatavyo:

Afisa Mtendaji Mkuu
DAWASCO
P. O. Box 5340
Sokoine Drive
Dar es Salaam, Tanzania.

4. Au kwa kupiga simu huduma kwa wateja dawasco
0800110064 /022 2164800 ( Kupiga namba hizi ni Bure)

THREAD IMELALA SANA DAWASCO. Ni bora muifunge kama hamkujipanga kuitumia kuwafikia wateja. Kama kuna pesa munailipia, basi ni matumizi yasiyo na tija.
 
Hivi nyinyi kwanini mpo hivyo?

Tokeni maofisini ingieni mitaani muone hasara munayoiingizia serikali.....mabomba yenu 80% machakavu na yanatiririsha maji yanaharibu miundombinu ya barabara nyie mnakula viyoyozi tu ofisini.....mimi ndio ningekuwa magu hakililah ningeanza na nyinyi kwanza kisha wengine wangefata
 
Jamani watu wa tanesco tunaomba kama mnakata umeme taarifa ni muhimu maana mtatuunguzia vitu vyetu
 
DAWASCO,Mungu,anawaona
Mwaka mzima sasa mmefunga barabara toka Tandale- Chama hadi Manjunju Mwananyamala kwa kutengeza madimbwi makubwa kwa mabomba yenuChakavu.
Hatuwezi kwenda ama Tandale sokoni au Mwananyamala hospitali kupitia hapo kwani hata bodaboda haipiti
Madimbwi haya ni Mazalia ya mbu na vimekaza vya magonjwa ya tumbo kwa uchafu huu unaopenya kwenye Bomba zenu
Njooni mtengeneze kama hamuwezi tutafuta msaada kwa Makonda
TUMECHOOOKAAA
 
Nilijaza fomu ya kuomba kuunganishiwa maji. Nilimpeleka surveyor kutoka ofisi zenu zilizoko kimara matangini sasa ni kama mwezi wa pili muko kimya. Nifanyeje sasa?
 
Mimi ni mteja wenu nipo Goba Kunguru kwa Ndambi, Baada ya nyie(DAWASCO) kuamua kusimamia mradi wa maji Goba wananchi wengi walihamasika sana na kuomba kuunganishiwa maji, japo tulikuwa tunapata maji kwa wiki mara 2 au 3 lakini ilikuwa inapendeza sana.
CHANGAMOTO: toka mwezi wa 11, 2017 maeneo yote ya kwa Ndambi hatupati maji, baada ya kuulizia tunaambiwa eti gharama za ku pump maji zimekuwa kubwa sana kwahiyo kwa sasa tutaendelea kukosa huduma.(SINA HAKIKA MAENEO MENGINE YA GOBA KAMA WANAPATA HUDUMA)

OMBI/USHAURI: Kwa sasa unit 1 mnatuuzia 1,200/= ki ukweli ni kiwango cha chini sana ukizingatia mazingira ya eneo la mradi na matumizi ya hiyo pump., hivyo nashauri unit 1 iwe japo 2,000/=
kwa jinsi tunavyo pata shida ya maji na inatugharimu sana kwa sasa kununua maji ambayo siyo salama hatuwezi kupinga hiyo 2,000/= kwa unit na hata huduma za usimamizi wa mradi zitaboreshwa.
 
ndugu mteja namba zetu zinapatikana siku zote kwa saa 24. tafadhali wasiliana na huduma kwa wateja dawasco 0800110064
Uku ubungo maji ynamwagika sana. Mabomba yamepasuka kutokana na presha ya maji. Kingine imetokea michezo, watu wanatoboa bomba nyuma ya mita, ili wapate maji ya bure. Alafu hamfanyiii kazi tukitoa taarifa. Na kuna watu wa dawasco wanakula sana rushwa. Kwa nini zoezi la kupitia mabomba yaliyotøboka msiwashirikishe mabaroźi wa mitaa
 
Sisi wakazi wa Pugu tunashida kubwa ya maji hamja sambaza mabomba na wala hna dalili hizo je mnatuambiaje juu ya hili
 
Uku ubungo maji ynamwagika sana. Mabomba yamepasuka kutokana na presha ya maji. Kingine imetokea michezo, watu wanatoboa bomba nyuma ya mita, ili wapate maji ya bure. Alafu hamfanyiii kazi tukitoa taarifa. Na kuna watu wa dawasco wanakula sana rushwa. Kwa nini zoezi la kupitia mabomba yaliyotøboka msiwashirikishe mabaroźi wa mitaa
Yaani hana maoni mazuri hayazingatiwi, maswali hayajibiwi toka mwaka jana. Fungeni huu uzi wenu hauna faida.
 
Ndugu viongozi wa DAWASCO tunawaomba haya maji machafu yana tiririka zaid ya mwaka mmoja hv hamuon?au mnataka nini?
Kero hyo ipo mtaa wa omary londo na swahili lakin hapo ndio yanapo simamia na kusababisha kero kwa wapita njia na watu wenye shughuli zao, tunaomba tujue kwa nn haiwezekani kutatuliwa tatizo hilo limekua sugu..
 
DAWASCO kama mmeamua kufanya kazi kwenye mitandao mumuajili mtu special humu wa kujibu kero za watu
Wenzenu Tanesco kitengo kama hiki humu humu jf anafanya kazi kweli kweli
Na kazi yake inaonekana
Ukitoa leo malalamiko yako kesho asubuhi unapigiwa hodi faster
Tanesco wako vizuri sana tena kwa kuongezea wao wanaongea na wateja nchi nzima.
 
Mm nipo bunju A usalama
Mtandao wa maji umeishia pale kwenye kanisa la EFATHA, yaani bomba kubwa
Kutoka pale kanisani mbaka nyumbani kwangu ni umbali wa Mita kama 100
Ili nipate maji inahitajika niunganishiwe bomba kubwa kutoka pale EFATHA Kushuka bonde mbaka chini pale ni kama mita 50
alafu mm niunganishe tena hiyo mita 50 nyingine kwa bomba la kawaida dogo
Sasa Basi nilitaka kujua Coast yake endapo nitahitaji maji nyumbani kwangu yafike
au unanipa ushauri gani ? Kwa sababu huduma ya kuunganishiwa maji naitaka kweli kweli na pesa ninayo.
 
Gerezani mtaa wa Swahili na Omary londo kuna kero ya maji taka yanatiririka na harufu mbaya na hili tatizo linafika mwaka mzima na kila mnapokuja kwa nini mnashindwa kutatua tatizo ? Na sijaona mkija na njia mbadala zaidi ya ile bajaji na wale mafundi wenu wanne na fimbo za kuchokole kwa hili tatizo nahisi hata fimbo zenyewe haziwezi kutatua tatizo
Baya zaidi mtaani tuna Afisa mtendaji,Diwani,Mwenyekiti wa mtaa,Bibi afya wao kazi yao ni kukwaruzana na wafanyabiashara ndogo ndogo na si kushikilia jambo hili liondoke.
Natoa rai kwa viongozi wa juu wa serikali kwanza hao nilowataja hapo juu hawaendani na kasi ya mkuu na nyinyi DAWASCO mna nini mpaka mshindwe kutatua tatizo hili
 
Gerezani mtaa wa Swahili na Omary londo kuna kero ya maji taka yanatiririka na harufu mbaya na hili tatizo linafika mwaka mzima na kila mnapokuja kwa nini mnashindwa kutatua tatizo ? Na sijaona mkija na njia mbadala zaidi ya ile bajaji na wale mafundi wenu wanne na fimbo za kuchokole kwa hili tatizo nahisi hata fimbo zenyewe haziwezi kutatua tatizo
Baya zaidi mtaani tuna Afisa mtendaji,Diwani,Mwenyekiti wa mtaa,Bibi afya wao kazi yao ni kukwaruzana na wafanyabiashara ndogo ndogo na si kushikilia jambo hili liondoke.
Natoa rai kwa viongozi wa juu wa serikali kwanza hao nilowataja hapo juu hawaendani na kasi ya mkuu na nyinyi DAWASCO mna nini mpaka mshindwe kutatua tatizo hili

Dawasco watu wa Manzese na Tandale hakuna maji wiki nzima na hamtoi taarifa yoyote kama ni matengenezo ya barabara kwa nini maji yasifunguliwe hata kama mgao kwa masaa kuwepo na level ya tatizo 6, 12 au masaa 24 kukata maji kwa siku 7x 24 ni hujuma kwa wananchi kwani tuko Capetown ? Hapa kazi bila maji na hivyo viwanda ni ndoto ya mchana. Mkurugenzi wa Dawasco toka mafichoni ueleze tatizo ni nini na litakwisha lini. Huku kubebana hakuna maana! Weka basi hata ratiba saa utapata wapi mapato kama maji hayauzwi. Kama 40% - 6% ni upotevu tutafika kweli?
 
Mbona bomba la kijiji ntyuka-Dodoma kama unaelekea dampo tangia muweke halijawahi kutoa maji? Au mliweka ' bortion' !!!
 
kwanza nawapa pongezi kwa Kazi nzuri mlioifanya ya kutandaza mabomba ktk maeneo mbali mbali ya DSM na Pwani,
nataka kujua taratibu ili niweze kuunganishwa kupata Huduma ya maji nyumbani, maana tangu mradi huo ukamilike mwaka jana hadi leo sioni kinacho endelea wala sijaona dawasco wakitoa taarifa
 
MBONA HUKU TABATA KISUKURU ENEO LA KILIMANJARO BAR KUNA TATIZO LA MUDA MREFU LA MAJI LAKINI HAKUNA SULUHISHO LICHA YA SISI WAKAZI KUTOA MALALAMIKO DAWASCO TABATA KILA MARA? MAJI YANATOKA MARA MOJA KWA MWEZI NA KILA TUNAPOWASILIANA NA WAHUSIKA BW. MAKELELE, BWANA PASCO NA INJINIA WAO JIBU NI LILE LILE KILA SIKU "KUNA MATENGENEZO KIMARA". KWA VILE SUALA HILI NI LA MUDA MREFU TUNATUMIA NJIA HII KWA SASA NA IKISHINDIKANA TUNAOMBA KWA RIDHAA YENU DAWASCO ILI TUUSHIRIKISHE UONGOZI WA MKOA TUPATIWE UFUMBUZI WA KUDUMU
 
Back
Top Bottom