David Kafulila,na Serikali Tatu

David Kafulila,na Serikali Tatu

Nimefurahishwa mno na hotuba ya Kafulila. Kama ningekuwa naandika kichwa cha habari cha gazeti saa hizi, kichwa cha habari hiyo kingekuwa "KAFULILA AMFUNIKA JK". Kaongea maneno ya kujenga kuliko maneno ya JK ya kutishia watu kuwa eti serikali tatu zitapinduliwa na jeshi!
Na wewe umemalizia kabisa, Duhhh.
 
hakika amejenga hoja, labda tu kwa wale ambao hawakupata nafasi ya kufuatilia niwape baadhi ya hoja alizojenga
1: kama kuna watu (ccm) ambao wanadai maoni ya watu 17000 juu ya kuwa na serikali 3 ni idadi ndogo sana ambayoyo haiakisi matakwa ya watanzania 46ml, je hawa wabunge 600 wanapata wapi nguvu ya kuwa na uwakilishi wa wananchi ili hali wao ni wachache zaidi kuliko hata hao waliotoa maoni juu ya kuwa na serikali 3?
2: Amehoji kama ishu ni kumtii mwl nyere ambae hakuta kuvunjika kwa muungano,wamesahau kuwa mwl alikuwa anabadilika kulingana na wakati. Mf mwaka 1965 mwl alifuta vyama vingivlakini kulingana na mabadiliko yaliyohitaji mageuzi mwaka 1992 ni mwl uyohuyo aliweze kuwa na vyama vingi ambavyo alivifuta hapo mwanzo. Akauliza je mwl angekufa kabla ya kuanzishwa vyama vingi inamaana mpaka sasa kungekuwa na chama kimoja tu?
3: Viongozi waliopo madarakani leo wafanikishe kuwa na muungano mzuri zaidi wa serikali 3 kwakuwa hii nafasi walionayo hawatakuwa nayo tena miaka ijayo kwani ni dhahir wingi wao (ccm) utapungua hivyo watalazimika kukubali mabadiliko kwa shinikizo kubwa kitu ambacho kitazalisha muundo mbovu zaidi . Hili alitoa kama ushauri kwa viongozi waliopo madarakani kutumia hii nafasi kufanya mabadiliko mazuri tena kwa busara kuliko kusubiri presha hapo baadae.
Yaani, Yaani, Yaani Nondo tupu. Kijana mtanganyika huyu. Mungu ambariki.
 
Basi ni vyema kwa ipo cku tanganyika itarudi tu
 
Hi mdau jamaa kanisababisha hata sijanywa kitu jamaa kapiga ikulu nice presentation maccm wamezimika gafula ,hawana hoja wa data zozote za why note serikali tatu...nawasilisha
 
Niliziona sura za Prof Muhongo, Wassira na Mwakyembe zikiwa zimetahayari jinsi kijana alivyokuwa akitiririka hoja zake bila jazba wala kusoma popote. Ina maana alikuwa anasema kitu anachokiamini. Hoja zilikuwa zimesimama hata hivyo vidampa wa CCM wasiojua chochote zaidi ya kufuata maagizo waliyopewa wakawa wakati mwingine wanaanza kuzomea. Ila kwa jinsi walivyoona sura za viongozi wao nao wakanywea.
Ushauri wangu kwa hao wachache watakaotoa maoni kwa kamati zilizobaki waondoe jazba na kuzungumza kwa utulivu ndio njia sahihi ya ku win hadhira na kuwanyima maccm nafasi ya kuchafua mjadala kwa kuomba miongozo na taarifa.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Nimevutiwa na jinsi Mbuge Huyu alivyo weza kujieleza na kutetea Serikali Tatu kwenye Bunge Maaluma La Katiba,ameeleza kwa ufasaha na nguvu za hoja kiasi kwa waliosikiliza/kuangalia live.
Ametetea Serikali Tatu na Kumpongeza Jaji Mstaafu Joseph Warioba kwa kazi aliyoifanya na Tume yake,na kuwabeza wanaoipinga Tume ya Warioba.

Hongera kwa mr Kafurira; I was moved by his arguments
sio kama hawa wanao tetea serikali mbili bila hoja
 
Sikutegemea jinsi dogo alivyoeleza mambo. Hoja baada ya nyingine bila kelele bila jaziba wala woga. mfano wa kuigwa na wajumbe wote wa katika hasa kundi la 201. Thanks kafulila you have made my day.
 
Nimemkubali mh.ni jembe
wanafiki na wenye akili za kuazima wanaumbuka
 
Namsubiri mchungaji Mtikila kwa hamu sana.
 
The guy is very concistence and smart.nimempenda sana.

Kafulila wewe nimiongoni mwa vijana wachache wanaojitambua. kuna watu wanaojifanya wanajua huku wakiwa hakui kama hawajui. mfano wabunge wote wabala kimsingi niwatanganyika lakini leo wanaukana utanganyika huu niusaliti tunaitaka tanganyika yetu
 
Muanzisha uzi at least ungeelezea alicho eleza kafulila sio wote tumefuatilia
 
Nimevutiwa na jinsi Mbuge Huyu alivyo weza kujieleza na kutetea Serikali Tatu kwenye Bunge Maaluma La Katiba,ameeleza kwa ufasaha na nguvu za hoja kiasi kwa waliosikiliza/kuangalia live.
Ametetea Serikali Tatu na Kumpongeza Jaji Mstaafu Joseph Warioba kwa kazi aliyoifanya na Tume yake,na kuwabeza wanaoipinga Tume ya Warioba.
Ndio walichobakiza tena wapinzani hawana lengine, kelele za serikali tatu tu kwa sasa.

Kila wakitia maguu vijijini na hadithi za ufisadi wanakuta wanaulizwa fine tunajua hupo lakini maji vipi? soko la mazao liko wapi? miundombinu hipo wapi? na mtatusaidia vipi?. Wanauma uma majibu hawana sera hawana, zaidi ya kutukana jitihada zinazo onekana.

Sasa wanakimbilia serikali tatu kwa sababu ni popular stand ndani ya JF, wasubiri uchaguzi ujao yetu macho badala ya kuwa concerned na what really their local constituents want wao unafiki tu kama kiongozi alietoa mapendekezo ya serikali tatu.

Huyo Sharif Hamad kapewa tamko moja tu tayari anaweweseka, wapemba watabaki bara, asubiri aone watavyopanga mstari uhamiaji kuomba visa, mnajianzia tu serikari tatu.
 
Tunaomba pls aliyerekodi hata kama ni audio atuwekee hapa ili nasi tuliokuwa mashambani na migodini nyakati hizo tuweze kusikia alichokisema mpendwa wetu David Kafulila!

Mkuu bahati mbaya sikulipata hilo wazo. Waliofanya hivyo wataweka mkuu usijali
 
Back
Top Bottom