Darasa la saba aukwaa u-DC

Darasa la saba aukwaa u-DC

mapogolo unaijua katiba ya tz? Tusiwe tunachangia vitu tusivyo na uhakika navyo. Kuna taarifa kuzipata ni taabu hata katia? Ndo nyie kweli mtafanya mabadiliko yenye manufaa kwa watz? Katiba inasema uweze kusoma na kuandika kiingereza na kiswahili. Mbona kina lusinde,agripina,airo wamo humo,? Inaumiza sana kuona mtu ambaye ana access ya information hataki kuzitafuta. So painful!
 
Kwani STD 7 hawana haki ya kutuongoza jamani? mbona Hayati Kawawa ilikua mhhh, hao maprofessor wametutenda mbona yaani hata kutaja majina yao naona kinyaa
 
Hata wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa kujadili katiba mpya pale Nkrumah UDSM, Jenerali Ulimwengu alisema kuwa hayo ni mojawapo ya mapungufu ya nafasi hizo za kisiasa yaani ukuu wa wilaya/mkoa. "Kuna kuanzia Koplo hadi Jenerali, darasa la saba hadi phD holder. Hakuna specific job requirement for those posts.

Kifupi chake, hao nimakada wa ccm na wanapelekwa huko kuangalia maslahi ya chama chao. Hakuna kingine.
 
nafikiri hakuna ajuaye kazi ya mkuu wa wilaya yenye kupimika na kwa ajili hiyo kisomo siyo tatizo kwa CCM.
Kikubwa ni uwezo wa kusaidiana na Msimamizi wa Uchaguzi KUIBA kura na kuchakachua matokeo kiasi kwamba hata Mbunge wa upinzani ile kura aliyojipigia inapotea pia
 
kwanza sioni kabisaaa umuhimu wa uwepo wao labda kulinda maslahi ya ccm
 
Ubaguzi mwingine ni mbaya kuliko ukimwi.
Katiba ya nchi inamruhusu Rais kuteua viongozi bila ubaguzi.
 
mhe. kanyunyu una hakika na ulichokiandika? bw. maneno alikuwa mbunge wa jimbo la chalinze katika bunge lililopita na minimum qualification ya ubunge ni elimu ya kidato cha nne, ni vipi angeukwaa ubunge bila kuwa na elimu hiyo. kumbuka huyu aligombea na omary madega kwenye kura za maoni ndani ya ccm mwaka 2005 ambaye kwa vyovyote asingenyamaza angemlipua tu maneno kama kweli ni darasa la saba. bunge lililopita mbunge pekee aliyefahamika kutokuwa na elimu ya kidato cha nne ni samwel chitalilo aliyekuwa mbunge wa buchosa. wapiga kura walimfungulia kesi ya kudanganya kuhusu elimu yake lakini kwasababu ambazo hazijulikani kesi hiyo haikufanikiwa.
Kama hujui kitu ama ukae kimya au google katiba ya jamhuri wa muongano Tanzania hala nenda kwenyekipengele husika ndiyo uje na ujinga wako....
 
nafikiri hakuna ajuaye kazi ya mkuu wa wilaya yenye kupimika na kwa ajili hiyo kisomo siyo tatizo kwa CCM.
Kikubwa ni uwezo wa kusaidiana na Msimamizi wa Uchaguzi KUIBA kura na kuchakachua matokeo kiasi kwamba hata Mbunge wa upinzani ile kura aliyojipigia inapotea pia
Hukuona kazi ya Mkuu wa wilaya kule Igunga, wanamchango mkubwa sana kwa serikali ya CCM...
 
mhhh. kazi kwelikweli, kama ni darasa la 7 kwelikweli atakuwa hata ung'eng'e haupandi! na ikitokea wakija wageni kutembelea wilaya yake kutoka ng'ambo atakuwa anawakimbia kama mshikaji wangu fulani ambaye ni mwenyekiti wa halmashauri na ni standard 7 lever anapatashida sana wakija wageni lazima atakula kona na kumwachia kazi makamu mwenyekiti wa halmashauri ambaye ni form 4 amsaidie kazi

kuna DC mmoja, yeye akipata ugeni wa wazungu au anaohisi kuwa wanajua ung'enge basi yeye hupiga MEDIA marufuku, i think hata huyu DC anaweza tumia hii strategy
 
Kuna aina ya watu wamepelekwa maeneo yanayoendana na elim zao na haiba zao,,,,hata ukiirudia list,,,,mfano mkuu wa wilaya ya NANYUMBU
Mkuu thats true,na nipo ofisi na jamaa angu mmoja hapa anasema huyu bwana anamjua tokea kitambo hapo Bagamoyo kuwa hana lolote na hana ujenzi wa hoja zaidi ya ubabe,ngoja tumcheki atakuja na kasi gani hapa Kigoma ila mwenzie Mongella ndio alikua anapga siasa sana hapa namna ya kuilinda hii ccm,nashukuru alikoenda Arusha watamtia adabu na ubabe wake huo.
 
Uwapige wenzio wakati na wewe uko kama wao?
Hebu ona ulivyovurunda: umeandika digree badala ya degree
enteview badala ya interview
anulizwa badala ya anaulizwa
Sasa wewe unajejidai una elimu hata ya kuweza kuwasaili wenzako unaweza nini hasa? Kiingereza ndio hivyo tena, hata Kiswahili? Sijui wapuuzi kama ninyi mtaisha lini nchi hii iweze kuendelea. Na usikute nyie ndio ma-HR au washauri wa Mkwerrrreee kwenye uteuzi wa ma-DC. Pambaf!
inawezekana ikawa kweli fanya utafiti ..hebu fikiria mtu yupo form one lakini hawezi kusoma na kuandika kwa ufasaha...hata wenye digree hawawezi kujieleza kwa mambo ya kawaida tu kwa kiingereza hii nimeiona mwenyewe kwenye michujo ya baadhi ya enteview kwa mfano mtu anulizwa umetoka wapi? kuja hapa anasema nimetoka mwanza swali lingine lina kuja hivi ............explain your journey from mwanza to dar
unatamani umpige

 
Ahhh mkuuu hapo umepote uliza tunaomjua maan alisoma hr ustawi wa jamii angewezeja kuwa pale bila hiyo elimu? na laikua afisa tra samora hebu fuatilia ujue bana, bahati ya mtu usiilalie mlango wazi kama zamu yake imefika acha na wao wale
 
Mkuu unashaanga Darasa la Saba kuteuliwa kuwa DC?Mbona ushangai Profesa kuchakuliwa kuwa Waziri asiyekuwa na wizara maalumu!
Ukishaa staajabu ya Mussa utayaona ya Firauni!

Prof. asiye na wizara, atafanyakazi kama consultant
 
kweli, jamaa anafahamika ni kilaza wa ukweli, hata wakati akiwa mjengoni haukuwa kuchangia chochote, hata kwenye zile kamati alikuwa hana mchango zaidi ya kusaini posho....ukuu wa wilaya unamfaa, coz anaoungea na wananchi wa kawaida, wenye matatizo madogo madogo... nimewahi kufanya intern ifis ya mkuu wa wilaya ya kinondoni, enzi hizo chini ya Kanal Massawe, haukuna kazi pale, zaidi ya kuongea na machinga kila siku....
 
Huhitaji hata kujua kusoma na kuandika kuwa DC au RC sembuse darasa la saba? Sifa za msingi, ajue kupora mali za umma na kuamrisha polisi waue waandamanaji. He is over qualified
 
JK yuko on record kwa kusema kwamba uraisi hausomewi! so the same applies to U-PM; Uwaziri, U-RC, U-DC nk. nk..........
hiyo ndio falsafa ya serikali tukufu ya CheCheMea kuhusu uongozi.
Aluta Continua!!
 
Back
Top Bottom