Mulangila Mukuru
JF-Expert Member
- Feb 24, 2010
- 1,945
- 729
laiti kama kelele hizi
zinazopigwa sasa juu ya mauaji ya kikatili yanayofanywa na jeshi letu
tusingeweka double standards tungefanikiwa kupambana na ukatili huu pia
na kuiondoa ccm madarakani kirahisi.Nakumbuka mauaji ya Zanzibar baada
ya maandamano yalikuwa makubwa sana,idadi ya wafu ilkuwa kubwa na mali
nyingi ziliangamia lakini watanzania wakashawishiwa wayaone yale ni
tatizo la kichama cha cuf na udini wa wazanzibar ikapita, yakaja ya
morogoro watu wakaamka wakaanza piga mayowe yakapita, yakaja ya Iringa
duuh ni hatari.HIVI TUNGEANZA MAKELELE HAYA TANGU MWANZO TUNGEKUWA
TUMEFANIKIWA MAPEMA KABISA.Tatizo ni ubaguzi wa watanzania ndio
unaotumaliza! Na ngoja tuone uchaguzi ukikaribia utasikia tu hili ni
chaguo la mungu,hili lina maslahi ni dini yetu,hili linatufaa na
kadhalika!!
kwa ushuhuda niliouona Zanzibar harakati nyingi za kisiasa Zanzibar huendana na maneno ya kashfa dhidi ya ukristo na uharibifu wa makanisa tofauti na huku Bara ambapo siasa hubaki kuwa siasa na dini hukaa kado,
Ndo maana wakati mwingine inakuwa ngumu harakati za kisiasa znz kuungwa mkono na watanzania walio wengi