SILENT WHISPER
JF-Expert Member
- Jun 26, 2009
- 2,209
- 821
GT hilo la Mlimani city movie theatre umeme kukatika naona ni mpya
Check out how dar village will look like...!
du umeona panya kwenye cinema!!!ata mimi nimeona panya mlimani city cinema!! lol
kwani alikuwa anajenga kutumia hela zake au mkopo???so far nasikia majani yanaota na walinzi hawajalipwa huu mwezi wa pili
hawa ndio the so called LOCAL INVESTORS
i do not think dar village will evet come up! the owner i hear one ZADOCK is in big shit and lost 3much money in advertising..he is a nut............
Of course kila mtu anajua kuwa kulitokea uhuni wao kupata ile sehemu na nashangaaa kwa nini wasingepewa maeneo kama kule Pugu wakaweza investment kubwa kama ile...wangejenga retail park nzuri na ardhi kubwa lakini wajanja na mafisadi kule serikalini wakaamua kuinyanganya serikali kiwanja na bila aibu viongozi wakuu serikalini washapalekwa pale kama kuendorse hiyo project
Haya tukubali ndio washaiba, mbona hawa jamaa hawamalizi huo ujenzi tujue moja? Maana bila kukuongopea wale wanaojenga/waliojenga kule milimani City naona walichukua ramani za shule na designs za correctional facilities za ulaya wakaenda kuzipeleka pale na lile jumba a cinema kila wakati umeme unakatika...bila kusahau Panya ambao nishawaona pale
who knows maybe Dar Village might bring vibe tofauti mjini lakini sijui waliotoa vibali kujenga pale kama walizingatia traffic kubwa itakayokwenda pale maana sisi pia ni ovyo kwenye hilo la traffic management
Mara tu zile pesa alizoahidi muungwana kuwa zitakwenda TIB zikiingia, utaona mjengo utakavyokwenda kasi! Inangojewa yule jamaa aliyefaciltate EPA kule BOT[Peter Noni] azoee ofisi pale TIB ndio waanze kuchota pamoja na za uchaguzi wa CCM!
Kwa ninavyofahamu hakuna mfanyabiashara ambaye hapati hasara, kwa Zadock kusuasua katika ujenzi wa Dar Village hilo sidhani kama ni tatizo kwani ni majengo mangapi ambayo yanajengwa na hayakamiliki katika wakati muafaka, lazima kutakuwa na sababu ya msingi maana lengo ni kuwekeza na kukamilisha mradi kwa wakati muafaka ili kupata faida na mengineo.
Huyu ni miongoni mwa wajasiriamali Watanzania waliothubutu kuwekeza na kutumia fursa mbalimbali zilizopo hapa nchini na si kukaa pembeni na kulalamika na kuwa kama mashabiki wa mpira badala ya wachezaji, hivyo anastahili kila aina ya ushirikiano na ushauri wa namna gani ajikwamue katika matatizo aliyonayo na si kumponda.
Kwa sisi wana JF kulalamika na kuponda haisadii sana wakati mwingine tuwaunge mkono watu kama hawa. Tusisahau kwa mlolongo wa kampuni za Zadock kama vile ZEK Properties, A1 OUTDOOR, ZK PR, ZK ADVERTISING, Intergrated Communications na nyingine ametoa ajira kwa watanzania wengi.
Mimi namfahamu vizuri jinsi gani huyu bwana anatoa fursa kwa watanzania mbalimbali ambao wanafanya kazi katika kampuni zake, kwa kweli ana uzalendo na hana mtizamo mbaya juu ya nchi yake kama wengi mnavyofikiria. Kuna wakati aliwahi kumtoa Mkenya kwenye nafasi ya Mtendaji Mkuu katika moja wapo ya kamouni zake na akampa Mtanzania lakini matokeo yake huyo mtanzania alichemsha, sasa hapa wa kumlaumu nani?
Mradi wa Dar Village ni mradi ambao ni endelevu na hata kama lengo la kufungua MAY halikukamilika hilo si tatizo, kwani hata sisi huwa tuna melengo mbalimbali lakini mara nyingine huwa hayakamilki kwa wakati tuliotegemea sasa cha kushangaa Dar Village kutokukamilika ni nini?
Ni kweli kuwa Huyu bwana kunawakati alihamishia makao makuu Joberg, sasa kwa mtizamo wangu hili ni jambo jema na zuri sana kwani mfanyabiashara yeyote ni lazima aangalie wapi kuna fursa za kufanya biashara na la msingi hata akipata pesa ndio kama hivyo anakuja kuwekeza nchini kwake na vijana na watotoo wetu wanapata ajira.
Kwa sasa hivi huyu bwana ni kweli mambo yake hayaendi vizuri kwa sababu mteja wake mkubwa ni kampuni ya ZAIN ambayo inampa biashara katika kampuni zake za matangazo, pr, outdoor advertising, sasa hawa ZAIN walikata bajeti zao kwa asilimia 50% kukabiliana na mtikisiko wa uchumi, na jambo hili lilimuathiri sana kimapato kiasi kwamba ilibidi pia apunguze idadi ya wafanyakazi katika kampuni zake.
Jambo hili ni la kawaida kabisa katika biashara na kwa mtu kama yeye ni lazima ajipange ili kampuni zake zisife na watu wengine waendelee kupata ajira na yeye aendelee kulipa kodi mbalimbali serikalini, bila shaka lengo la mfanyabiashara ni kupata faida lakini pia lazima aangalie pia asije kufunga kampuni zote na akakosa yote.
Zadock amejitahidi sana kwa kweli maana alipotoka ni mbali tangu enzi za kupiga picha, wale vijana wa tazara watakuwa wanamjua, kwa msukosuko huu tumeona nchi nyingine matajiri wanajiua na mambo mengineo lakini MWANAUME HUKIMBII MATATIZO, HONGERA SANA ZADOCK...
unalijua wewe mimi silijui nilichoandika nakijua na wala sina nia ya kuprovokebe caferul of what you wish for au ndio unataka kuprovoke watu wamweke wazi huyu ZADOCK kisha uje kulalama kuwa ohhh mmekuwa personal..?
hiyo ya pesa za TIB mbona hujaligusa?