Darasa la saba aukwaa u-DC

Darasa la saba aukwaa u-DC

hiyo wilaya nayokwenda wasahau maendeleo. huko itakuwa ni ubabe tu!!! there wont any reasoning¬¬¬¬¬
 
Darasa la saba ni Elimu ya juu mno, kazi ya DC unatakiwa ujuwe kusoma na kuandika tu hakuna la zaidi na hawana kazi yoyote.
 
Ataweza tu, ukuu wa wilaya sikazi, kwani wilaya yetu imekaa bila mkuu wa wilaya kwa miaka 3 na hakuna tatizo, hao MADC hawana kazi hata wakigoma hakuna athari katika nchi yetu watakao athirika ni Jk, siye tunataka madaktari si uliona kasheshe ya mgomo wa madaktari? hiyo ni nafasi ya kupeana ulaji ulaji tu kama zilivyo za akina Lukuvi, Lukuvi naye darasa la saba na ni waziri wa muda mrefu na anaendelea kuchapa mzigo, kazi kubwa za vyeo vya kupeana ni umbeya na unafiki nafiki kama Lukuvi
 
Kwani huyo aliyemchagua naye si darasa la saba tu! (Kwa uwezo na upeo wake mdogo)
 
Mkulu anadai 'ukuu wa wilaya hausomewi'!

kwani uongo??? hebu tuambie chuo kinachotoa kozi ya ukuu wa wilaya, mkoa, kitongoji etc.

sana sana utasema aah..si unasomea uongozi, kwani katika wilaya kuna uongozi gani? kila eneo wapo wataalamu wenye kufanya kazi kwa taaluma zao.

ndiyo sababu ss tunasema kama kweli serikali inataka kupunguza matumizi yake, basi lazima ifanze mabadiliko ya makubwa ya msingi na ki-mkakati ikiwemo kuondoa baadhi ya nafasi za kiutawala.

kwanini uwe na DC, DAS, Mganga Mkuu wa Wilaya, Mhasibu wa Wilaya, Mhandisi wa Wilaya, Ofisa...wa wilaya na bado bureucracy hiyo ikajirudie tena katika ngazi ya mkoa...wanafanya nini watu wote hao????

Jenerali Ulimwengu alisema long time kwenye RAI, hii nchi iko over governed kwa msingi huo hapo juu.
 
Hapo bongo ukishakuwa kwenye system tu umewini haijalishi una elimu gani.
 
Anatoka BGMY! Sasa mlitaka nyumbani kwa mzee kusipate mgawo? Wivu acheni kule ni home, lazima nako mtu atoke tangu lini kiwango ch elimu imekuwa ni hoja zaidi ya umwenzetu.
 
mhhh. kazi kwelikweli, kama ni darasa la 7 kwelikweli atakuwa hata ung'eng'e haupandi! na ikitokea wakija wageni kutembelea wilaya yake kutoka ng'ambo atakuwa anawakimbia kama mshikaji wangu fulani ambaye ni mwenyekiti wa halmashauri na ni standard 7 lever anapatashida sana wakija wageni lazima atakula kona na kumwachia kazi makamu mwenyekiti wa halmashauri ambaye ni form 4 amsaidie kazi

Ukizingatia kuwa yake iko TOWN!
 
Mbona mgombea umakamu wa Rais kwa tiketi ya Chadema mwaka 2010 alikuwa darasa la saba?.
.
"MADARAKA HUMBADILISHA MTU, YAPATE KWANZA NDIPO TUJUE TABIA YAKO".

darasa la saba ana exposure gani? Acha kutetea mfumo usio kuwa na tija kisa mbona flani alifanya hivi. Yale yale ya posho za wabunge.............. oh mbona Tanapa wanalipwa sana hamsemi! Badilika.
 
Ndugu wana jamii katika kile kinachoonekana kulipana fadhila ndani ya serikali hii, aliyekuwa mbunge wa chalinze 2005-2010 RAMADHANI A MANENO, alishindwa vibaya kwenye kura za maoni mwaka 2010 baada ya kuwadanganya wapiga kura wake kwamba angejiendeleza kielimu,na hakufanya hivyo, mpaka anateuliwa mkuu wa wilaya ya KIGOMA elimu yake ni DARASA LA SABA_____________TAFAKARI.

Mkuu umekurupuka.
Mimi sio gamba lakini mchakato uliomtoa maneno kwenye kugombea ubunge naufahamu.
Kulitokea sintofahamu kati ya JK na maneno,maana JK ndiye haswa anayewachagulia wanachalinze wabunge(nina uhakika na hili).
Maneno alitafuna pesa fulani iliyopelekwa chalinze kwa jina la jk na sehemu ya pesa hiyo alnunua mashine za kusaga na kuamua kywapa akina mama waliojiunga kwenye vikundi na kumwomba mama salma aje kuzindua ambaye alikataa. gogoro likaanzia hapo.
Maneno elimu yake sio ya Darasa la saba. Nina uhakika na hilo kwa sababu mwaka 2004 alimaliza Diploma ya Markering CBE na niliwahi kumfundisha. Aliwahi kuji-enroll na openuniversity sijui viliishia wapi.
 
Ndugu wana jamii katika kile kinachoonekana kulipana fadhila ndani ya serikali hii, aliyekuwa mbunge wa chalinze 2005-2010 RAMADHANI A MANENO, alishindwa vibaya kwenye kura za maoni mwaka 2010 baada ya kuwadanganya wapiga kura wake kwamba angejiendeleza kielimu,na hakufanya hivyo, mpaka anateuliwa mkuu wa wilaya ya KIGOMA elimu yake ni DARASA LA SABA_____________TAFAKARI.

Nionavyo mimi hili ni jibu tosha kwa dai kongwe kuwa Wakuu wa wilaya wanaweza hata kutokuwepo na mambo yakaenda pale wilayani. Hii ni kwa sababu kuna Mkurugenzi wa Halmashauri ambaye ni mtu wa taaluma. Mkuu wa wilaya anaweza hata kuwa darasa la Nne, lakini akiweza kufanya angalau siasa za ndio mzee zinatosha kumbakisha madarakani!
 
Wilaya ya Hanang tulikuwa na Mkuu wa wilaya anaitwa Mefunya.
Huyu mzee alikuwa hajui kusoma wala kuandika.

What is the Qualificatin requirements needed to become DC?
 
Ndo maana amepelekwa KIGOMA,,,,,NO CHALLENGES OVA THERE

Mkuu acha mambo ya kuhisi. Pale Kigoma ajiharishia huyo changamoto kubwa pale ni wageni wanaokuja kwa ajili ya wakimbizi. Hebu nambie siku RC hayupo halafu jamaa ndo anakaimu u-RC! Mara wageni wanatia timu atafanyaje huyu? Hata aliyemteua HAMNAZO! Kwa nini kama ni fadhila kwa Mkw.ere mwenzie si angempa moja kati ya zile 10! Namhurumia kwa kupelekwa Kigoma atawakimbia UNHCR, WFP, UNICEF n.k.
 
Ndo maana amepelekwa KIGOMA,,,,,NO CHALLENGES OVA THERE

Mkuu acha mambo ya kuhisi. Pale Kigoma atajiharishia huyo changamoto kubwa pale ni wageni wanaokuja kwa ajili ya wakimbizi. Hebu nambie siku RC hayupo halafu jamaa ndo anakaimu u-RC! Mara wageni wanatia timu atafanyaje huyu? Hata aliyemteua HAMNAZO! Kwa nini kama ni fadhila kwa Mkw.ere mwenzie si angempa moja kati ya zile 10! Namhurumia kwa kupelekwa Kigoma atawakimbia UNHCR, WFP, UNICEF n.k.
 
Wilaya ya Hanang tulikuwa na Mkuu wa wilaya anaitwa Mefunya.
Huyu mzee alikuwa hajui kusoma wala kuandika.

What is the Qualificatin requirements needed to become DC?

Kwani Yusuph Rajab Makamba yule mwalimu mwenye kashfa ya ubakaji na baba wa naibu waziri wa mawasiliano sayansi na teknolojia,alikuwa mkuu wa mkoa, unaifahamu elimu yake?
 
mhhh. kazi kwelikweli, kama ni darasa la 7 kwelikweli atakuwa hata ung'eng'e haupandi! na ikitokea wakija wageni kutembelea wilaya yake kutoka ng'ambo atakuwa anawakimbia kama mshikaji wangu fulani ambaye ni mwenyekiti wa halmashauri na ni standard 7 lever anapatashida sana wakija wageni lazima atakula kona na kumwachia kazi makamu mwenyekiti wa halmashauri ambaye ni form 4 amsaidie kazi

Acha kututia aibu na wewe, kujua ung'eng'e siyo kuwa na elimu. Rais wa China hajui ung'eng'e, kuna nchi zinaongea kifaransa, kireno, kihispaniola, kirusi, kikorea nk lakini wana elimu iliyo waletea maendeleo. Kuna matoto madogo yako darasa la 5 humuhumu bongo kwenye shule za "Saints" yanaondoka ung'eng'e balaa, lakini hayana uelewa wa kutosha.

Kwa hiyo tofautisha lugha na uelewa wa mambo!
 
Elimu siyo tatizo. Watu wengi wanaochaguliwa na JK kushika nyadhifa serikalini, wengi hawana sifa/vigezo stahiki kwa nafasi wanazoteuliwa kuzitumikia. Mtu anaweza kuteuliwa bila hata ya kujua historia yake. Hii inafifisha heshima ya ofisi husika. Mifano halisi ni Adamu Malima, Abubakar Kimolo, Henjewele, DC wa igunga, Maige, DC aliyeteuliwa na ambaye alikuwa na kesi Mahakani. Kwa hiyo tatizo hapa siyo la wateule, bali la mamlaka ya uteuzi.
 
kwa kumbukumbu zangu ni kwamba alimaliza diploma ya akaunti CBE kati ya mwaka 2005 au 2006. kwa hiyo inawezekana labda baada ya kumaliza darasa la saba ilimchukua muda ndo akajiedeleza na masomo ya sekondari na baadae chuo jambo ambalo ni zuri
 
Back
Top Bottom