Dawa ya Kuvuta Wateja kwenye Biashara Mpya

Dawa ya Kuvuta Wateja kwenye Biashara Mpya

SamuraiJack

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2017
Posts
461
Reaction score
703
Habari wakuu. Nimekuja leo nikiwa na maswali mawili kuhusu biashara yangu mpya ya restaurant/mkahawa.


Swali la kwanza linahusu biashara yenyewe. Nimefungua restaurant wiki mbili zilizopita baada ya kuwahi kufanya biashara kama hii miaka kadhaa nyuma lakini sikufanikiwa sana. Safari hii nimerudi nikiwa na mtaji mkubwa, plan nzuri, usafi, na nidhamu ya biashara. Eneo nililopo lipo barabarani na kuna movement ya watu hasa asubuhi, mchana na usiku lakini bado faida na mauzo sio mazuri kama nilivyotarajia. Kwa sasa naisimamia mwenyewe muda wote kabla ya kuja kuweka meneja na pia nina mpango wa kufunga CCTV jikoni na maeneo ya mbele ili kudhibiti wizi, matumizi mabaya ya bidhaa, na kuongeza usimamizi wa kazi. Changamoto kubwa ninayoiona ni upande wa chipsi. Naomba msaada kwa wenye uzoefu, kilo 1 ya viazi inatakiwa kutoa sahani ngapi za chips kwa portion ya kawaida ya mjini? Nahisi huenda portion zangu ni kubwa sana ndio maana faida inakuwa ndogo. Ushauri wowote wa kuongeza faida na kuimarisha restaurant unakaribishwa.


Swali la pili linahusu kuvuta wateja. Naomba kujua ni vitu gani hasa vinafanya restaurant mpya kuvuta na kuhifadhi wateja wengi. Ukiachana na location, huduma, usafi, bei, matangazo, ubora wa chakula, maombi ya kuombea biashara, kwa maana haya yote nayafanya kwa asilimia 90-95%, au kuna mambo mengine muhimu zaidi? Pia kama kuna watu wanaoamini katika “dawa ya biashara” kuvuta wateja, naomba mnishauri kwa hekima na uzoefu wenu. Niko tayari kujifunza na kuboresha biashara yangu.
 
Consistency tu mkuu,
1)hakikisha wateja wako hawakosi huduma Bora ya chukula Kila siku wawe na uhakika wa kupata chakula kwako,

2)Gharama za chakula ziwe affordable usitake kurudisha mtaji haraka kwa kukandamiza wateja.

3)Usafi wa mazingira haitoshi ila wahudumu wawe wanavutia na wachangamfu

Mwisho: chakula ni ibada kwa biashara ndogo kama hiyo kuwaza ulozi,dawa ni mapema sana mkuu acha mawazo hayo.
 
Habari wakuu. Nimekuja leo nikiwa na maswali mawili kuhusu biashara yangu mpya ya restaurant/mkahawa.


Swali la kwanza linahusu biashara yenyewe. Nimefungua restaurant wiki mbili zilizopita baada ya kuwahi kufanya biashara kama hii miaka kadhaa nyuma lakini sikufanikiwa sana. Safari hii nimerudi nikiwa na mtaji mkubwa, plan nzuri, usafi, na nidhamu ya biashara. Eneo nililopo lipo barabarani na kuna movement ya watu hasa asubuhi, mchana na usiku lakini bado faida na mauzo sio mazuri kama nilivyotarajia. Kwa sasa naisimamia mwenyewe muda wote kabla ya kuja kuweka meneja na pia nina mpango wa kufunga CCTV jikoni na maeneo ya mbele ili kudhibiti wizi, matumizi mabaya ya bidhaa, na kuongeza usimamizi wa kazi. Changamoto kubwa ninayoiona ni upande wa chipsi. Naomba msaada kwa wenye uzoefu, kilo 1 ya viazi inatakiwa kutoa sahani ngapi za chips kwa portion ya kawaida ya mjini? Nahisi huenda portion zangu ni kubwa sana ndio maana faida inakuwa ndogo. Ushauri wowote wa kuongeza faida na kuimarisha restaurant unakaribishwa.


Swali la pili linahusu kuvuta wateja. Naomba kujua ni vitu gani hasa vinafanya restaurant mpya kuvuta na kuhifadhi wateja wengi. Ukiachana na location, huduma, usafi, bei, matangazo, ubora wa chakula, maombi ya kuombea biashara, kwa maana haya yote nayafanya kwa asilimia 90-95%, au kuna mambo mengine muhimu zaidi? Pia kama kuna watu wanaoamini katika “dawa ya biashara” kuvuta wateja, naomba mnishauri kwa hekima na uzoefu wenu. Niko tayari kujifunza na kuboresha biashara yangu.
Maji ya kwa Mwamposa.

NB: Dawa za Kishirikina zitakuingiza kwenye utumwa wa huko.
 
Habari wakuu. Nimekuja leo nikiwa na maswali mawili kuhusu biashara yangu mpya ya restaurant/mkahawa.


Swali la kwanza linahusu biashara yenyewe. Nimefungua restaurant wiki mbili zilizopita baada ya kuwahi kufanya biashara kama hii miaka kadhaa nyuma lakini sikufanikiwa sana. Safari hii nimerudi nikiwa na mtaji mkubwa, plan nzuri, usafi, na nidhamu ya biashara. Eneo nililopo lipo barabarani na kuna movement ya watu hasa asubuhi, mchana na usiku lakini bado faida na mauzo sio mazuri kama nilivyotarajia. Kwa sasa naisimamia mwenyewe muda wote kabla ya kuja kuweka meneja na pia nina mpango wa kufunga CCTV jikoni na maeneo ya mbele ili kudhibiti wizi, matumizi mabaya ya bidhaa, na kuongeza usimamizi wa kazi. Changamoto kubwa ninayoiona ni upande wa chipsi. Naomba msaada kwa wenye uzoefu, kilo 1 ya viazi inatakiwa kutoa sahani ngapi za chips kwa portion ya kawaida ya mjini? Nahisi huenda portion zangu ni kubwa sana ndio maana faida inakuwa ndogo. Ushauri wowote wa kuongeza faida na kuimarisha restaurant unakaribishwa.


Swali la pili linahusu kuvuta wateja. Naomba kujua ni vitu gani hasa vinafanya restaurant mpya kuvuta na kuhifadhi wateja wengi. Ukiachana na location, huduma, usafi, bei, matangazo, ubora wa chakula, maombi ya kuombea biashara, kwa maana haya yote nayafanya kwa asilimia 90-95%, au kuna mambo mengine muhimu zaidi? Pia kama kuna watu wanaoamini katika “dawa ya biashara” kuvuta wateja, naomba mnishauri kwa hekima na uzoefu wenu. Niko tayari kujifunza na kuboresha biashara yangu.
Hongera sana, Hakuna dawa, dawa zote umezifanya tayari, ubora wa huduma, nidhamu na Mungu wa Mbinguni. Next, jipe muda, biashara zinapitia vipindi kama ukuaji wa mtoto, just jipe muda na MAINTAIN.
 
Consistency tu mkuu,
1)hakikisha wateja wako hawakosi huduma Bora ya chukula Kila siku wawe na uhakika wa kupata chakula kwako,

2)Gharama za chakula ziwe affordable usitake kurudisha mtaji haraka kwa kukandamiza wateja.

3)Usafi wa mazingira haitoshi ila wahudumu wawe wanavutia na wachangamfu

Mwisho: chakula ni ibada kwa biashara ndogo kama hiyo kuwaza ulozi,dawa ni mapema sana mkuu acha mawazo hayo.
Asante sana mkuu, ibada ninafanya ndio....nitachukua hiyo point ya consistency na wahudumu kuwa wachangamfu kwa wateja...
 
Kwanza unatakiwa uajiri wafanyakazi wanayoielewa biashara,wenye lugha nzuri, jitahidi kupika chakula kizuri,jitahidi pia kuongeza kipimo cha chakula, hii itakufanya upate faida kidogo ila mzunguko mkubwa wa biashara. Nikukumbushe tu,hakuna mtu hapa duniani aliyefanikiwa bila kuhusisha nguvu za waganga na dawa! Sisemi kuwa uache maombi ya kuiombea biashara yako,la yakupasa utembelee kwa wataalamu pia. Kila la kheri ndugu.
 
Consistency tu mkuu,
1)hakikisha wateja wako hawakosi huduma Bora ya chukula Kila siku wawe na uhakika wa kupata chakula kwako,

2)Gharama za chakula ziwe affordable usitake kurudisha mtaji haraka kwa kukandamiza wateja.

3)Usafi wa mazingira haitoshi ila wahudumu wawe wanavutia na wachangamfu

Mwisho: chakula ni ibada kwa biashara ndogo kama hiyo kuwaza ulozi,dawa ni mapema sana mkuu acha mawazo hayo.
Fata huu ushauri

Consistency is everything.
Na kuwa na chakula kizuri plus good customer care .

Hayo mambo ya madawa na uchawi ni kupoteza muda wako na fedha
 
Hongera sana, Hakuna dawa, dawa zote umezifanya tayari, ubora wa huduma, nidhamu na Mungu wa Mbinguni. Next, jipe muda, biashara zinapitia vipindi kama ukuaji wa mtoto, just jipe muda na MAINTAIN.
Asante mkuu.....nitajitahidi kumaintain na kuwa consistency....japo kwenye hii biashara yangu nimejipa siku moja ya mapumziko ( hii ni kwa ajili ya work life balance kwa upande wangu mimi na staff) je hairaathiri biashara au wateja watazoea with time?
 
Kwanza unatakiwa uajiri wafanyakazi wanayoielewa biashara,wenye lugha nzuri, jitahidi kupika chakula kizuri,jitahidi pia kuongeza kipimo cha chakula, hii itakufanya upate faida kidogo ila mzunguko mkubwa wa biashara. Nikukumbushe tu,hakuna mtu hapa duniani aliyefanikiwa bila kuhusisha nguvu za waganga na dawa! Sisemi kuwa uache maombi ya kuiombea biashara yako,la yakupasa utembelee kwa wataalamu pia. Kila la kheri ndugu.
Asante mkuu, hii nikikuwa naitafuta!
 
Asante mkuu.....nitajitahidi kumaintain na kuwa consistency....japo kwenye hii biashara yangu nimejipa siku moja ya mapumziko ( hii ni kwa ajili ya work life balance kwa upande wangu mimi na staff) je hairaathiri biashara au wateja watazoea with time?
Hilo ni sawa kabisa, nalo maintain, siku isibadilike badilike, wata comply ! Si unaona huko mijini tunakaa nje ya maduka ya wahindi tukisubiri wamalize ibada between 1 & 2 pm ? Hatujawahi kuwakimbia ! Tunajua tunachokitaka kipo ndani.
 
Hilo ni sawa kabisa, nalo maintain, siku isibadilike badilike, wata comply ! Si unaona huko mijini tunakaa nje ya maduka ya wahindi tukisubiri wamalize ibada between 1 & 2 pm ? Hatujawahi kuwakimbia ! Tunajua tunachokitaka kipo ndani.
Naam hakika, nitaifanyia kazi hii.
 
Kwa uzoefu wangu , biashara inaanzaga taratibu sana .

Haijalishi una offer good service or not.

Aliyesema consistency ndo kakupa ushauri mzuri.

Kwakuwa ukimuhudumia Mteja Mmoja vizuri atamleta mwenzake.

Sifikirii kama Kuna dawa ya uhakika ya kukupa wateja kama ipo mbona mama ntilie wanaopika mtaani wanatumia ila hatuoni growth yao .

Means kama huduma mbovu na hauna consistency means nothing can exit.
 
Kwa uzoefu wangu , biashara inaanzaga taratibu sana .

Haijalishi una offer good service or not.

Aliyesema consistency ndo kakupa ushauri mzuri.

Kwakuwa ukimuhudumia Mteja Mmoja vizuri atamleta mwenzake.

Sifikirii kama Kuna dawa ya uhakika ya kukupa wateja kama ipo mbona mama ntilie wanaopika mtaani wanatumia ila hatuoni growth yao .

Means kama huduma mbovu na hauna consistency means nothing can exit.
I conquer with you! Ni kweli mama ntilie wengi utasikia wanatumia dawa, but miaka nenda rudi utamkuta palepale kwenye kakibanda chake with less capital growth or expansion...au ndo masharti yenyewe 😁😎
 
I conquer with you! Ni kweli mama ntilie wengi utasikia wanatumia dawa, but miaka nenda rudi utamkuta palepale kwenye kakibanda chake with less capital growth or expansion...au ndo masharti yenyewe 😁😎
Pia watu wako , ule muda wa lunch , wanakuwa wanatembelea kuchukua oda then wanakuja Wana deliver.

Kuna wateja wao kutokana na majukumu yao hawezi akafunga duka ili aje kula katika mgahawa wako

Ila kama ukampelekea anakula

Means watu wako watumie mbinu hii kipindi biashara inaanza Anza.
 
Asante mkuu, hii nikikuwa naitafuta!
chukua ushauri wote ila nakuapia pia ukiacha kwenda kwa waganga na wataalamu utashtuka tu biashara imedoda. Mjini ndipo kuna uchawi zaidi kuliko popote,unaweza ukawa na mwendelezo,sijui customer care,usafi,huduma nzuri lakini wateja wakakuhama na unakuwa unapata hasara kila siku,ndugu kama unataka ufanikiwe katika biashara yako tembelea kwa wataalamu,kama unahtaji tu mtaji wa kujishikiza na showoff kwamba na wewe una mgahawa basi usichoke kupiga maombi. MAFANIKIO HAYAJI KWA KUKATA TAMAA.
 
Mkazo uwe kwenye huduma bora, staff wenye bashasha ila wasiwe mapepe.

Baki njia kuu kwa kutoa hudumu iliyo nyooka.
Usibadilishe bei ya chakula hovyo hovyo.
Treat you customers with equal value.
Staff anae enenda nje ya mstari mpe karipio kali kimiakimia akirudia fukuza chap.

Usafi wa chakula, mazingira na mavazi.
Usibadilishe wapishi pasipo na ulazima.

Maintain hospitality na epuka usumbufu kwa wateja kama kauri za "chenchi hamna, acha hela utakuja kuchukua baadae" hayo ni mambo ya kiswahili.

Achana na ndumba.
 
Pia watu wako , ule muda wa lunch , wanakuwa wanatembelea kuchukua oda then wanakuja Wana deliver.

Kuna wateja wao kutokana na majukumu yao hawezi akafunga duka ili aje kula katika mgahawa wako

Ila kama ukampelekea anakula

Means watu wako watumie mbinu hii kipindi biashara inaanza Anza.
Sawa hili nimeliona nafikiria niajiri kijana wa kuwa anapeleka delivery na kuomba oda za chips specifically.
 
Back
Top Bottom