David Kafulila,na Serikali Tatu

David Kafulila,na Serikali Tatu

Nimevutiwa na jinsi Mbuge Huyu alivyo weza kujieleza na kutetea Serikali Tatu kwenye Bunge Maaluma La Katiba,ameeleza kwa ufasaha na nguvu za hoja kiasi kwa waliosikiliza/kuangalia live.
Ametetea Serikali Tatu na Kumpongeza Jaji Mstaafu Joseph Warioba kwa kazi aliyoifanya na Tume yake,na kuwabeza wanaoipinga Tume ya Warioba.

Jamaa ameongea kisomi na kwa hoja zenye nguvu na nilikuwa sijui kuwa ofisi ya Rais nayo ilipendekeza serikali 3
 
Nimefurahishwa mno na hotuba ya Kafulila. Kama ningekuwa naandika kichwa cha habari cha gazeti saa hizi, kichwa cha habari hiyo kingekuwa "KAFULILA AMFUNIKA JK". Kaongea maneno ya kujenga kuliko maneno ya JK ya kutishia watu kuwa eti serikali tatu zitapinduliwa na jeshi!
 
nimevutiwa na jinsi mbuge huyu alivyo weza kujieleza na kutetea serikali tatu kwenye bunge maaluma la katiba,ameeleza kwa ufasaha na nguvu za hoja kiasi kwa waliosikiliza/kuangalia live.
Ametetea serikali tatu na kumpongeza jaji mstaafu joseph warioba kwa kazi aliyoifanya na tume yake,na kuwabeza wanaoipinga tume ya warioba.

kwa kweli huyu jamaa yuko njema sana.
 
kafulila amefunika sana leo, ameuliza kuwa kuna uhalali gani wa watu mia sita ( wajumbe wa bunge maalumu la katiba) kuona watu elfu kumi na saba waliosupport serikali tatu ni wachache, tatizo wajumbe wengi wanaounga mkono serikali mbili hawana hoja na nimeanza kuamini kuwa siku zote kutetea uongo ni kazi sana. nakuhitaji Tanganyika.
 
Hata mimi nimempa big up, anajua kujenga hoja nzuri sana...
 
Hakika ametuwakilisha vyema ingawa dakika zake zimepunguzwa kiaina,amotoa hoja ambazo anayetaka kuzipiku basi aziweke hadharani mpaka tujisikie kutokwa na machozi kama alivyofanya Kafulira.Hongera sana kijana.Wakipatikana mia kama huyo mambo yataenda sawa.
 
kafulila amefunika sana leo, ameuliza kuwa kuna uhalali gani wa watu mia sita ( wajumbe wa bunge maalumu la katiba) kuona watu elfu kumi na saba waliosupport serikali tatu ni wachache, tatizo wajumbe wengi wanaounga mkono serikali mbili hawana hoja na nimeanza kuamini kuwa siku zote kutetea uongo ni kazi sana. nakuhitaji Tanganyika.

Kichwa kama cha Mwigulu, Mrema, profesa Mwandosya vina hoja gani zaidi ya kufuata mkumbo tu
 
kafulila amewakilisha kundi la watanganyika vizuri sana. Hongera sana kijana mdogo uliyeweza kuwaziba midomo ma pf fake (@kapuya, maghembe na wenzao)
Kuna Maprof wengine watattu jana waliwakilisha rasimu yao,nilicheka hadi mbavu zikauma nilipowaona wakikabidhi ilo likitabu lao,kweli nchi hii ina usanii na wasanii wa aina nyingi.
 
Nilijihisi kulia ujue afu nikajistukia nimajisemea i'm a man...hamna kulia lia..ila kanikosha asee!!
 
hakika amejenga hoja, labda tu kwa wale ambao hawakupata nafasi ya kufuatilia niwape baadhi ya hoja alizojenga
1: kama kuna watu (ccm) ambao wanadai maoni ya watu 17000 juu ya kuwa na serikali 3 ni idadi ndogo sana ambayoyo haiakisi matakwa ya watanzania 46ml, je hawa wabunge 600 wanapata wapi nguvu ya kuwa na uwakilishi wa wananchi ili hali wao ni wachache zaidi kuliko hata hao waliotoa maoni juu ya kuwa na serikali 3?
2: Amehoji kama ishu ni kumtii mwl nyere ambae hakuta kuvunjika kwa muungano,wamesahau kuwa mwl alikuwa anabadilika kulingana na wakati. Mf mwaka 1965 mwl alifuta vyama vingivlakini kulingana na mabadiliko yaliyohitaji mageuzi mwaka 1992 ni mwl uyohuyo aliweze kuwa na vyama vingi ambavyo alivifuta hapo mwanzo. Akauliza je mwl angekufa kabla ya kuanzishwa vyama vingi inamaana mpaka sasa kungekuwa na chama kimoja tu?
3: Viongozi waliopo madarakani leo wafanikishe kuwa na muungano mzuri zaidi wa serikali 3 kwakuwa hii nafasi walionayo hawatakuwa nayo tena miaka ijayo kwani ni dhahir wingi wao (ccm) utapungua hivyo watalazimika kukubali mabadiliko kwa shinikizo kubwa kitu ambacho kitazalisha muundo mbovu zaidi . Hili alitoa kama ushauri kwa viongozi waliopo madarakani kutumia hii nafasi kufanya mabadiliko mazuri tena kwa busara kuliko kusubiri presha hapo baadae.
4: Kama ishu ni mapato ya serikali ya muungano,amependekeza mapato yatokanayo na customs yote yawe ya muungano. Akafafanua kuwa zipo hoja kuwa kuna wanaodai ikiwa hivyo bara(tanganyika) italipa zaidi,akasema hilo sio shida kwani matumizi makubwa ya hiyo fedha yataelekezwavbara pia kwenye maeneo kama ya magereza,ulinzi,uhamiaji,polis nk. Akauliza wanaodai kuwa hili likitekelezwa watu wa bara watabeba huo mzigo,je kwa sasa ni kinani wanabeba huo mzigo?
5: Akaeleza kuwa tafiti zinaonesha kuwa muungano upo kwenye maeneo matatu ambayo ni ; serikali moja, serikali ya shirikisho na ile ya mkataba. Sasa hii yetu ni ya mfumo gani mbona haieleweke inafiti mfumo gani?
6: Akauliza kuwa kwakuwa muungano huu uliopo kwa sasa umedumu kwa takribani miaka 50, na umeshindwa kutatua changamoto zilizojitokeza kwa kipindi chote cha nusu karne, Je viongozi wanataka wapewe karne kangapi zaidi ili waweze kutatua hizi changamoto zilizopo?
7: Akafafanua zaidi kwa kusema wanaomhukumu jaji warioba wanamuonea. Akaeleza kuwa ukifanya tafiti na ukapata majibu kama ya wale walikutangulia kufanya tafiti maana yake ni kwamba hayo majibu ni sahihi. Sasa kwakuwa tume zilizomtangulia jaji warioba pamoja na wataalamu mbalimbali waliwahi kufanya tafiti juu ya muundo wa muungano na kuja na majibu ya serikali 3 inakuwaje leo wakatae hoja ya warioba ilihali inaendana na hoja za watangulizi wake kwenye jambo hilo?
8:Amehoji kama ofisi ya raisi,ya makamu wa raisi na ya waziri mkuu zote zilipendekeza serikali 3 inakuwaje tena ndani ya muda mfupi watu haohao wageuke na kudai serikali 2, au walitoa hayomaoni ili mwishowe waje wamdhalilishe jaji warioba?
9: Akaeleza kuwa yeye ni kijana mdogo lakini anamuheshimu sana jaj warioba. Akadai anashangazwa na watu wakawaida sana ( ambao ni wajumbe wa bunge la katiba - kwa mtizamo wangu lakini) ambao wanamdharau jaji warioba ilihali sio level yao kabisaa kwani jaji warioba yupo next level kabisa na anaheshimika ndani na nje ya nchi, hivyo inakuwaje watu wa kawaida sana wamtreat jaji warioba kwa kiwango cha chini sana ili hali yeye sio level yao?
10: Muundo wa serikali 3 ndio utakaotatua changamoto za sasa na zijazo,kuliko kufichaficha mambo kwa kisingizio cha serikali mbili kwani huko tuendako kutakuwa kigumu sana.
11: ....................nikikumbuka mengine nitayatupia hapa.....
 
Aisee kweli Kafulila katoa maelezo yanayokidhi kuwa na serikali 3 nadhani wale ambao walikuwa wanafuatilia leo bunge wameona
 
Nilijihisi kulia ujue afu nikajistukia nimajisemea i'm a man...hamna kulia lia..ila kanikosha asee!!

Tunaomba pls aliyerekodi hata kama ni audio atuwekee hapa ili nasi tuliokuwa mashambani na migodini nyakati hizo tuweze kusikia alichokisema mpendwa wetu David Kafulila!
 
Back
Top Bottom