Dar: TRL yabomoa nyumba kadhaa eneo la Buguruni

Dar: TRL yabomoa nyumba kadhaa eneo la Buguruni

Tatizo sisi Watanzania tumezoea mitelemko, wewe mwenyewe na akili zako unaenda unajenga karibu na vyanzo vya maji,juu kuna nyaya za umeme za 33KV au zaidi, ifadhi ya barabara, ifadhi ya reli ...unakuja unabomolewa unailaumu serikali au anataka fidia je ulitumwa akajenge hapo??
wengine wakisikia kuna mradi sehemu wanavamia ardhi ..ili baadae waje wilipwe fidia....kuna watu walifanya fojali kigamboni now viwanja vimewadodea. watanzania tunakiwa tubadilike
Mwenye shibe hamjui mwenye njaa.
Bravo Cheepkiz
 
Ndio kujenga kwenye eneo la reli? Chama gani kinaruhusu?
Hakuna anayeruhusiwa kujenga eneo la reli kama isivyoruhusiwa kutumia vyeti fake au visivyo vyako kuajiriwa.
Ndio maana wanaoona mbele zaidi walishauri wazo la kuwa na tume ya ukweli na maridhiano.
Hebu angalia tz ya sasa:
- karibia 70% ya kipato ni 'wapiga dili'.
- zaidi ya 70% ya ujenzi ni sehemu zisizopimwa
- asilimia 50% ya elimu ni vyeti fake au vya kuiba
- msingi wa nchi yoyote ni familia na zaidi ya 65% ya ndoa tz zinajihusisha na michepuko.
Je, ni sahihi kudanganyana hapa kuwa unaweza kujenga nchi bila kurekebisha haya na mengineyo!? Maana hata anayevunja naye unakuta kajenga kusikoruhusiwa, kwani hata AZAM walivyopanua pale hawajaingilia eneo la TRL!?
 
Kura za ubunge za jimbo hili ziligawanyika kwa watu watatu yaani cdm, cuf na ccm walioshinda. Ukijumlisha kura za cuf na cdm kwa pamoja zilikuwa myingi kuzidi za ccm lakini katika principle ya simple majority ccm wakashinda!
Sasa siwezi kujua hapa ni nani anasomeshwa namba na ukweli kwa sasa familia nyingi hazina uhakika wa hata kula mlo mmoja hivyo shelter pekee ndio ilikuwa tumaini lililobakia. Kubomoa na nyumba si ajabu tukasikia tena tukio kama la mfanyabiashara wa vinywaji wa Dodoma!
Bomoa ili tuwe na miundo mbinu mizuri
 
Safi sana..Tuendelee kuiombea serikali hasa Rais wetu.Hakika kwake kila mtanzania atanyooka.
 
Kura za ubunge za jimbo hili ziligawanyika kwa watu watatu yaani cdm, cuf na ccm walioshinda. Ukijumlisha kura za cuf na cdm kwa pamoja zilikuwa myingi kuzidi za ccm lakini katika principle ya simple majority ccm wakashinda!
Sasa siwezi kujua hapa ni nani anasomeshwa namba na ukweli kwa sasa familia nyingi hazina uhakika wa hata kula mlo mmoja hivyo shelter pekee ndio ilikuwa tumaini lililobakia. Kubomoa na nyumba si ajabu tukasikia tena tukio kama la mfanyabiashara wa vinywaji wa Dodoma!
Tufanya nini mkuu na standard gauge inapita?
 
Duu poleni aisee
Yaan hapo life inaanza upyaaa haijalishi una maiden unasomesha!!!!!
Mungu awape uvumilivu

Nasikia na Moro nako wako njiani kuja kwa waliojenga kwenye hifadhi ya barabara


Lakn je hiki kisu kinakata kote kote!!!!!!
 
Omba Mungu sana kumbuka waliojenga walisukumwa na umaskini na sio maamuzi yao binafsi
Mfumo wa kibepari hauna huruma kwa maskini. So watu wasikumbatie Umaskini kama tunusuru. Ni lazima wafanye kazi tena kwa bidii sana vinginevyo wataishia jela tu hakuna namna.
 
Mfumo wa kibepari hauna huruma kwa maskini. So watu wasikumbatie Umaskini kama tunusuru. Ni lazima wafanye kazi tena kwa bidii sana vinginevyo wataishia jela tu hakuna namna.
Tanzania inafuata siasa za kibepari au siasa za ujamaa na kujitegemea
 
Zaidi ya nyumba 200 zabomolewa katika eneo la Tazara DSM kupisha ujenzi wa reli ya kisasa inayotarajiwa kujengwa hapo baadae ktk eneo hilo.
 
Halafu maskini mjini unafuata nini?si Ukae huko UBENA ZOMOZI ufuge kuku wa kienyeji na kulima mananasi!!!!
Aisee napitia comments zako ila huwa naamini usimseme mwenzio vibaya sababu ndo maana wanasema hujafa hujaumbika au mwenzio akinyolewa zako tia maji si vizuri kuropoka hata kama walikosea sababu hakuna ajuaye kesho itakuwaje unaweza na wewe ukaadhibiwa kwa njia yoyote ile labda kama wewe unaishi kwenu unakula na kwenda toilet bure hapo hutaona uchungu wanaopata wenzako kuwa makini
 
Back
Top Bottom