Kafulila sio Lazima uwe Mbunge ni Muda sasa uje ujenge chama.Unakumbuka uliingia bungeni kwa NCCR bila hata kujenga Tofali kujenga chama.Sasa uje umsaidie Mbatia kujenga Chama kimekufa.Mwambie Mkosamali pia aje na sio kusubiri kipindi cha uchaguzi ndio mnaenda majimboni.
Hapo Uvinza hamna ofisi,jenga sasa!
Pia kazi zipo nyingi za kufanya hujazaliwa kuwa Mbunge.Mrema alifanya kazi kubwa sana kupambana lakini kakubali matokeo.
Mbona kwa mujibu wa Husna umepeleka matokeo ya vituo 366 badala ya 382?
Sio lazima wewe na mkeo muwe wabunge tunahitaji mawazo kutoka watu mbali mbali.Hongera kwa miaka mitano,karibu uraiani.