Safi sana Zitto.. Umeshtuka mapema......hawa jamaa ni wauaji siku izi..Ndo taarifa zinavyodai...
======
TAARIFA KWA UMMA
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, ndugu Zitto Kabwe amekamatwa na Polisi muda huu uwanja wa ndege wa JNIA, Dar es Salaam wakati akitoka Kigoma.
Kwa sasa wanasheria wa chama wanafuatilia kujua sababu za kukamatwa kwake.
Abdallah Khamis
Afisa Habari - ACT Wazalendo
======
UPDATE:
Zitto atasafirishwa kwenda Dodoma kesho tayari kwa kuhojiwa na Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amethibitisha kukamatwa kwa mbunge huyo.
UPDATE 2:
Polisi wanasema madereva wametoka Dodoma usiku huu na gari la Bunge na wanatarajiwa kuingia saa nane Usiku. Zitto kasema haendi na gari Dodoma kwa madereva waliokuja usiku kwani hawaamini kama hawana ndege, yeye yupo tayari kulipa gharama lakini haendi na gari.
Petro E. Mselewa Dragoon. karibuni huku mtuambieJamaa si huwa anajigamba anandumba hakamatiki? Au wazee wa Dom na Kigoma wanapimana nguvu, ile nyumba inaweza ikawa imeunguza ndunguli muhimu sana.
WASIOwanaojulikanaduh !aliwah sema akitaka kushikwa atashikwa nadhan leo AMETAKA
Yaani kuna vitu vinafanyika ata mtoto mdogo anaweza kushangaa imebaki mwanafunzi akiwa suspension skul cku ya kurudi badala ya kuja na mzazi watakuwa wanatumwa polisi ndo tz yetu tunakoelekeaMnaojua Sheria hvi kuitwa kwenye Kamati ni lazma ukamatwe na Polis?
Hizi nguvu zingeelekezwa kwe maendeleo tungekuwa ChinaInatumika nguvu kiasi unaweza kufikiri anatafutwa jangili
kipaumbele No. 1 Kamata Sweka ndani. inchi ya VIWONDERSahhaa na tulivyo mioga !
Itatokea ajali ya kupangwaKwanini hatak kusafiri na gari
swali tafakarishi
No simwamini saana huyo Bwn.Siku za hivi karibuni Zitto amebadilika naona atakuwa ameamua kukinywea kikombe wanachokinywea wapinzani wenzake hasa baada ya CCM kutokumjali kama awali.
Safar hii wamemdaka zito au tunguli zake pia zimeungua kigoma