David Kafulila,na Serikali Tatu

David Kafulila,na Serikali Tatu

Ngoja nikusaidie
Mwaka 1992 Maccm mlizunguka Tanzania yote kupiga propaganda kuwa vyama vingi vitaleta vita!
Sasa chama gani kilicholeta vita?-Kafulila
Siasa za CDM zingechekewa na wangeshinda uchaguzi mkuu, wangeipelekea nchi matatizo tayari, sera za majimbo ni matatizo makubwa, siasa zao kuchongea na maandamano ni hatari, hivi ulijifunza nini na sakata la uchinjaji lilioanzia mwanza na kwenda kufanya watu watandikane mapanga Tunduma. Trust me tungeenda kwenye majmbo ingekuwa hatari you can see why there is the danger of multi party democracy in the third world in general, kwa sababu vyama vya siasa vikizidiwa huwa vinatumia kundi fulani kutokana na kabila, dini, regions to demand changes that is danger thanks god Lema kafanikiwa Arusha mjini tu, lakini siasa zake zingekuwa nationally ni hatari (well hilo linataka topic nyengine).

Propaganda zilezile za 1992 leo mnazirudia kwa style nyengine kuwa seikali 3 zitavunja Muungano-Kafulila
Watu hawajiamki asubuhi na kujianzia waungane tu bila ya sababu, huko nyuma baada ya kutandikana sana watu kwa kuogopa kuvamiwa mmoja mmoja ni bora waungane na serikali za majimbo ili wasaidiane kumshinda common enemy, vile vile ukubwa wa eneo la nchi ndio maana kuna kuwa na serikari nyingi hili local people waweze kuwa served locally.

Kwenye mahala watu walipoona sisi tulikuwa wamoja au tuna historia moja wengi walipenda kurudi kama historia yao, sisi tumetokea hapo na swala hili lilifanywa mara baada ya mapinduzi ya ZnZ, leo tena tuvunje muungano huko ni kuwapa ushindi watu wanaong'an'gana na historia mbaya ya utumwa as 'Salmini Amour' referred to them Manyan'gau's.

Serikali tatu ndio lenye lengo hilo kuturudisha nyuma, huyo kafulila akachungulie Kigoma kila kukicha uhamiaji inakamata raia wakirundi kwenye mashamba huko wakifanya kazi illegally without the right papers if he is so concerned na nchi yake.

Serikari mbili sio propaganda, serikali tatu ndio propaganda you cant call propaganda on what already exists, propaganda is what you want to make people believe is right for them kama wanafiki wa serikali tatu (kitu ambacho hatujawahi kuwa nacho), kwa hivyo kusema serikari tatu zinaweza vunja muungano that is a real outcome.

Si kuna proponents pia wa serikari tatu wanaosema wazi muungano uvunjwe na zanzibar ipewe mamlaka kamili. Well if you accumulate thoughts of these people plus the three tier government proposed hakuna mwenye akili timamu atakae taka kutupa hela kuendesha serikali ya tatu by virtue of common sense huko ni kutaka kuuvunja muungano in the long run.

Besides mapendekezo ya tatu, ambayo ndio serikali kuu aina nguvu kama nchi zake inazotakiwa kuziongoza ina mabavu tu kwa sababu ina majeshi lakini aina power to influence policies za nchi ,bili ambazo si maswala ya muungano, sasa Zanzibar ikisema inataka kufanya biashara na Rwanda ya madini, wakati tunajua rwanda hawana madini, where are the limitations of governments free will,.

Hiwapo Tanzania bara inataka kwenda SADC na EAC halafu ZnZ ikaamua kwenda kwenye umoja wa visiwa na nchi za kiislamu au muungano mwengine wa kimataifa, ni hivi there are no clear autonomous limitations which could lead to countries making allies who do not see eye to eye with the other union state, there are many things i can think of ambapo jaji warioba hakuzingatia ambayo yataenda leta sinto-kufahamu huko mbele.
 
moja ya mambo aliyosema ni kwamba watu 17 elfu walipendekeza serikali tatu katika tume ya warioba, je bunge la watu 600 wana uwingi gani wakukataa maoni ya watu elfu 17?

Halafu wajihalalishie kuwa wale elfu 17 ni wachache ila wao 600 ni wengi. Kuna vichwa mle ndani vinahitaji kupimwa kama viko sawa. Ila huu mtiririko wa hoja za wachache Tanganyika inanukia kama pilau lililo jikoni.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Kwa kweli, hata mimi nimemwelewa vizuri. Amejieleza kiufasaha sana. Natumaini Kamati nyingine zijitahidi kuwapa watu wa jinsi hii nafasi kuwatetea wachache. Hapa mwananchi wa kawaida ameelewa na hata wzle wenye mioyo migumu kushtuka kiasi fulani.
Ambaye hajaelewa au kukubaliana na hoja za Kafulila, ni adui wa mustakabali mwema kwa Taifa.
 


Mr. Kafulila vs Prof. Shivji

Naomba tufanye rating ya hao, maximum point ni 10
 
dont panic mkuu!!hujitambui sikun ukijielewa huta kuja kuonyesha jinsi gani ulivyo mjinga

Mkuu, huyu happy feet amesau kuwa ukweli humuweka mtu huru. Yeye ameamua kutetea kitu tofauti na dhamira yake, ataishia kuwa mtumwa.
Ukisikiliza baadhi ya wabunge wanavyochangia unajua kabisa maneno yao yanapingana na dhamira zao. Watu wa jinsi hii watatesa ktk maisha yao yote, sawa na mwanamke aliyezaa mtoto na kumtupa chooni.
 
kwanza ameongea kwa lugha ya heshima ya hali ya juu
hoja kwa hoja na kwa takwimu na ameohoji wale wanaomdhihaki jaji Warioba utadhani katika tume yote yaliyoandikwa ni mawazo ya warioba kumbe ni mawazo ya wale walio hojiwa
 
dont panic mkuu!!hujitambui sikun ukijielewa huta kuja kuonyesha jinsi gani ulivyo mjinga
Mimi ni Mtanzania wa kuzaliwa mama Mdengereko na Baba Muhehe, naambiwa wahehe ni wandereko waliosogea zamani. Naamini na Wazanzibar ni watanzania walio chukuliwa na utumwa zamani na kuna walio amia wenyewe hila aliondoi asili yao napigania muungano wa watu wamoja.

Wewe je unajitambua?
 
Ofisi ya rais ilipendekeza serikal 3, ofis ya w/mkuu serikal 3, ofis ya m/rais selikali 3, baraza la wawakilishi serikal 3, hapa nan mnafiki jk au warioba? hongera sana prof. kafulila umetisha, umeweka mambo sawa wanafiki historia itawahukumu.
 
Namsubiri mchungaji Mtikila kwa hamu sana.

Tatizo la Mtikila ni kuwa anaweza kuwa na hoja ila ana jazba na atatukana hivyo Wajumbe wale wa CCM ndio kitu wanataka ili waanze kuzomea na kutaka mwongozo ili kuharibu mada. Njia sahihi kwa sasa ni kuwapa za uso huku umetulia wasikilizie maumivu moyoni pekee maana huko akilini ni box tupu.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Achana nae huyo,atatuharibia siku ya leo.Hana lolote zaidi ya kusema ovyo.
 
"Mapenzi yakizidi ni upofu"
Inaonekana akili unayo lakini umeruhusu akili yako kwenda likizo ili utetee hoja dhaifu ya CCM
Mnaweza mkazipata hizo selikali mbili kwa kutumia wingi wenu lakini mjue kuwa ipo siku Tanganyika itarudi
Sasa sijui nani ni kipofu kati ya mimi na wewe, hivi kutetea serikari mbili ni kutetea CCM. Kweli CDM wamewachukua na akili nyie watu, hivi wewe kwanini unaitaka Tanganyika? wewe kama wewe na si kwa akili za kuambiwa.
 
Kuna Maprof wengine watattu jana waliwakilisha rasimu yao,nilicheka hadi mbavu zikauma nilipowaona wakikabidhi ilo likitabu lao,kweli nchi hii ina usanii na wasanii wa aina nyingi.

Waspmi wetu hawatutendei haki katu!
 
Mkuu, huyu happy feet amesau kuwa ukweli humuweka mtu huru. Yeye ameamua kutetea kitu tofauti na dhamira yake, ataishia kuwa mtumwa.
Ukisikiliza baadhi ya wabunge wanavyochangia unajua kabisa maneno yao yanapingana na dhamira zao. Watu wa jinsi hii watatesa ktk maisha yao yote, sawa na mwanamke aliyezaa mtoto na kumtupa chooni.
Utumwa ni kulilia mkoloni na mambo yake kuanzia majina aliyo tuachia kama tanganyika na siasa za CUF na Jamsheed wao. Mimi ni mwafrikna na proud of being one na ntapigania chochote chenye kulinda hadhi yetu including umoja wetu.

Mtumwa ni yule anaejitambulisha kinyume na hapo na kuona mambo anayofanya mwafrika na jitihada za kujikomboa hazina maana.
 
Ofisi ya rais ilipendekeza serikal 3, ofis ya w/mkuu serikal 3, ofis ya m/rais selikali 3, baraza la wawakilishi serikal 3, hapa nan mnafiki jk au warioba? hongera sana prof. kafulila umetisha, umeweka mambo sawa wanafiki historia itawahukumu.

Angemtaja tuu kuwa kati ya JK na Warioba nani ni Hypocrite kuliko kutumia neno mnafiki kupunguza makali. Hawa jamaa tafsiri zao za kiingereza huwa wanajichanganya sana. Nakumbuka wakati Wenje aliposema serikali hii ni impotence kuna waziri akang'aka kuwa Wenje kamaanisha hii ni serikali -------! Kwa hiyo hawa ni kuwa changanya kwa maneno.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Back
Top Bottom