Darasa la saba aukwaa u-DC

Darasa la saba aukwaa u-DC

sioni kama kuna tatizo hapo! Huenda akafanya vizuri kuliko ambao ni graduates.
mimi sioni kama kuna tatizo kumteua darasa la 7 kuwa mkuu wa wilaya.kwani ukuu wa wilaya ni kazi?!ni kijiwe cha fadhila tu..sioni kama mkuu wa wilaya ana kazi ya kufanya zaidi ya kumpelekea mkulu uongo.hata mtu akimaliza darasa la pili bado ataumudu ukuu wa wilaya barabara!
 
Hivi hawa wasomi wetu tunaojitapa nao wamelisaidiaje Taifa letu?
 
Mbona mgombea umakamu wa Rais kwa tiketi ya Chadema mwaka 2010 alikuwa darasa la saba?.
.
"MADARAKA HUMBADILISHA MTU, YAPATE KWANZA NDIPO TUJUE TABIA YAKO".

Mbona! Achana na 'mbona' zako! Fikiria kwa wilaya ya mpakani na changamoto ilipofika nazo, hasa wakimbizi, wawekezaji na wageni wa namna nyingi, tena kwa maafisa waliokuwepo tayari wenye kujituma, unawapelekea kihiyo Kama huyo! Namhurumia sana Mkurugenzi wa Kigoma ambaye ni mweledi katika taaluma yake, msikilizaji na musk umma maendeleo. Unapompelelkea Mtu aliyeshindwa hata kura ndani ya chama chake unategemea nini? JK anataka kuwadhoofisha wana Kigoma, kwa nini asingempeleka Hugo Hugo Chalinze au Bagamoyo?
 
mhe. kanyunyu una hakika na ulichokiandika? bw. maneno alikuwa mbunge wa jimbo la chalinze katika bunge lililopita na minimum qualification ya ubunge ni elimu ya kidato cha nne, ni vipi angeukwaa ubunge bila kuwa na elimu hiyo. kumbuka huyu aligombea na omary madega kwenye kura za maoni ndani ya ccm mwaka 2005 ambaye kwa vyovyote asingenyamaza angemlipua tu maneno kama kweli ni darasa la saba. bunge lililopita mbunge pekee aliyefahamika kutokuwa na elimu ya kidato cha nne ni samwel chitalilo aliyekuwa mbunge wa buchosa. wapiga kura walimfungulia kesi ya kudanganya kuhusu elimu yake lakini kwasababu ambazo hazijulikani kesi hiyo haikufanikiwa.
Mkuu ubunge kulingana na katiba ya sasa darasa la saba wanaruhusiwa kugombea. Profesa majimarefu ni mfano tu! Labda kwenye katiba mpya tufanye marekebisho!
 
Cheo cha mkuu wa wilaya nafikiri hakiitaji elimu ya kiwango fulani maana hata job descripition haijulikani. Ni cheo ambacho general wa jeshi na coplo wa jeshi wanateuliwa cheo kimoja, darasa la saba na phd holder, retired na fresh from school wote wamo. Ukiwa tu kad، basi unafaa!
 
Hivi hawa wasomi wetu tunaojitapa nao wamelisaidiaje Taifa letu?

Lumuli Alipipi Kasyupa Mbunge wa Kyela alikuwa na masters ya kilimo toka UK;Livingstone Mwakipesile aliyekuja baadae alikuwa na Masters ya uchumi toka UK;Mbunge wetu wa sasa Dr Mwakyembe yeye ni PhD holder toka Germany;mbona lkn hawajatusadia lolote wapiga kura Kyela kutuhamasishia maendeleo zaidi ya wao wenyewe na familia zao kuishi maisha ya raha?

Kwanza tuone wasomi wetu wanatukwamua vipi kwenye umaskini ndipo tuwatenge darasa la 7!Wakati Mzee Moringe Sokoine anateuliwa kuwa PM kwa mara ya kwanza alikuwa na elimu gani?Kuna PM bora anayethubutu hata kumfikia Sokoine na usomi woa akina Pinda?
 
Ndugu wana jamii katika kile kinachoonekana kulipana fadhila ndani ya serikali hii, aliyekuwa mbunge wa chalinze 2005-2010 RAMADHANI A MANENO, alishindwa vibaya kwenye kura za maoni mwaka 2010 baada ya kuwadanganya wapiga kura wake kwamba angejiendeleza kielimu,na hakufanya hivyo, mpaka anateuliwa mkuu wa wilaya ya KIGOMA elimu yake ni DARASA LA SABA_____________TAFAKARI.

Kwani U-DC unahitaji kiwango gani cha elimu? Mimi nadhani kigezo pekee ni matakwa ya Rais ambaye ndiye "appointing authority" na ana uhuru kikatiba kuamua sifa anazoona yeye kuwa zinafaa kwa mteuliwa.
 
Ndugu wana jamii katika kile kinachoonekana kulipana fadhila ndani ya serikali hii, aliyekuwa mbunge wa chalinze 2005-2010 RAMADHANI A MANENO, alishindwa vibaya kwenye kura za maoni mwaka 2010 baada ya kuwadanganya wapiga kura wake kwamba angejiendeleza kielimu,na hakufanya hivyo, mpaka anateuliwa mkuu wa wilaya ya KIGOMA elimu yake ni DARASA LA SABA_____________TAFAKARI.

ndugu wewe ni muongo, mzushi, mnafiki na unachuki binafsi.

Ndg Ramadhani Maneno elimu yake sio darasa la saba, anashahada ya kwanza ya rasilimali watu ya Chuo cha Ustawi wa Jamii amehitimu mwaka 2009.
Kabla ya kuwa mbunge alikuwa meneja wa TRA mkoa wa Ilala akiwa na Diploma.

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, kwa uzushi huu mnaharibu utimamu wa Jukwaa hili, mnaharibu sifa ya JAMII FORUMS ambapo mwanzo ilikuwa chanzo cha taarifa nyingi nyeti zilizojaa ukweli mtupu
 
Huyu jamaa alimaliza degree ya social works mwaka 2010 pale chuo cha ustawi. Tuandike vitu baada ya kufanya utafiti. Sio kila mtu aliyeteuliwa hana uwezo. Au ulitaka uteukiwe wewe.


Ni ngumu pia kukuamini na wewe. Chuo cha ustawi ndo kipi hicho?? Kama mwaka 2005 alikuwa na elimu ya darasa la saba tu, je unataka kutuambia ndani ya miaka mitano mpk 2010 alisha qualify kujiunga na University na kusoma miaka ya kutosha kumpa degree??? Hebu rudi tena utoe muongozo
 
Ndugu wana jamii katika kile kinachoonekana kulipana fadhila ndani ya serikali hii, aliyekuwa mbunge wa chalinze 2005-2010 RAMADHANI A MANENO, alishindwa vibaya kwenye kura za maoni mwaka 2010 baada ya kuwadanganya wapiga kura wake kwamba angejiendeleza kielimu,na hakufanya hivyo, mpaka anateuliwa mkuu wa wilaya ya KIGOMA elimu yake ni DARASA LA SABA_____________TAFAKARI.

Ulishawahi kuiona Job Description ya wakuu wa wilaya? btw, una ushahidi kuthibitisha kwamba ni darasa la saba?
 
Acheni uzushi jamani, CV yake ni hii: Ni darasa la Saba mkondo A, alishakuwa Mbunge, Board member wa TANAPA na sasa DC wa miongoni mwa mikoa iliyoko nyuma kielimu Tz.

Kama hajui ung'eng'e kwenye mkutano au penye ugeni si atumie wakalimani kama inavyofanyika kwenye mikutano ya kimataifa au atumie mitambo ya kutafsiri lugha? Mimi namfagilia Ramadhani Maneno kwa cheo kisichomstahiki.

Ama kweli, kipimo cha elimu siyo madaraka wala elimu bali ni fikra ndani ya utendaji na mzimu ndani ya mfumo wa uongozi.

Namkumbuka msomi mmoja aliyesema kwamba athari za kukosa elimu hazionekani haraka. Hivi waweza kumwalika DC wa hivi kufungua mikutano ya ujirani mwema na Burundi, mashirika ya wakimbizi yaliyoko Kigoma nk kama nilivyoona kwa ma DC akina Clemence na Mongela kwa ung'eng'e wa kisomi wakifanya?

Mwenzangu! ukimkuta tena mwenyekiti wa Halmashauri ya Kigoma wa elimu ya darasa la pili 2 utazimia na BP kupanda mithili ya kukwea Mlima Kilimanjaro. Huuni mtihani kwa wana migebuka na mawese
 
Hao ni sekretari wa CCM katika ngazi ya wilaya ndo maana kazi za magamba katika levo zote za utawala zinayumba angalia Dr Kadeghe ameshindana na Anna Kilango miaka 10 sasa ameshindwa. Ameacha kufundisha UDSM ili afanye kazi hii isiyo na maana. Pia ni mmiliki wa Perfect Vision Sekondari pale Ubungo na sijui atasimamiaje kazi zake na utajiri wake.
 
mhe. kanyunyu una hakika na ulichokiandika? bw. maneno alikuwa mbunge wa jimbo la chalinze katika bunge lililopita na minimum qualification ya ubunge ni elimu ya kidato cha nne, ni vipi angeukwaa ubunge bila kuwa na elimu hiyo. kumbuka huyu aligombea na omary madega kwenye kura za maoni ndani ya ccm mwaka 2005 ambaye kwa vyovyote asingenyamaza angemlipua tu maneno kama kweli ni darasa la saba. bunge lililopita mbunge pekee aliyefahamika kutokuwa na elimu ya kidato cha nne ni samwel chitalilo aliyekuwa mbunge wa buchosa. wapiga kura walimfungulia kesi ya kudanganya kuhusu elimu yake lakini kwasababu ambazo hazijulikani kesi hiyo haikufanikiwa.

Ni Katiba ya nchi ipi unazungumzia ndugu.Vigezo vya kuwa mbunge unavijua lakini ama umechangia tu kuongeza michango yako humu.Ahhhhhhh samahani kumbe siyo Mtanganyika
 
Mpe pole kigoma ndiko kwa kina ZITTO kibao,
Bora ingekuwa Bagamoyo au Kisarawe na Mkuranga:israel:
 
Mkuu unashaanga Darasa la Saba kuteuliwa kuwa DC?Mbona ushangai Profesa kuchakuliwa kuwa Waziri asiyekuwa na wizara maalumu!
Ukishaa staajabu ya Mussa utayaona ya Firauni!
 
Lumuli Alipipi Kasyupa Mbunge wa Kyela alikuwa na masters ya kilimo toka UK;Livingstone Mwakipesile aliyekuja baadae alikuwa na Masters ya uchumi toka UK;Mbunge wetu wa sasa Dr Mwakyembe yeye ni PhD holder toka Germany;mbona lkn hawajatusadia lolote wapiga kura Kyela kutuhamasishia maendeleo zaidi ya wao wenyewe na familia zao kuishi maisha ya raha?

Kwanza tuone wasomi wetu wanatukwamua vipi kwenye umaskini ndipo tuwatenge darasa la 7!Wakati Mzee Moringe Sokoine anateuliwa kuwa PM kwa mara ya kwanza alikuwa na elimu gani?Kuna PM bora anayethubutu hata kumfikia Sokoine na usomi woa akina Pinda?

Malafyale.
Good Analysis...
 
Last edited by a moderator:
Sifa pekee katika nafasi za uongozi wa kisiasa ukiondoa URAIS ni kujua kusoma na kuandika kiswahili! Sasa kama sifa hii anayo anastahili kuwa M/kiti wa kijiji hadi M/kiti wa Taifa wa CCM; anastahili kuwa diwani, katibu tarafa, mbunge , mkuu wa wilaya na hata kuwa mkuu wa mkoa!
 
Back
Top Bottom