Dar: TRL yabomoa nyumba kadhaa eneo la Buguruni

Dar: TRL yabomoa nyumba kadhaa eneo la Buguruni

Ukweli usiofichika ni kwamba hii hali inaumiza, lakini inatakiwa kuwa fundisho kwetu watanzania kwa kujenga maeneo rasmi ili kuepuka maumivu haya, tunajifunza kutokana na makosa yetu.
 
Tatizo sisi Watanzania tumezoea mitelemko, wewe mwenyewe na akili zako unaenda unajenga karibu na vyanzo vya maji,juu kuna nyaya za umeme za 33KV au zaidi, ifadhi ya barabara, ifadhi ya reli ...unakuja unabomolewa unailaumu serikali au anataka fidia je ulitumwa akajenge hapo??
wengine wakisikia kuna mradi sehemu wanavamia ardhi ..ili baadae waje wilipwe fidia....kuna watu walifanya fojali kigamboni now viwanja vimewadodea. watanzania tunakiwa tubadilike

Unanikumbusha Arusha, watu kusikia tu kwamba kuna barabara ya EAC itapita huku, jamaa zetu wa mkoa jirani wakavamia kununua pori na mashamba bila kujua mwisho wake ni upi. sasa hivi ukiwauliza, wanang'ara macho tu.
 
kweli wamekosea na inawezekana waliujua hata mwisho wao lakini hawakutegemea kuwa ingeweza kutokea kwa kuwa tulishazoea maisha ya mazoea na kuonewa huruma hatatunapovunja sheria.
poleni kwa kuwa wengi wenu huenda hayo maeneo mliuziwa na hamkujua hayo!
lakini pole hazitoshi letu ni kuomba serikali ya ilala ifikirie ni kwa jinsi gani iwasaidie katika wakati huu mgumu ikiwa ni pamoja na kuwapa viwanja na msaada wa dharura.
 
Nashauri watu wapime ardhi zao hata kama mmejenga kihorela mnaweza kupima ila kwa,, watu 30 au 40 mliokaa sehemu 1 mnajikusanya mnapima eneo lenu gharama huwa ni ndogo sana mkiwa wengi kwenye hifadhi za barabara au reli mtaalam anajua ataacha mita ngapi,,, nashauri watu wote mpime hata kabla hujanunua eneo nenda na mtaalam atakuwa na kifaa cha kuchukua coordinates ili ajue eneo Hilo ni ni la matumiz gani,,
 
Duuuh,,serikali haiko kwa ajili ya kuwaliza wananchi wake
 
Back
Top Bottom