BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,416
- 8,201
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imemkuta na kesi ya kujibu aliyekuwa mke wa mfanyabiashara wa madini mkoani Arusha, marehemu Erasto Msuya, maarufu kwa jina la Bilionea Msuya, Miriam Mrita, anayetuhumiwa kumuua wifi yake, Aneth.
Mbali na Mrita mshtakiwa mwingine aliyekutwa na kesi ya kujibu ni mfanyabiashara Revocatus Muyela. Wamedai kuwa watapeleka mashahidi na vielelezo kuthibitisha tuhuma hizo dhidi yao na pia watajitetea kwa kiapo.
Uamuzi huo mdogo ulitolewa na Jaji Edwin Kakolaki wa mahakama hiyo, baada ya upande wa mashtaka kufunga kesi kwa mashahidi 25 na vielelezo mbalimbali kikiwamo kisu ambacho kinadaiwa kilitumika kumchinjia Aneth koromeo.
Jaji Kakolaki alisema mahakama baada ya kuzingatia ushahidi na vielelezo vilivyotolewa, imejiridhisha kwamba kuna kesi ya msingi ambayo inawatosheleza washtakiwa wajitetee kama sheria inavyotaka.
"Washtakiwa simameni, kwa mujibu wa kifungu 293 (2) na (a) (b) na cha (3) mahakama inawafahamisha pamoja na haki zenu nilizokwisha waeleza na pia mawakili wenu watawaelewesha kama mtakuwa hamjaelewa vizuri.
NIPASHE
Mbali na Mrita mshtakiwa mwingine aliyekutwa na kesi ya kujibu ni mfanyabiashara Revocatus Muyela. Wamedai kuwa watapeleka mashahidi na vielelezo kuthibitisha tuhuma hizo dhidi yao na pia watajitetea kwa kiapo.
Uamuzi huo mdogo ulitolewa na Jaji Edwin Kakolaki wa mahakama hiyo, baada ya upande wa mashtaka kufunga kesi kwa mashahidi 25 na vielelezo mbalimbali kikiwamo kisu ambacho kinadaiwa kilitumika kumchinjia Aneth koromeo.
Jaji Kakolaki alisema mahakama baada ya kuzingatia ushahidi na vielelezo vilivyotolewa, imejiridhisha kwamba kuna kesi ya msingi ambayo inawatosheleza washtakiwa wajitetee kama sheria inavyotaka.
"Washtakiwa simameni, kwa mujibu wa kifungu 293 (2) na (a) (b) na cha (3) mahakama inawafahamisha pamoja na haki zenu nilizokwisha waeleza na pia mawakili wenu watawaelewesha kama mtakuwa hamjaelewa vizuri.
NIPASHE